< 2 Corinthians 6 >

1 So we therefore as workers together beseech you, that ye receiue not the grace of God in vaine.
Na kwa hiyo, kufanya kazi pamoja, tunawasihi ninyi msiipokee neema ya Mungu pasipo matokeo.
2 For he sayth, I haue heard thee in a time accepted, and in the day of saluation haue I succoured thee: beholde nowe the accepted time, beholde nowe the day of saluation.
Kwa kuwa anasema, “Wakati uliokubalika nilikuwa makini kwenu, na katika siku ya wokovu niliwasaidia.” Tazama, sasa ni wakati uliokubalika. Tazama, sasa ni siku ya wokovu.
3 We giue no occasion of offence in any thing, that our ministerie shoulde not be reprehended.
Hatuweki jiwe la kizuizi mbele ya mtu yeyote, kwa kuwa hatuitakii huduma yetu iletwe katika sifa mbaya.
4 But in all things we approue our selues as the ministers of God, in much patience, in afflictions, in necessities, in distresses,
Badala yake, tunajihakiki wenyewe kwa matendo yetu yote, kwamba tu watumishi wa Mungu. Tu watumishi wake katika wingi wa ustahimilivu, mateso, dhiki, ugumu wa maisha,
5 In stripes, in prisons, in tumults, in labours,
kupigwa, vifungo, ghasia, katika kufanya kazi kwa bidii, katika kukosa usingizi usiku, katika njaa,
6 By watchings, by fastings, by puritie, by knowledge, by long suffering, by kindnesse, by the holy Ghost, by loue vnfained,
katika usafi, maarifa, uvumilivu, wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo halisi.
7 By the worde of trueth, by the power of God, by the armour of righteousnesse on the right hand, and on the left,
Tu watumishi wake katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu. Tuna silaha ya haki kwa ajili ya mkono wa kuuume na wa kushoto.
8 By honour, and dishonour, by euill report, and good report, as deceiuers, and yet true:
Tunafanya kazi katika heshima na kudharauliwa, katika kashfa na sifa. Tunatuhumiwa kuwa wadanganyifu na wakati tu wakweli.
9 As vnknowen, and yet knowen: as dying, and beholde, we liue: as chastened, and yet not killed:
Tunafanya kazi kana kwamba hatujulikani na bado tunajulikana vizuri. Tunafanya kazi kama wanaokufa na -Tazama! - bado tunaishi. Tunafanya kazi kama tunaoadhibiwa kwa ajili ya matendo yetu lakini sio kama waliohukumiwa hata kufa.
10 As sorowing, and yet alway reioycing: as poore, and yet make many riche: as hauing nothing, and yet possessing all things.
Tunafanya kazi kama wenye masikitiko, lakini siku zote tuna furaha. Tunafanya kazi kama maskini, lakini tunatajirisha wengi. Tunafanya kazi kana kwamba hatupati kitu bali kama tunaomiliki kila kitu.
11 O Corinthians, our mouth is open vnto you: our heart is made large.
Tumezungumza ukweli wote kwenu, Wakorintho, na mioyo yetu imefunguka kwa upana.
12 Ye are not kept strait in vs, but ye are kept strait in your owne bowels.
mioyo yenu haizuiliwi na sisi, bali mnazuiliwa na hisia zenu wenyewe.
13 Nowe for the same recompence, I speake as to my children, Be you also inlarged.
Sasa katika kubadilishana kwa haki - ninaongea kama kwa watoto - fungueni mioyo yenu kwa upana.
14 Be not vnequally yoked with the infidels: for what fellowship hath righteousnesse with vnrighteousnesse? and what communion hath light with darkenesse?
Msifungamanishwe pamoja na wasioamini. Kwa kuwa kuna uhusiano gani kati ya haki na uasi? Na kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
15 And what concord hath Christ with Belial? or what part hath the beleeuer with the infidell?
Ni makubaliano gani Kristo anaweza kuwa nayo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na asiyeamini?
16 And what agreement hath the Temple of God with idols? for ye are the Temple of the liuing God: as God hath said, I will dwell among them, and walke there: and I will be their God, and they shalbe my people.
Na kuna makubaliano gani yapo kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi ni hekalu la Mungu aliye hai, kama ambavyo Mungu alisema: “Nitakaa kati yao na kutembea kati yao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
17 Wherefore come out from among them, and separate your selues, saith the Lord, and touch none vncleane thing, and I wil receiue you.
Kwa hiyo, “Tokeni kati yao, na mkatengwe nao,” asema Bwana. “Msiguse kitu kichafu, na nitawakaribisha ninyi.
18 And I will be a Father vnto you, and ye shalbe my sonnes and daughters, saith the Lord almightie.
Nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu wa kiume na wa kike,” asema Bwana Mwenyezi.

< 2 Corinthians 6 >