< 2 Nyakati 20 >

1 Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati.
Il arriva, après cela, que les enfants de Moab et les enfants d'Ammon (car avec eux il y avait des Ammonites), vinrent contre Josaphat pour lui faire la guerre.
2 Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako kutoka Edomu tokea ngʼambo ile nyingine ya Bahari. Tayari liko Hasason-Tamari” (yaani En-Gedi).
On vint donc le rapporter à Josaphat, en disant: Il vient contre toi une grande multitude d'au delà de la mer, de Syrie; et les voici à Hatsatson-Thamar, qui est En-Guédi.
3 Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafuta Bwana, na akatangaza kwa Yuda wote kufunga.
Alors Josaphat craignit; et il se disposa à rechercher l'Éternel, et il publia un jeûne pour tout Juda.
4 Watu wa Yuda wakakusanyika pamoja ili kutafuta msaada kutoka kwa Bwana. Wakaja kutoka kila mji wa Yuda ili kumtafuta.
Juda s'assembla donc pour demander du secours à l'Éternel; on vint même de toutes les villes de Juda pour chercher l'Éternel.
5 Kisha Yehoshafati akasimama katika kusanyiko la Yuda na Yerusalemu katika Hekalu la Bwana, mbele ya ua mpya,
Et Josaphat se tint debout dans l'assemblée de Juda et de Jérusalem, dans la maison de l'Éternel, devant le nouveau parvis;
6 akasema: “Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe ndiwe uliye Mungu mbinguni? Si wewe ndiwe utawalaye juu ya falme zote za mataifa? Uweza na nguvu viko mkononi mwako, wala hakuna yeyote awezaye kushindana nawe.
Et il dit: Éternel, Dieu de nos pères! n'es-tu pas Dieu dans les cieux, et n'est-ce pas toi qui domines sur tous les royaumes des nations? Et n'as-tu pas en ta main la force et la puissance, en sorte que nul ne peut te résister?
7 Je, si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Abrahamu, rafiki yako, hata milele?
N'est-ce pas toi, ô notre Dieu! qui as dépossédé les habitants de ce pays devant ton peuple d'Israël, et qui l'as donné pour toujours à la postérité d'Abraham, qui t'aimait?
8 Wameishi ndani yake na humo wamekujengea mahali patakatifu kwa ajili ya Jina lako, wakisema:
Ils l'ont habité, et t'y ont bâti un sanctuaire pour ton nom, en disant:
9 ‘Kama maafa yakitujia, ikiwa ni upanga, hukumu, tauni, au njaa, tutasimama mbele zako, mbele ya Hekalu hili ambalo limeitwa kwa Jina lako na kukulilia katika shida yetu, nawe utatusikia na kutuokoa.’
S'il nous arrive quelque mal, l'épée, le jugement, la peste, ou la famine, nous nous tiendrons devant cette maison, et en ta présence; car ton nom est en cette maison; et nous crierons à toi dans notre détresse, et tu exauceras et tu délivreras!
10 “Lakini sasa hawa watu wa kutoka Amoni, Moabu na Mlima Seiri, ambao hukuwaruhusu Israeli wazivamie nchi zao wakati walitoka Misri, hivyo wakageukia mbali nao na hawakuwaangamiza,
Maintenant, voici les enfants d'Ammon et de Moab, et ceux de la montagne de Séir, chez lesquels tu ne permis pas à Israël d'entrer, quand il venait du pays d'Égypte, car il se détourna d'eux, et ne les détruisit pas,
11 tazama jinsi wanavyotulipa kwa kuja kututupa nje ya milki uliyotupa sisi kuwa urithi.
Les voici qui nous en récompensent, en venant nous chasser de ton héritage, dont tu nous as donné la possession.
12 Ee Mungu wetu, je, wewe hutawahukumu? Kwa kuwa sisi hatuna uwezo wa kukabiliana na jeshi hili kubwa linalokuja kutushambulia. Sisi hatujui la kufanya, bali macho yetu yanakutazama wewe.”
O notre Dieu! ne les jugeras-tu pas? Car il n'y a point de force en nous devant cette grande multitude qui vient contre nous, et nous ne savons que faire; mais nos yeux sont sur toi.
13 Watu wote wa Yuda pamoja na wake zao, watoto wao na wadogo wao wakasimama pale mbele za Bwana.
Or tout Juda se tenait devant l'Éternel, même avec leurs familles, leurs femmes et leurs enfants.
14 Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya mtu mmoja jina lake Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, Mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi mzao wa Asafu alipokuwa amesimama katika kusanyiko.
Alors l'Esprit de l'Éternel fut sur Jachaziel, fils de Zacharie, fils de Bénaja, fils de Jéïel, fils de Matthania, Lévite, d'entre les enfants d'Asaph, au milieu de l'assemblée;
15 Akasema: “Sikilizeni, enyi Yuda wote nanyi nyote mkaao Yerusalemu, nawe Mfalme Yehoshafati! Hili ndilo Bwana asemalo kwenu, ‘Msiogope wala msifadhaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Kwa maana vita hivi si vyenu, bali ni vya Mungu.
Et il dit: Vous, tout Juda, et habitants de Jérusalem, et toi, roi Josaphat, soyez attentifs! Ainsi vous dit l'Éternel: Ne craignez point, et ne soyez point effrayés à cause de cette grande multitude; car ce ne sera pas à vous de combattre, mais à Dieu.
16 Kesho shukeni kukabiliana nao. Watakwea kwa kupandia Genge la Sisi, nanyi mtawakuta mwisho wa bonde, kabla ya Jangwa la Yerueli.
Descendez demain contre eux; les voici qui montent par la montée de Tsits, et vous les trouverez à l'extrémité de la vallée, en face du désert de Jéruël.
17 Hamtahitaji kupigana vita hivi. Kaeni kwenye nafasi zenu, simameni imara na mkaone wokovu Bwana atakaowapatia, enyi Yuda na Yerusalemu. Msiogope, wala msifadhaike. Kesho tokeni mwende mkawakabili, naye Bwana atakuwa pamoja nanyi.’”
Ce ne sera point à vous de combattre en cette bataille; présentez-vous, tenez-vous là, et voyez la délivrance que l'Éternel va vous donner. Juda et Jérusalem, ne craignez point, et ne soyez point effrayés! Demain, sortez au-devant d'eux, et l'Éternel sera avec vous.
18 Yehoshafati akainamisha uso wake chini, nao watu wote wa Yuda na Yerusalemu wakaanguka chini ili kuabudu mbele za Bwana.
Alors Josaphat s'inclina le visage contre terre, et tout Juda et les habitants de Jérusalem se jetèrent devant l'Éternel, se prosternant devant l'Éternel.
19 Ndipo baadhi ya Walawi kutoka kwa Wakohathi na kwa wana wa Kora wakasimama na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sauti kuu sana.
Et les Lévites, d'entre les enfants des Kéhathites et d'entre les enfants des Corites, se levèrent pour célébrer l'Éternel, le Dieu d'Israël, d'une voix forte et haute.
20 Asubuhi na mapema wakaondoka kuelekea Jangwa la Tekoa. Walipoanza safari, Yehoshafati akasimama akasema, “Nisikilizeni, enyi Yuda, na watu wa Yerusalemu! Mwaminini Bwana Mungu wenu, hivyo mtathibitika, wasadikini manabii wake nanyi mtafanikiwa.
Puis, le matin, ils se levèrent de bonne heure et sortirent vers le désert de Thékoa; et comme ils sortaient, Josaphat se tint là et dit: Juda et vous, habitants de Jérusalem, écoutez-moi: Croyez en l'Éternel votre Dieu, et vous serez en sûreté; croyez en ses prophètes, et vous réussirez.
21 Alipomaliza kushauriana na watu, Yehoshafati akawaweka watu wa kumwimbia Bwana na kumsifu katika utukufu wa utakatifu wake walipokuwa wametangulia mbele ya jeshi, wakisema: “Mshukuruni Bwana kwa kuwa upendo wake wadumu milele.”
Puis, ayant délibéré avec le peuple, il établit des chantres de l'Éternel, qui célébraient sa sainte magnificence; et, marchant devant l'armée, ils disaient: Louez l'Éternel, car sa miséricorde demeure à toujours!
22 Walipoanza kuimba na kusifu, Bwana akaweka waviziao dhidi ya watu wa Amoni, Moabu na wale wa Mlima Seiri waliokuwa wamekuja kuishambulia Yuda, nao wakashindwa.
Et au moment où ils commencèrent le chant et la louange, l'Éternel mit des embuscades contre les enfants d'Ammon, et de Moab, et ceux de la montagne de Séir, qui venaient contre Juda, et ils furent battus.
23 Watu wa Amoni na Moabu wakawainukia watu wa Mlima Seiri ili kuwaua na kuwaangamiza kabisa. Baada ya kumaliza kuwachinja watu wa Seiri, wakaangamizana wao kwa wao.
Les enfants d'Ammon et de Moab se levèrent contre les habitants de la montagne de Séir, pour les vouer à l'interdit et les exterminer; et quand ils en eurent fini avec les habitants de Séir, ils s'aidèrent l'un l'autre à se détruire.
24 Yuda walipofika katika mnara wa ulinzi wa jangwani, wakaliangalia lile jeshi kubwa, wakaona ni maiti tupu zimetapakaa ardhini, wala hakuna yeyote aliyenusurika.
Et quand Juda arriva sur la hauteur d'où l'on voit le désert, ils regardèrent vers cette multitude, et voici, c'étaient des cadavres gisant à terre, sans qu'il en fût échappé un seul.
25 Hivyo Yehoshafati na watu wake wakaenda kujitwalia nyara kutoka kwao, nao wakakuta humo wingi wa mifugo, mali, nguo na vitu vya thamani, ambavyo vilikuwa vingi zaidi ya vile walivyoweza kuchukua. Wakakusanya nyara kwa siku tatu kwa sababu zilikuwa nyingi mno.
Ainsi Josaphat et son peuple vinrent pour piller leur butin, et ils trouvèrent parmi eux, au milieu des cadavres, des biens en abondance, et des objets précieux; et ils en enlevèrent tant, qu'ils ne le pouvaient porter; et ils pillèrent le butin pendant trois jours, car il était considérable.
26 Siku ya nne wakakusanyika katika Bonde la Beraka kwa maana huko ndiko walikomsifu Bwana. Ndiyo sababu linaitwa Bonde la Beraka mpaka leo.
Et, le quatrième jour, ils s'assemblèrent dans la vallée de Bénédiction; car ils bénirent là l'Éternel; c'est pourquoi, on a appelé ce lieu, jusqu'à ce jour, la vallée de Bénédiction.
27 Kisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu, wakiongozwa na Yehoshafati, wakarudi Yerusalemu wakiwa na furaha kwa kuwa Bwana alikuwa amewasababisha wafurahi juu ya adui zao.
Puis tous les hommes de Juda et de Jérusalem, et Josaphat, à leur tête, reprirent joyeusement le chemin de Jérusalem; car l'Éternel leur avait donné de la joie au sujet de leurs ennemis.
28 Wakaingia Yerusalemu na kwenda hekaluni mwa Bwana wakiwa na vinubi, zeze na tarumbeta.
Ils entrèrent donc à Jérusalem, dans la maison de l'Éternel, avec des lyres, des harpes et des trompettes.
29 Hofu ya Mungu ikazipata falme zote za nchi waliposikia jinsi Bwana alivyokuwa amepigana dhidi ya adui za Israeli.
Et la terreur de Dieu fut sur tous les royaumes des divers pays, quand ils eurent appris que l'Éternel avait combattu contre les ennemis d'Israël.
30 Ufalme wa Yehoshafati ukawa na amani, kwa kuwa Mungu wake alikuwa amemstarehesha pande zote.
Ainsi le royaume de Josaphat fut tranquille, et son Dieu lui donna du repos de tous côtés.
31 Hivyo Yehoshafati akatawala Yuda. Alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, akatawala katika Yerusalemu kwa miaka ishirini na mitano. Mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
Josaphat régna donc sur Juda. Il était âgé de trente-cinq ans quand il devint roi, et il régna vingt-cinq ans à Jérusalem. Sa mère s'appelait Azuba, fille de Shilchi.
32 Alienenda katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana.
Il suivit les traces d'Asa, son père, et il ne s'en détourna point, faisant ce qui est droit devant l'Éternel.
33 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa, na watu wakawa bado hawajaelekeza mioyo yao kwa Mungu wa baba zao.
Seulement les hauts lieux ne furent point ôtés, et le peuple n'avait pas encore tourné son cœur vers le Dieu de ses pères.
34 Matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Yehu mwana wa Hanani, ambazo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli.
Or le reste des actions de Josaphat, les premières et les dernières, voici, elles sont écrites dans les mémoires de Jéhu, fils de Hanani, insérés dans le livre des rois d'Israël.
35 Hatimaye Yehoshafati mfalme wa Yuda akafanya urafiki na Ahazia mfalme wa Israeli ambaye alifanya maovu sana.
Après cela, Josaphat, roi de Juda, s'associa avec Achazia, roi d'Israël, dont la conduite était impie.
36 Akaungana naye kutengeneza meli nyingi za kwenda Tarshishi, nazo zilitengenezwa huko Esion-Geberi.
Il s'associa avec lui pour faire des navires, afin d'aller à Tarsis; et ils firent des navires à Etsjon-Guéber.
37 Ndipo Eliezeri mwana wa Dodavahu wa Maresha akatoa unabii dhidi ya Yehoshafati, akasema, “Kwa kuwa umeungana na Ahazia, Bwana ataangamiza vile mlivyotengeneza.” Zile meli zikavunjika na hazikuweza kungʼoa nanga ili kwenda Tarshishi.
Alors Éliézer, fils de Dodava, de Marésha, prophétisa contre Josaphat, en disant: Parce que tu t'es associé avec Achazia, l'Éternel a détruit ton œuvre. Et les navires furent brisés, et ne purent aller à Tarsis.

< 2 Nyakati 20 >