< 2 Nyakati 19 >

1 Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu.
Josaphat, roi de Juda, revint sain et sauf dans sa maison, à Jérusalem.
2 Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukia Bwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu ya Bwana iko juu yako.
Mais Jéhu, fils de Hanani, le Voyant, sortit au-devant du roi Josaphat, et lui dit: Est-ce le méchant qu'il faut aider? Sont-ce les ennemis de l'Éternel que tu aimes? A cause de cela, l'Éternel est irrité contre toi.
3 Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa kuwa umeondoa katika nchi nguzo za Ashera na umeukaza moyo wako katika kumtafuta Mungu.”
Mais il s'est trouvé de bonnes choses en toi, car tu as ôté du pays les emblèmes d'Ashéra, et tu as appliqué ton cœur à rechercher Dieu.
4 Yehoshafati aliishi huko Yerusalemu, naye akatoka akaenda tena miongoni mwa watu, kuanzia Beer-Sheba hadi nchi ya vilima ya Efraimu na kuwageuza wakamrudia Bwana, Mungu wa baba zao.
Et Josaphat habita à Jérusalem. Puis, de nouveau, il sortit parmi le peuple, depuis Béer-Shéba jusqu'à la montagne d'Éphraïm, et il les ramena à l'Éternel, le Dieu de leurs pères.
5 Akawaweka waamuzi katika nchi, kwenye miji yote ya Yuda yenye maboma.
Il établit aussi des juges dans le pays, dans toutes les villes fortes de Juda, dans chaque ville.
6 Akawaambia, “Angalieni kwa makini yale mtendayo, kwa kuwa hamkuhukumu kwa ajili ya mwanadamu bali kwa ajili ya Bwana ambaye yu pamoja nanyi kila mtoapo hukumu.
Et il dit aux juges: Regardez à ce que vous ferez; car ce n'est pas pour l'homme que vous jugerez, mais pour l'Éternel, qui sera avec vous quand vous jugerez.
7 Basi sasa hofu ya Bwana na iwe juu yenu. Hukumuni kwa uangalifu, kwa kuwa kwa Bwana Mungu wetu hakuna jambo lisilo la haki, upendeleo, wala rushwa.”
Maintenant, que la crainte de l'Éternel soit sur vous; prenez garde à ce que vous ferez; car il n'y a point d'iniquité dans l'Éternel notre Dieu, ni d'acception de personnes, ni d'acceptation de présents.
8 Pia huko Yerusalemu, Yehoshafati akaweka baadhi ya Walawi, makuhani na viongozi wa jamaa za Waisraeli ili kutoa hukumu kwa ajili ya Bwana na kuamua magomvi. Nao waliishi huko Yerusalemu.
Josaphat établit aussi à Jérusalem des Lévites, et des sacrificateurs, et des chefs des pères d'Israël, pour le jugement de l'Éternel, et pour les contestations. Et on revint à Jérusalem.
9 Akawapa maagizo haya: “Ni lazima mtumike kwa uaminifu na kwa moyo wote katika kicho cha Bwana.
Et il leur donna des ordres, en disant: Vous agirez ainsi dans la crainte de l'Éternel, avec fidélité et avec intégrité de cœur.
10 Katika kila shauri lifikalo mbele yenu kutoka kwa ndugu zenu wale waishio katika miji, ikiwa ni la umwagaji wa damu au mambo mengine yahusuyo sheria, amri, hukumu au maagizo, inawapasa ninyi kuwaonya kwamba wasiingie katika hatia dhidi ya Bwana, la sivyo ghadhabu yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Tendeni hivyo, nanyi hamtatenda dhambi.
Et pour les différends qui viendront devant vous, de la part de vos frères qui habitent dans leurs villes, qu'il s'agisse d'un meurtre, d'une loi, d'un commandement, de statuts ou d'ordonnances, vous les éclairerez, afin qu'ils ne se rendent pas coupables envers l'Éternel, et qu'il n'y ait point de courroux sur vous et sur vos frères. Vous agirez ainsi, et vous ne serez point trouvés coupables.
11 “Amaria kuhani mkuu atakuwa juu yenu katika jambo lolote linalomhusu Bwana naye Zebadia mwana wa Ishmaeli, kiongozi wa kabila la Yuda, atakuwa juu yenu kwa jambo lolote linalomhusu mfalme, nao Walawi watatumika kama maafisa mbele yenu. Tendeni kwa ujasiri, naye Bwana atakuwa pamoja na wale watendao vyema.”
Et voici, Amaria, le principal sacrificateur, est préposé sur vous pour toutes les affaires de l'Éternel, et Zébadia, fils d'Ismaël, prince de la maison de Juda, pour toutes les affaires du roi; et pour secrétaires vous avez devant vous les Lévites. Fortifiez-vous et agissez; et que l'Éternel soit avec l'homme de bien!

< 2 Nyakati 19 >