< San Lucas 17 >

1 YA ilegña ni y disipuluña sija: Ti siña ti ufato y escandalo; lao ay, ay ayo y munafato!
Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.
2 Maulegña na umagode gui agagaña un alutong, ya umayute gui tase, antes qui uninaquepodong uno güine gui mandiquique sija.
Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.
3 Adaje jamyo: Yanguin umisao y chelumo contra jago, reprende: y yanguin mañotsot, asie.
Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, mwonye; akitubu, msamehe.
4 Yanguin siete biaje gui un jaane umisao contra jago, ya siete biaje mafato guiya jago, ya ilelegña: Mañotsotyo, un asie.
Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema Nimetubu, lazima umsamehe.”
5 Ya y apostoles, ilegñija nu y Señot: Aumenta, y jinengguenmame.
Mitume wakamwambia Bwana, “Utuongezee imani.”
6 Ya y Señot ilegña: Yanguin mangaejinenggue jamyo taegüije y granon mostasa, ya mojon ilegmiyo nu este na sicómoro trongcon jayo: Chapag jao güenao, ya unplanta jao gui tase; ya mojon infaninesgueja.
Naye Bwana akajibu, “Kama imani yenu ingekuwa ndogo hata kama chembe ndogo ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu: Ng'oka ukajipandikize baharini, nao ungewatii.
7 Lao jaye guiya jamyo y guaja tentagoña, na manalalado, pat mamamasto quinilo, y yanguin mato guinin y fangualuan, ualog nu güiya; maela enseguidas y fatachong, ya unchocho?
“Tuseme mmoja wenu ana mtumishi ambaye analima shambani au anachunga kondoo. Je, anaporudi kutoka shambani, atamwambia: Haraka, njoo ule chakula?
8 Ya ti ualog nu güiya finena: Nalisto y senajo para juchocho, ya undudog jao, ya unsetbeyo asta qui munjayanyo chumocho, yan gumimen: ya despues nae unchocho, ya unguimen?
La! Atamwambia: Nitayarishie chakula, ujifunge tayari kunitumikia mpaka nitakapomaliza kula na kunywa, ndipo nawe ule na unywe.
9 Numae grasias ayo na tentago, sa jafatinas y matagoña? Jinasoco na aje.
Je utamshukuru huyo mtumishi kwa sababu ametimiza aliyoamriwa?
10 Taegüineja locue jamyo, yanguin esta inchegüe todo ayo sija y jutago jamyo, ualog: Maninutil jam na tentago; sa ayoja y para y chechomame inchegüe.
Hali kadhalika na ninyi mkisha fanya yote mliyoamriwa, semeni: Sisi ni watumishi tusio na faida, tumetimiza tu yale tuliyotakiwa kufanya.”
11 Ya susede anae jumanao para Jerusalem, ya malofan gui inanaco Samaria, yan Galilea.
Yesu akiwa safarini kwenda Yerusalemu alipitia mipakani mwa Samaria na Galilaya.
12 Ya anae jumalom gui un songsong, manasoda güije yan dies na taotao na manategtog; ya manojgue desde y chago.
Alipokuwa anaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wenye ukoma walikutana naye, wakasimama kwa mbali.
13 Ya jajatsa y inagangñija, ya ilegñija: Jesus, Maestro, gaease nu jame.
Wakapaza sauti wakisema, “Yesu Mwalimu, tuonee huruma!”
14 Ya anae jalie, ilegña nu sija: Janao ya infanue y mamale nu jamyo. Ya susede anae manjajanao, manjuyong mangasgas.
Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.
15 Ya y uno guiya sija, anae jalie na jomlo güe, jabira güe tate, ya janaagagang mannae si Yuus minalag.
Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.
16 Ya jatomba güe papa gui fion adeng si Jesus, ya janae grasias: este na taotao, Samaritano.
Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.
17 Ya manope si Jesus, ilegña: Ada ti dies y mangasgas? ya manmangue y nuebe?
Hapo Yesu akasema, “Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?
18 Taya masoda tumalo mague para unae si Yuus grasias, na esteja y taotao juyong.
Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu ila tu huyu mgeni?”
19 Ya ilegña bu güiya: Cajulo ya unjanao; y jinengguemo munajomlo jao.
Halafu akamwambia huyo mtu, “Simama, uende zako; imani yako imekuponya.”
20 Ya anae mafaesen ni y Fariseo sija, ngaean nae ufato y raenon Yuus, jaope ilegña: Y raenon Yuus, ti matungo finatoña.
Wakati mmoja, Mafarisayo walimwuliza Yesu, “Ufalme wa Mungu utakuja lini?” Naye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.
21 Ni ujaalog: Estagüe! pat ayogüe! sa y raenon Yuus, gaegueja gui sumanjalommiyo.
Wala hakuna atakayeweza kusema, Uko hapa, au Uko pale. Kwa kweli Ufalme wa Mungu uko kati yenu.”
22 Ya ilegña ni y disipuluña sija: Ufato y jaane sija, na infanmalago na inlie uno gui jaanin y Lajin taotao, ya ti inlie.
Halafu akawaambia wanafunzi wake, “Siku zinakuja ambapo mtatamani kuona mojawapo ya siku za Mwana wa Mtu, lakini hamtaiona.
23 Ya ujaalog nu jamyo: Estagüe, pat ayogüe; chamiyo tumatitiye, ni indalalaque sija.
Na watu watawaambieni: Tazameni yuko hapa; ninyi msitoke wala msiwafuate.
24 Sa taegüijeja y lamlam, yan mañila gui un lugat gui papa y langet, ya inina y otro banda gui papa y langet; taegüineja locue y Lajin taotao, gui jaaniña.
Kwa maana kama vile umeme unavyotokea ghafla na kuangaza anga upande mmoja hadi mwingine, ndivyo Mwana wa Mtu atakavyokuwa siku yake.
25 Lao nesesita na ufamadese finena megae, ya umarechasa ni este na generasion.
Lakini kabla ya hayo, itambidi ateseke sana na kukataliwa na kizazi hiki.
26 Sa jaftaemanoja y jaanin Noe, taegüijeja locue y jaanin y Lajin taotao.
Kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Mtu.
27 Mañocho, yan manguimen, yan manasagua, yan manafanasagua, asta ayo na jaane anae jumalom si Noe gui atca, ya mato y dilubio ya manyinilang sija todo.
Watu waliendelea kula na kunywa, kuoa na kuolewa mpaka wakati ule Noa alipoingia katika safina. Gharika ikatokea na kuwaangamiza wote.
28 Taegüineja locue jasusede gui jaanin Lot: mañocho, manguimen, manmamajan, manmanbende, manmananom, yan manmanjatsa guma;
Itakuwa kama ilivyotokea wakati wa Loti. Watu waliendelea kula na kunywa, kununua na kuuza, kupanda mbegu na kujenga.
29 Lao ayoja na jaane anae jumanao si Lot guiya Sodoma, janauchan guafe, yan asufre guinin y langet, ya manyinilang todo sija.
Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na kiberiti vikanyesha kama mvua kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote.
30 Taegüijeja uguaja güije na jaane yanguin ufamanue y Lajin taotao.
Ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mtu atakapofunuliwa.
31 Ayo na jaane, ayo y gaegue gui jilo guma ya y güinajaña gaegue gui jalom guma, chaña tumutunog ya uchule; parejoja locue yan y gaegue gui fangualuan, chaña tumatalo tate.
“Siku hiyo, yeyote atakayekuwa juu ya paa asishuke nyumbani kuchukua mali yake. Kadhalika, naye atakayekuwa shambani asirudi nyuma.
32 Jaso y asaguan Lot.
Kumbukeni yaliyompata mke wa Loti.
33 Masquesea jaye y umaliligao na usatba y linâlâña, ufinalingaeguan; ya masquesea jaye y finalingaeguan y liânâlña umasatba.
Yeyote anayetaka kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na yeyote anayeipoteza, ataiokoa.
34 Jusangane jamyo, na ayo na puenge uguaja dos na taotao gui un catre; y uno umacone ya y otro umapolo.
Nawaambieni, siku ile usiku watu wawili watakuwa wanalala pamoja, mmoja atachukuliwa na yule mwingine ataachwa.
35 Dos na palaoan dumadaña manguleg; y uno umacone, ya y otro umapolo.
Wanawake wawili watakuwa wakisaga nafaka pamoja; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.”
36 Dos na taotao ugaegue gui fangualuan; y uno umacone, ya y otro umapolo.
Watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
37 Ya manmanope ilegñija nu güiya: Manggue Señot? Ya jaope ilegña: Manoja nae gaegue y tataotao, ayoja nae mandaña y pojaro aguila sija.
Hapo wakamwuliza, “Ni wapi Bwana?” Naye akawaambia, “Ulipo mzoga, ndipo tai watakapokusanyikia.”

< San Lucas 17 >