< 2 Nyakati 3 >

1 Ndipo Solomoni akaanza kujenga Hekalu la Bwana katika Yerusalemu juu ya Mlima Moria, pale ambapo Bwana alikuwa amemtokea Daudi baba yake. Ilikuwa katika kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi, mahali palipotolewa na Daudi.
Et Salomon commença de bâtir la maison de l'Eternel à Jérusalem, sur la montagne de Morija, qui avait été montrée à David son père, dans le lieu que David son père avait préparé en l'aire d'Ornan Jébusien.
2 Alianza kujenga siku ya pili ya mwezi wa pili katika mwaka wa nne wa utawala wake.
Et il commença de [la bâtir] le second [jour] du second mois, la quatrième année de son règne.
3 Msingi aliouweka Solomoni kwa ajili ya kulijenga Hekalu la Mungu ulikuwa urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa ishirini.
Or ce fut ici le dessin de Salomon pour bâtir la maison de Dieu. Pour la première mesure, soixante coudées de long, et vingt coudées de large.
4 Ukumbi wa mbele wa Hekalu ulikuwa na urefu wa dhiraa ishirini, yaani, kuanzia upande mmoja hadi upande mwingine wa upana wa nyumba hiyo na kimo chake dhiraa thelathini. Akaufunika ndani kwa dhahabu safi.
Et le porche, qui [était] vis-à-vis de la longueur, en front de la largeur de la maison, [était] de vingt coudées; et la hauteur de six vingt coudées; et il le couvrit par dedans de pur or.
5 Akaufunika ukumbi mkuu kwa mbao za miberoshi na kufunikwa kwa dhahabu safi na kuupamba kwa miti ya mitende na kuifanyizia kwa minyororo.
Et il couvrit la grande maison de bois de sapin; il la couvrit d'un or exquis, et il y releva en bosse des palmes, et des chaînettes.
6 Alilipamba Hekalu kwa vito vya thamani. Hiyo dhahabu aliyotumia ilikuwa dhahabu ya Parvaimu.
Et il couvrit la maison de pierres exquises afin qu'elle en fût ornée; et l'or était de l'or de Parvaïm.
7 Akazifunika boriti za dari, miimo na vizingiti vya milango, kuta na milango ya Hekalu kwa dhahabu, naye akatia nakshi ya makerubi kwenye kuta.
Il couvrit donc d'or la maison, ses sommiers, ses poteaux, ses murailles, et ses portes, et il entailla des Chérubins dans les murailles.
8 Akajenga Patakatifu pa Patakatifu, urefu na upana wake ulikuwa dhiraa ishirini, sawasawa na upana wa Hekalu. Alifunika ndani kwa talanta 120 za dhahabu safi.
Il fit aussi le lieu Très-saint, dont la longueur était de vingt coudées selon la largeur de la maison; et sa largeur, de vingt coudées; et il le couvrit d'un or exquis, montant à six cents talents.
9 Misumari ya dhahabu ilikuwa na uzito wa shekeli hamsini. Alivifunika pia vyumba vya juu kwa dhahabu.
Et le poids des clous montait à cinquante sicles d'or; il couvrit aussi d'or les voûtes.
10 Katika sehemu ya Patakatifu pa Patakatifu akafanyiza jozi moja ya makerubi ya kuchongwa na kuyafunika kwa dhahabu.
Il fit aussi deux Chérubins en façon d'enfants dans le lieu Très-saint, et les couvrit d'or.
11 Urefu wa mabawa ya hao makerubi ulikuwa jumla ya dhiraa ishirini. Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa dhiraa tano, nalo liligusa ukuta wa Hekalu, bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano, ambalo liligusa bawa la kerubi lingine.
Et la longueur des ailes des Chérubins était de vingt coudées, tellement qu'une aile avait cinq coudées, et touchait la muraille de la maison; et l'autre aile avait cinq coudées, et touchait l'aile de l'autre Chérubin.
12 Vivyo hivyo bawa moja la kerubi wa pili lilikuwa na urefu wa dhiraa tano na liligusa ukuta mwingine wa pili wa Hekalu na bawa lake lingine, lilikuwa pia na urefu wa dhiraa tano nalo liligusa bawa la kerubi wa kwanza.
Et une des ailes de l'autre Chérubin, ayant cinq coudées, touchait la muraille de la maison; et l'autre aile ayant cinq coudées, était jointe à l'aile de l'autre Chérubin.
13 Mabawa ya makerubi hawa yalitanda dhiraa ishirini. Walisimama kwa miguu yao, nyuso zao zikielekea ukumbi mkubwa.
[Ainsi] les ailes de ces Chérubins étaient étendues le long de vingt coudées, et ils se tenaient droits sur leurs pieds, et leurs faces regardaient vers la maison.
14 Akatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na za kitani safi, na kutarizi makerubi juu yake.
Il fit aussi le voile de pourpre, d'écarlate, de cramoisi, et de fin lin, et y fit par dessus des Chérubins.
15 Mbele ya Hekalu Solomoni akatengeneza nguzo mbili, ambazo kwa pamoja zilikuwa na dhiraa thelathini na tano kwenda juu kwake, na urefu wa kila moja ilikuwa na taji juu yake yenye dhiraa tano.
Et au devant de la maison il fit deux colonnes, qui avaient trente-cinq coudées de longueur; et les chapiteaux qui étaient sur le sommet de chacune étaient de cinq coudées.
16 Akatengeneza minyororo iliyosokotwa, na kuiweka juu ya zile nguzo. Pia akatengeneza makomamanga 100, na kuyashikamanisha kwenye minyororo.
Or comme il avait fait des chaînettes pour l'Oracle, il en mit aussi sur le sommet des colonnes; et il fit cent pommes de grenade, qu'il mit aux chaînettes.
17 Akazisimamisha hizo nguzo mbele ya Hekalu, moja upande wa kusini na nyingine upande wa kaskazini. Ile moja ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.
Et il dressa les colonnes au devant du Temple, l'une à main droite, et l'autre à main gauche, et il appela celle qui était à la droite, Jakin; et celle qui était à la gauche, Bohaz.

< 2 Nyakati 3 >