< 2 Korinæanima 10 >

1 A sam ja Pavle molim vas krotosti radi i tišine Hristove, koji sam pred vama ponižen prema vama, a kad nijesam kod vas, slobodan sam prema vama.
Basi, mimi Paulo ninawasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye “mwoga” ninapokuwa pamoja nanyi ana kwa ana, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi!
2 Molim pak da mi ne bude trijebe kad budem kod vas, onako slobodan biti kao što mislim da smijem protiv nekijeh koji misle za nas da po tijelu živimo;
Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani, kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu.
3 Jer ako i živimo u tijelu, ne borimo se po tijelu.
Ingawa tunaishi duniani, hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo.
4 Jer oružje našega vojevanja nije tjelesno, nego silno od Boga na raskopavanje gradova, da kvarimo pomisli
Silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome,
5 I svaku visinu koja se podiže na poznanje Božije, i robimo svaki razum za pokornost Hristu,
tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo,
6 I u pripravnosti imamo osvetu za svaku nepokornost, kad se izvrši vaša pokornost.
tena tukiwa tayari kuadhibu kila tendo la kutotii, kutii kwenu kutakapokamilika.
7 Gledate li na ono što vam je pred oèima? Ako se ko uzda da je Hristov neka misli opet u sebi da kako je on Hristov tako smo i mi Hristovi.
Angalieni yale yaliyo machoni penu. Kama mtu yeyote anaamini kuwa yeye ni mali ya Kristo, basi kumbuka kuwa kama ulivyo wa Kristo, vivyo hivyo na sisi ndivyo tulivyo.
8 Jer ako se što i više pohvalim vlašæu našom koju nam dade Gospod na popravljanje, a ne na kvarenje vaše, neæu se postidjeti.
Basi hata kama nikijisifu zaidi kidogo kuhusu mamlaka tuliyo nayo, ambayo Bwana alitupa ili kuwajenga wala si kuwabomoa, mimi sitaionea haya.
9 Ali da se ne pokažem kao da vas plašim poslanicama;
Sitaki nionekane kama ninayejaribu kuwatisha kwa nyaraka zangu.
10 Jer su poslanice, veli, teške i jake, a kad je tijelom pred nama, slab je, i rijeè njegova ne valja ništa.
Kwa maana wanasema, “Nyaraka zake ni nzito na zenye nguvu, lakini ana kwa ana ni dhaifu na kuzungumza kwake ni kwa kudharauliwa.”
11 Ovo neka pomisli takovi da kaki smo u rijeèi po poslanicama kad nijesmo kod vas, taki smo i u djelu kad smo tu.
Watu kama hao wajue ya kuwa, yale tusemayo kwa barua tukiwa hatupo pamoja nanyi, ndivyo tulivyo na ndivyo tutakavyofanya tutakapokuwa pamoja nanyi.
12 Jer ne smijemo sebe miješati ili se porediti s drugima koji hvale sami sebe; ali kad sami po sebi sebe mjere i porede sami sebe sa sobom, ne razumijevaju.
Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojitukuza wenyewe kuwa wao ni wa maana sana. Wanapojipima na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara.
13 A mi se neæemo hvaliti preko mjere, nego po mjeri pravila kojega nam Bog mjeru razdijeli da dopremo i do vas.
Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ile Mungu aliyotuwekea, mipaka ambayo inawafikia hata ninyi.
14 Jer se mi daleko ne prostiremo, kao da ne dosežemo do vas; jer doprijesmo i do vas s jevanðeljem Hristovijem,
Kwa maana hatukuwa tunavuka mipaka katika kujisifu kwetu, kama vile ambavyo ingekuwa kama hatukuwa tumekuja kwenu. Kwa maana sisi ndio tuliokuwa wa kwanza kuja kwenu na Injili ya Kristo.
15 Ne hvaleæi se preko mjere u tuðijem poslovima, imajuæi pak nad kad uzraste vjera vaša da æemo se u vama velièati po pravilu svojemu izobilno,
Wala hatuvuki mipaka kwa kujisifu kwetu kwa ajili ya kazi iliyofanywa na watu wengine. Tumaini letu ni kwamba imani yenu inavyozidi kukua, eneo letu la utendaji miongoni mwenu litapanuka zaidi,
16 Da i u daljnijem stranama od vas propovjedimo jevanðelje, i da se ne pohvalimo onijem što je po tuðemu pravilu ureðeno.
ili tuweze kuhubiri Injili sehemu zilizo mbali na maeneo yenu. Kwa maana hatutaki kujisifu kwa ajili ya kazi ambayo imekwisha kufanyika tayari katika eneo la mtu mwingine.
17 A koji se hvali, Gospodom neka se hvali.
Lakini, “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
18 Jer onaj nije valjan koji se sam hvali, nego kojega Gospod hvali.
Kwa maana si yeye ajisifuye mwenyewe akubaliwaye, bali yeye ambaye Bwana humsifu.

< 2 Korinæanima 10 >