< Ephesians 4 >

1 I therefore, being prisoner in the Lord, praie you that yee walke worthie of the vocation whereunto yee are called,
Kwa hiyo, kama mfungwa kwa ajili ya Bwana, nawasihi mtembee sawasawa na wito ambao Mungu aliwaita.
2 With all humblenesse of minde, and meekenesse, with long suffering, supporting one an other through loue,
Muishi kwa unyenyekevu mkuu na upole na uvumilivu. Mkichukuliana katika upendo.
3 Endeuouring to keepe the vnitie of the Spirit in the bond of peace.
Fanyeni bidii kuutunza umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 There is one body, and one Spirit, euen as yee are called in one hope of your vocation.
Kuna mwili mmoja na Roho moja, kama ambavyo pia mlikuwa mmeitwa katika uhakika wa taraja moja la wito wenu.
5 There is one Lord, one Faith, one Baptisme,
Na kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
6 One God and Father of all, which is aboue all, and through all, and in you all.
na Mungu mmoja na Baba wa wote. Yeye yuko juu ya yote, na katika yote na ndani ya yote.
7 But vnto euery one of vs is giuen grace, according to the measure of the gift of Christ.
Kwa kila mmoja wetu amepewa kipawa kulingana na kipimo cha kipawa cha Kristo.
8 Wherfore he saith, Whe he asceded vp on hie, he led captiuity captiue, and gaue gifts vnto men.
Ni kama maandiko yasemavyo: “Alipopaa juu sana, aliongoza mateka katika utumwa. Akatoa vipawa kwa watu.”
9 (Nowe, in that hee ascended, what is it but that he had also descended first into the lowest partes of the earth?
Ni nini maana ya, “Alipaa,” isipokuwa kwamba alishuka pia pande za chini za dunia?
10 Hee that descended, is euen the same that ascended, farre aboue all heauens, that hee might fill all things)
Yeye ambaye alishuka ni mtu yuleyule ambae pia alipaa mbali juu ya mbingu zote. Alifanya hivi ili uwepo wake uwe katika vitu vyote.
11 Hee therefore gaue some to be Apostles, and some Prophets, and some Euangelists, and some Pastours, and Teachers,
Kristo alitoa vipawa kama hivi: mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji, na waalimu.
12 For the repairing of the Saintes, for the woorke of the ministerie, and for the edification of the bodie of Christ,
Alifanya hivi kuwawezesha waumini kwa ajili ya kazi ya huduma, kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo.
13 Till we all meete together (in the vnitie of faith and that acknowledging of the Sonne of God) vnto a perfite man, and vnto the measure of the age of the fulnesse of Christ,
Anafanya hivi hadi sisi sote tufikie umoja wa imani na maarifa ya mwana wa Mungu. Anafanya hivi hadi tuweze kukomaa kama wale waliofikia kimo kamili cha Kristo.
14 That we henceforth be no more children, wauering and caried about with euery winde of doctrine, by the deceit of men, and with craftines, whereby they lay in wait to deceiue.
Hii ni ili kwamba tusiwe tena kama watoto, tusirushwerushwe huku na huko. Ili kwamba tusichukuliwe na kila aina ya upepo wa fundisho, kwa hila za watu katika ujanja wa udanganyifu uliopotoka.
15 But let vs folowe the truth in loue, and in all things, grow vp into him, which is the head, that is, Christ.
Badala yake, tutaongea ukweli katika upendo na kukua zaidi katika njia zote ndani yake ambaye ndiye kichwa, Kristo.
16 By whome al the body being coupled and knit together by euery ioynt, for ye furniture therof (according to the effectual power, which is in the measure of euery part) receiueth increase of the body, vnto the edifying of itselfe in loue.
Kristo ameunganisha, kwa pamoja, mwili wote wa waumini. Umeungamanishwa pamoja na kila kiungo ili kwamba mwili wote ukue na kujijenga wenyewe katika upendo.
17 This I say therefore and testifie in the Lord, that yee hencefoorth walke not as other Gentiles walke, in vanitie of their minde,
Kwa hiyo, nasema hili, na nawasihi katika Bwana: Msitembee tena kama watu wa mataifa wanavyotembea katika ubatili wa akili zao.
18 Hauing their vnderstanding darkened, and being strangers from the life of God through the ignorance that is in them, because of the hardnesse of their heart:
Wametiwa giza katika mawazo yao. Wamefukuzwa kutoka katika uzima wa Mungu kwa ujinga ulio ndani yao kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao.
19 Which being past feeling, haue giuen themselues vnto wantonnesse, to woorke all vncleannesse, euen with griedinesse.
Hawajisikii aibu. Wamejikabidhi wenyewe kwa ufisadi katika matendo machafu, katika kila aina ya uchoyo.
20 But yee haue not so learned Christ,
Lakini, hivi sivyo mlivyojifunza kuhusu Kristo.
21 If so be yee haue heard him, and haue bene taught by him, as the trueth is in Iesus,
Nadhani kwamba mmesikia kuhusu yeye. Nadhani kwamba mmekuwa mkifundishwa katika yeye, kama tu ukweli ulivyo ndani ya Yesu.
22 That is, that yee cast off, concerning the conuersation in time past, that olde man, which is corrupt through the deceiueable lustes,
Lazima mvue mambo yote yanayoendana na mwenendo wenu wa zamani, utu wa zamani. Ni utu wa zamani unaooza kwa sababu ya tamaa za udanganyifu.
23 And be renued in the spirit of your minde,
Vueni utu wenu wa zamani ili kwamba mfanywe upya katika roho ya akili zenu.
24 And put on ye new man, which after God is created vnto righteousnes, and true holines.
Fanyeni hivi ili muweze kuvaa utu mpya, unaoendana na Mungu. Umeumbwa katika haki na utakatifu wa kweli.
25 Wherefore cast off lying, and speake euery man truth vnto his neighbour: for we are members one of another.
Kwa hiyo, weka mbali udanganyifu. “Ongeeni ukweli, kila mmoja na jirani yake,” kwa sababu tu washirika kwa kila mmoja kwa mwenzake.
26 Bee angrie, but sinne not: let not the sunne goe downe vpon your wrath,
Mwe na hasira, lakini msitende dhambi.” Jua lisizame mkiwa katika hasira zenu.
27 Neither giue place to the deuill.
Msimpe Ibilisi nafasi.
28 Let him that stole, steale no more: but let him rather labour, and worke with his handes the thing which is good, that hee may haue to giue vnto him that needeth.
Yeyote aibaye lazima asiibe tena. Badala yake ni lazima afanye kazi. Afanye kazi yenye manufaa kwa mikono yake, ili kwamba aweze kumhudumia mtu aliye na hitaji.
29 Let no corrupt comunication proceed out of your mouths: but that which is good, to ye vse of edifying, that it may minister grace vnto the hearers.
Kauli mbaya isitoke kinywani mwenu. Badala yake, maneno lazima yatoke katika vinywa vyenu yafaayo kwa mahitaji, kuwapa faida wale wanaosikiliza.
30 And grieue not the holy Spirit of God, by whom ye are sealed vnto ye day of redemption.
Na msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu. Ni kwa Yeye kwamba mmewekewa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
31 Let all bitternesse, and anger, and wrath, crying, and euill speaking be put away from you, with all maliciousnesse.
Lazima muweke mbali uchungu wote, ghadhabu, hasira, ugomvi, na matusi, pamoja na kila aina ya uovu. Iweni wema ninyi kwa ninyi.
32 Be ye courteous one to another, and tender hearted, freely forgiuing one another, euen as God for Christes sake, freely forgaue you.
Mwe na huruma. Msameheane ninyi kwa ninyi, kama vile Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.

< Ephesians 4 >