< San Lucas 18 >

1 YA jasangane un acomparasion, na y taotao sija janesesita ufanmanayuyut, ya chañija fanataeanima.
Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2 Ilelegña: Guaja gui un siuda un jues, na ti maañao as Yuus, ni urespeta ni jaye na taotao:
Alisema: “Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3 Ya guaja locue güije na siuda un biuda ni y mato guiya güiya ya ilelegña: Areglajam yan y enemigujo.
Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4 Ya ti malago finena; lao despues ilegña gui sumanjalomña: Achogja ti maañaoyo as Yuus, ni jufanrespeta taotao;
Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5 Lao pot y jarorobayo este na palaoan, bae juaregla sija, sa noseaja pot y sisigueja mague, uestotbayo.
lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!”
6 Ya y Señot ilegña: Ecungog jafa y ti tunas na jues ilelegña.
Basi, Bwana akaendelea kusema, “Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7 Ada ti unalibre si Yuus y inayigña, ni y maaagang güe jaane, yan puenge, ya apmam na jasungon pot sija?
Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8 Jusangane jamyo, na enseguidas unafanlibre. Lao anae ufato y Lajin taotao, ufañoda jinenggue gui jilo tano?
Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?”
9 Ya jasangan este na acomparasion ni ayo sija y umangocon maesa sija na manunas, ya jadespresia y pumalo:
Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10 Dos na taotao jumanao julo gui templo para ujafanaetae: Y un Fariseo, ya y otro publicano.
“Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11 Y Fariseo tumojgue, ya taegüine tinaetaeña gui sumanjalomña: Junae jao grasias Yuus, sa ti parejoyo yan y pumalo na taotao, ni y manáplacha, yan manábale, ni y este publicano.
Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12 Umayuyunatyo dos biaje gui semana; mannanaeyo diesmos ni y todo güinajajo.
Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13 Lao y publicano gaegue na tumotojgue gui chago; ya ti jaguesjatsa y atadogña julo gui langet; lao jaseseco y pechoña, ya ilelegña: Yuus, gaease nu guajo, sa taotao isaoyo.
Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14 Jusangane jamyo, na, este na taotao jumanao papa y guimaña, ya maasie y isaoña, mas mauleg qui y otro; sa cada uno y minadangculo güe, uninaumitde; ya y munamitde güe, umanadangculo.
Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa.”
15 Ya maconie guato guiya güiya ni y diquique na famaguonñija, para upacha; ya anae manlinie ni y disipulo sija, manmalalatde.
Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16 Lao si Jesus jaagang sija, ya ilegña: Polo y diquique na famaguon ya ufanmamaela guiya guajo, ya chamiyo chumochoma; sa iyon este sija y raenon Yuus.
Lakini Yesu akawaita kwake akisema: “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17 Magajet jusangane jamyo, na y ti rumesibe y raenon Yuus taegüije y diquique na patgon, ti ujalom güije.
Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo.”
18 Ya un taotao na magas, finaesen güe ilelegña: Mauleg na Maestro, jafa jufatinas para juereda y taejinecog na linâlâ? (aiōnios g166)
Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios g166)
19 Ya si Jesus ilegña nu güiya: Jafa na ilegmo nu guajo mauleg? taya mauleg na unoja, si Yuus.
Yesu akamwambia, “Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20 Utungo y tinago sija: Chamo umábale, Chamo famumuno, Chamo fañañaque, Chamo sumasangan y ti magajet na sinangan, Onra si tatamo, yan nanamo.
Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako.”
21 Ya ilegña: Todo este sija juadaje desde y pinatgonjo.
Yeye akasema, “Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
22 Anae jajungog este sija si Jesus, ilegña nu güiya: Guaja uno fattamo trabia: bende todo y güinajamo, ya unfacae y mamobble, ya uguaja güinajamo gui langet, ya maela dalalagyo.
Yesu aliposikia hayo akamwambia, “Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate.”
23 Lao anae jajungog estesija, ninágostriste; sa gosrico güe.
Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24 Ya anae linie as Jesus, ilegña: Namanminapot ayo sija y mangaegüinaja manjalom gui raenon Yuus!
Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25 Sa guseña malofan un cameyo gui matan y jaguja, qui ujalom un rico gui raenon Yuus.
Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 Ya ayo y jumungog, ilegñija: Jaye nae siña satbo?
Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”
27 Ya ilegña: Y güinaja ni y ti mansiña para y taotao sija; mansiña para as Yuus.
Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”
28 Ayonae ilegña si Pedro: Estagüeja na indingo y iyonmame, ya indalalag jao.
Naye Petro akamwuliza, “Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”
29 Ya ilegña nu sija: Magajet jusangane jamyo, na taya ni un taotao ni y dumingo guma, pat asagua, pat mañelu, pat mañaena, pat famaguon, pot y raenon Yuus,
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30 Ya ti uresibe mas megae pago na tiempo, lao y mamamaela na tiempo, taejinecog na linâlâ. (aiōn g165, aiōnios g166)
atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Ya jacone y dose, ya ilegña nu sija: Estagüe, na manjajanaojit julo Jerusalem, ya todosija y tinigue y profeta sija pot y Lajin taotao, ufanmacumple.
Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32 Sa nesesita na umaentrega gui taotao juyong, ya umabotlea, yan umafaesegnane, yan umatolae:
Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33 Ya umasaulag, ya umapuno; ya y mina tres na jaane, ucajulo talo.
Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34 Lao sija ti jatungo ni uno gui este sija: ya este na sinangan manaatog guiya sija, ya ni ti jatungo jafa sija y masangan.
Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35 Ya susede anae esta jijijot Jerico, estaba un taotao bachet gui oriyan chalan na matatachong, ya umógagao:
Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36 Ya anae jajungog y linajyan taotao na manmalolofan, mamaesen jafa ayo.
Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
37 Ya masangane güe, na si Jesus Nasareno malolofan.
Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”
38 Ya umagang ilelegña: Jesus, jago ni y Lajin David, gaease nu guajo.
Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
39 Ya machoma ni y manmofona para ufamatquilo: lao mas umagang megae: Jago ni y Lajin David, gaease nu guajo.
Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie;”
40 Ya tumojgue si Jesus, ya manago na umaconie guato guiya güiya: ya anae esta jijijot, finaesen:
Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41 Jafa malagomo jufatinas guiya jago? Ya güiya ilegña: Señot, para jufanlie.
“Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona tena.”
42 Ya ilegña si Jesus nu güiya: Fanlie: y jinengguemo unsinatba.
Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”
43 Ya enseguidas jaresibe y liniiña, ya jadalalag güe, yan janamalag si Yuus; yan todo y taotao sija, anae malie, maalaba si Yuus.
Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.

< San Lucas 18 >