< 2 Nyakati 4 >

1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
Il fit aussi un autel d'airain de vingt coudées de long, de vingt coudées de large, et de dix coudées de haut.
2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
Et il fit une mer de fonte, de dix coudées depuis un bord jusqu'à l'autre, ronde tout autour, et haute de cinq coudées, et un filet de trente coudées l'environnait tout autour.
3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
Et au dessous il y avait des figures de bœufs qui environnaient la mer tout autour, dix à chaque coudée; il y avait deux rangs de ces bœufs, qui avaient été jetés en fonte avec elle.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
Elle était posée sur douze bœufs, trois desquels regardaient le Septentrion, trois l'Occident, trois le Midi, et trois l'Orient; et la Mer était sur leurs dos, et tous leurs derrières [étaient tournés] en dedans.
5 Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
Et son épaisseur était d'une paume, et son bord était comme le bord d'une coupe à façon de fleurs de lis; elle contenait trois mille Baths.
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
Il fit aussi dix cuviers, et en mit cinq à droite, et cinq à gauche, pour s'en servir à laver; on y lavait ce qui appartenait aux holocaustes; mais la mer servait pour laver les Sacrificateurs.
7 Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
Il fit aussi dix chandeliers d'or selon la forme qu'ils devaient avoir; il les mit au Temple, cinq à droite, et cinq à gauche.
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
Il fit aussi dix tables; et les mit au Temple, cinq à droite, et cinq à gauche; et il fit cent bassins d'or.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
Il fit aussi le parvis des Sacrificateurs, et le grand parvis, et les portes pour les parvis, lesquelles il couvrit d'airain.
10 Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
Et il mit la mer à côté droit, tirant vers l'Orient, du côté du Midi.
11 Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
Hiram fit aussi des chaudières, et des racloirs, et des bassins, et acheva de faire tout l'ouvrage qu'il fit au Roi Salomon pour le Temple de Dieu;
12 zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
[Savoir] deux colonnes, et les pommeaux, et les deux chapiteaux qui [étaient] sur le sommet des colonnes, et les deux rets pour couvrir les pommeaux des chapiteaux qui étaient sur le sommet des colonnes.
13 yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
Et les quatre cents pommes de grenade pour les deux rets; deux rangs de pommes de grenade pour chaque rets, afin de couvrir les deux pommeaux des chapiteaux qui étaient au dessus des colonnes.
14 vishikio pamoja na masinia yake;
Il fit aussi les soubassements, et des cuviers pour les mettre sur les soubassements;
15 hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
Une mer, et douze bœufs sous elle.
16 pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
Et Hiram son père fit au Roi Salomon, pour l'usage du temple, des chaudières d'airain poli, des racloirs, des fourchettes, et tous les ustensiles qui en dépendaient.
17 Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
Le Roi les fondit dans la plaine du Jourdain, en terre grasse, entre Succoth et [le chemin qui tend] vers Tséréda.
18 Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
Et le Roi fit tous ces ustensiles-là en si grand nombre, que le poids de l'airain ne fut point recherché.
19 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
Salomon fit aussi tous les ustensiles nécessaires pour le Temple de Dieu, [savoir] l'autel d'or, et les Tables sur lesquelles on mettait les pains de proposition;
20 vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
Et les chandeliers avec leurs lampes de fin or, pour les allumer devant l'Oracle, selon la coutume;
21 maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
Et des fleurs, et des lampes, et des mouchettes d'or, qui étaient un or exquis;
22 mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.
Et les serpes, les bassins, les coupes, et les encensoirs de fin or. Et quant à l'entrée de la maison, les portes de dedans, [c'est-à-dire], du lieu Très-saint, et les portes de la maison, [c'est-à-dire], du Temple, étaient d'or.

< 2 Nyakati 4 >