< Esther 9 >

1 So in the twelft moneth, which is the moneth Adar, vpon the thirteenth daye of the same, when the Kings commandement and his decree drew neere to be put in execution, in the day that the enemies of the Iewes hoped to haue power ouer them (but it turned contrary: for the Iewes had rule ouer them that hated them)
Sasa katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya kumi na tatu ambayo ni siku ya Adari, siku ambayo adui wa Wayahudi walitarajia kutekeleza sheria ya mfalme na kupata nguvu dhidi ya Wayahudi. Badala yake Wayahudi wakapata nguvu dhidi ya adui zao.
2 The Iewes gathered themselues together into their cities throughout all the prouinces of the King Ahashuerosh, to lay hande on such as sought their hurt, and no man coulde withstande them: for the feare of them fel vpon al people.
Wayahudi wote wakakusanyika katika miji yao katika majimbo yote ya Mfalme Ahusiero, kutia mikono juu ya wale waliokusudia ubaya. Hakuna aliye kuwa tayari kusimama zao kwa sababu hofu yao ilikuwa imewaangukia watu wote.
3 And all the rulers of the prouinces, and the princes and the captaines, and the officers of the King exalted the Iewes: for the feare of Mordecai fell vpon them.
Wakuu wote wa majimbo, maakida na magavana, na watawala wa mfalme, waliwasaidia Wayahudi kwa kuwa hofu ya Modekai ilikuwa imewaangukia.
4 For Mordecai was great in the kings house, and the report of him went through all the prouinces: for this man Mordecai waxed greater and greater.
Kwa kuwa Modekai alikuwa mkuu katika nyumba ya mfalme, na umaarufu wake ukasambaa katika majimbo yote, kwa kuwa Modekai alikuwa akifanyika mkuu.
5 Thus the Iewes smote all their enemies with strokes of the sworde and slaughter, and destruction, and did what they woulde vnto those that hated them.
Wayahudi wakawavamia maadi zao kwa upanga, wakiwatenda vibaya kama walivyokuwa wamekusudiwa mabaya dhidi yao Wakawatenda kama walivyo ona vyema machoni pao.
6 And at Shushan the palace slewe the Iewes and destroyed fiue hundreth men,
Katika ngome ya mji wa Shushani pekee jumla ya maadui waliouawa na na kuharibiwa na Wayahudi ni wanaume mia tano.
7 And Parshandatha, and Dalphon, and Aspatha,
Miongoni mwa waliouawa ni pamoja na Parishandatha, Dalphoni, Aspatha,
8 And Poratha, and Adalia, and Aridatha,
Poratha, Adalia, Aridatha,
9 And Parmashta, and Arisai, and Aridai, and Vaiezatha,
Parimashita, Arisai, Aridai, Vaizatha,
10 The ten sonnes of Haman, ye sonne of Ammedatha, the aduersarie of the Iewes slewe they: but they layd not their hands on the spoyle.
na wana kumi wa Hamani, mwana wa Hammedatha, adui wa Wayahudi. Lakini hawakuchua mateka yoyote.
11 On the same day came ye nomber of those that were slayne, vnto the palace of Shushan before the King.
Idadi ya wale waliouawa siku hiyo katika mji wa Shushani, ilifikishwa kwa Mfalme Ahusiero.
12 And the King sayd vnto the Queene Ester, The Iewes haue slayne in Shushan the palace and destroyed fiue hundreth men, and the ten sonnes of Haman: what haue they done in the rest of the Kings prouinces? and what is thy petition, that it may be giuen thee? or what is thy request moreouer, that it may be performed?
Mfalme akamwambia malkia Esta. Mfalme akamwambia Malkia Esta, “Wayahudi wameua wanaume mia tano katika mji wa Shushani, wakiwemo wana kumi wa Hamani adui wa Wayahudi. Je wamefanya nini katika majimbo mengine? Na sasa haja yako ni nini? Utapewa. Ombi lako ni nini?”
13 Then sayd Ester, If it please the King, let it be granted also to morow to the Iewes that are in Shushan, to do according vnto this daies decree, that they may hang vpon ye tree Hamans ten sonnes.
Esta akamjibu, “Mfalme kama ikikupendeza, ruhusu Wayuadi walio katika mji wa Shushani wapige mbiu hii na kesho, na miili ya watoto wa Hamani itundikwe juu ya miti.”
14 And the King charged to doe so, and the decree was giuen at Shushan, and they hanged Hamans ten sonnes.
Mfalme akaamuru ombi la Esta litekelezwe. Mbiu ilipigwa katika mji wa Shushani, na wana kumi wa Hamani wakatundikwa juu ya miti.
15 So the Iewes that were in Shushan, assembled themselues vpon the fourteenth day of the moneth Adar, and slew three hundreth men in Shushan, but on the spoyle they layd not their hand.
Wayahudi katika mji wa Shushani walisanyika pamoja siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na kuwaua maadui zao mia tatu katika mji wa Shushani, lakini hawakugusa nyara zao.
16 And the rest of the Iewes that were in the Kings prouinces assembled themselues, and stood for their liues, and had rest from their enemies, and slewe of them that hated them, seuentie and fiue thousand: but they layd not their hand on the spoyle.
Na Wayahudi katika majimbo mengine wakakusanyika ili kujilinda na wakapata faraja kutoka kwa maadui na wakawaua maadui zao elfu sabini na tano, lakini hawakugusa mikono yao kwa vitu vya thamani wale waliouwawa.
17 This they did on the thirteenth day of the moneth Adar, and rested the fourteenth day thereof, and kept it a day of feasting and ioy.
Katika siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari, Wayahudi wakapumzika katika siku ya kumi na nne, wakapumzika siku hiyo ya karamu na furaha.
18 But the Iewes that were in Shushan assembled themselues on the thirteenth day, and on the fourteenth therof, and they rested on the fifteenth of the same, and kept it a day of feasting and ioy.
Lakini Wayahudi walioishi katika mji wa Shushani wakaja pamoja siku ya kumi na tatu na ya kumi na nne. Na siku ya kumi na tano wakapumzika na wafanya karamu na kufurahia.
19 Therefore the Iewes of the villages that dwelt in the vnwalled townes, kept the foureteenth day of the moneth Adar with ioy and feasting, euen a ioyfull day, and euery one sent presents vnto his neighbour.
Hii ndiyo sababu Wayahudi wa vijijini, wanaishi maeneo ya vijijini, huadhimisha siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari kama siku ya furaha na karamu na siku ambayo hutumiana zawadi kwa kila mmoja.
20 And Mordecai wrote these words, and sent letters vnto all the Iewes that were through all the prouinces of the King Ahashuerosh, both neere and farre,
Modekai akaweka mambo haya na akatuma nyaraka kwa Wayahudi wote waliokuwa katika utawala wa Mfalme Ahusiero,
21 Inioyning them that they shoulde keepe the fourteenth day of the moneth Adar, and the fifteenth day of the same, euery yeere.
akiwataka kuazimisha siku ya kumi na nne na kumi na tano ya mwezi wa Adari kila mwaka.
22 According to the dayes wherein the Iewes rested from their enemies, and the moneth which was turned vnto them from sorowe to ioy, and from mourning into a ioyfull day, to keepe them the dayes of feasting, and ioy, and to sende presents euery man to his neyghbour, and giftes to the poore.
Hizi zilikuwa ndizo siku ambazo Wahudi walipata faraja kutoka kwa maadui zao na wakati huu ndio wakati ambao huzuni ya Wayahudi iligeuzwa kuwa furaha, na kutoka kwa maombolezo hadi kwenye pumziko. Walipaswa kuzifanya siku za karamu na furaha, na kutumiana zawadi ya chakula, na zawadi kwa masikini.
23 And the Iewes promised to do as they had begun, and as Mordecai had written vnto them,
Wayahudi wakaendelea na maadhimisho wakifanya kile ambacho Modekai alikuwa amewaandikia.
24 Because Haman the sonne of Hammedatha the Agagite al the Iewes aduersarie, had imagined against the Iewes, to destroy them, and had cast Pur (that is a lot) to consume and destroy them.
Na wakati huo Modekai mwana wa Hammedatha mwagagi, adui wa Wayahudi aliyekuwa amepanga njama ya kuwaangamiza Wayahudi, na kwa kupiga Puri (yaani akapiga kura) ili kuwaangamiza kabisa.
25 And when she came before the King, he commanded by letters, Let this wicked deuise (which he imagined against the Iewes) turne vpon his owne head, and let them hang him and his sonnes on the tree.
Lakini Mfalme Ahusiero alipopata taarifa ya mpango mbaya huu alioupanga Modekai dhidi ya Wayahudi, aliagiza kwa nyaraka afanyiwe Modekai mwenyewe, na kwamba yeye na wana wake wanyongwe juu ya miti.
26 Therfore they called these dayes Purim, by the name of Pur, and because of all the wordes of this letter, and of that which they had seene besides this, and of that which had come vnto them.
Hivyo Wayahudi wakaziita siku hizi Purimu, kutokana na jina Puri. Kwa sababu ya mambo yote yaliyo kuwa yameandika katika barua, na mambo yote ambayo walikuwa wameyaona kwa macho yao, na yale yalikuwa yamewapata,
27 The Iewes also ordeined, and promised for them and for their seede, and for all that ioyned vnto them, that they would not faile to obserue those two dayes euery yeere, according to their writing, and according to their season,
Wayahudi wakapokea jukumu na desturi mpya. Desturi hii iwe kwa ajili yao, watoto wao, na kila ambaye aliyeungana nao. Na itakuwa kwamba maadhimisho haya watayafanya kwa kila mwaka. Wataadhimisha kwa namna fulani na nyakati hizo hizo kila mwaka.
28 And that these dayes shoulde be remembred, and kept throughout euery generation and euery familie, and euery prouince, and euery citie: euen these daies of Purim should not faile among the Iewes, and the memoriall of them should not perish from their seede.
Siku hizi zilipaswa kuadhimishwa katika kila kizazi, kila familia, kila jimbo na kwa kila mji. Wayahudi hawa na watoto wao hawakuacha kuadhimisha siku hizi za Purimu, ili kwamba wasizisahau.
29 And the Queene Ester ye daughter of Abihail and Mordecai the Iew wrote with al authoritie (to cofirme this letter of Purim ye second time)
Malkia Esta na Modekai wakaandika kwa mamlaka yote na kuthibitisha barua hii ya pili kuhusu Purimu.
30 And he sent letters vnto al the Iewes to the hundreth and seuen and twentie prouinces of the kingdome of Ahashuerosh, with words of peace and trueth,
Barua zilipelekwa katika majimbo 127 ya mfalme Ahusiero, zikiwatakia Wayahudi wote amani na kweli.
31 To confirme these dayes of Purim, according to their seasons, as Mordecai the Iewe and Ester the Queene had appointed them, and as they had promised for them selues and for their seede with fasting and prayer.
Na kuthibitisha siku za Purimu sawa sawa na maelekezo ya Modekai na Esta yaliyowataka Wayahudi waadhimishe. Wayahudi wakatii maagizo kwa ajili yao na uzao wao, kama walivyotii siku za kufunga na kuomboleza.
32 And the decree of Ester confirmed these words of Purim, and was written in the booke.
Agizo la Esta likahakikisha sheria hizi kuhusu Purimu, na ikaandikwa katika kitabu.

< Esther 9 >