< مکاشفهٔ یوحنا 17 >

و یکی از آن هفت فرشته‌ای که هفت پیاله را داشتند، آمد و به من خطاب کرده، گفت: «بیا تا قضای آن فاحشه بزرگ را که برآبهای بسیار نشسته است به تو نشان دهم، ۱ 1
Mmoja wa malaika saba aliyekuwa na vitasa saba alikuja na kuniambia, “Njoo, nitakuonesha hukumu ya kahaba mkuu akaaye juu ya maji mengi,
که پادشاهان جهان با او زنا کردند و ساکنان زمین، ازخمر زنای او مست شدند.» ۲ 2
ambaye wafalme wa nchi wamefanya mambo ya uzinzi naye na juu ya mvinyo wa uzinzi wake wakaao duniani wameleweshwa.”
پس مرا در روح به بیابان برد و زنی را دیدم بر وحش قرمزی سوارشده که از نامهای کفر پر بود و هفت سر و ده شاخ داشت. ۳ 3
Malaika akanichukua katika Roho mpaka nyikani, na nilimwona mwanamke amekaa juu ya mnyama mwekundu aliyejaa majina ya matukano. Mnyama alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
و آن زن، به ارغوانی و قرمز ملبس بود وبه طلا و جواهر و مروارید مزین و پیاله‌ای زرین به‌دست خود پر از خبائث و نجاسات زنای خودداشت. ۴ 4
Mwanamke alivikwa nguo ya zambarau na nyekundu na amepambwa kwa dhahabu, mawe ya thamani, na lulu. Alikuwa ameshikilia mkononi mwake kikombe cha dhahabu kilichojaa vitu vya machukizo ya uchafu wa uasherati wake.
و بر پیشانی‌اش این اسم مرقوم بود: «سرو بابل عظیم و مادر فواحش و خبائث دنیا.» ۵ 5
Juu ya paji la uso wake limeandikwa jina la siri: “BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA YA VITU VYA MACHUKIZO YA NCHI.”
وآن زن را دیدم، مست از خون مقدسین و از خون شهدای عیسی و از دیدن او بی‌نهایت تعجب نمودم. ۶ 6
Nikaona ya kuwa mwanamke huyo alikuwa amelewa kwa damu ya waumini na damu ya waliokufa kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona, nilikuwa na mshangao mkuu.
و فرشته مرا گفت: «چرا متعجب شدی؟ من سر زن و آن وحش را که هفت سر و ده شاخ دارد که حامل اوست، به تو بیان می‌نمایم. ۷ 7
Lakini malaika akaniambia, “Kwa nini unashangaa? Nitakueleza maana ya mwanamke na mnyama amchukuaye (mnyama huyo mwenye vichwa saba na zile pembe kumi).
آن وحش که دیدی، بود و نیست و از هاویه خواهدبرآمد و به هلاکت خواهد رفت؛ و ساکنان زمین، جز آنانی که نامهای ایشان از بنای عالم در دفترحیات مرقوم است، در حیرت خواهند افتاد ازدیدن آن وحش که بود و نیست و ظاهر خواهدشد. (Abyssos g12) ۸ 8
Mnyama uliyemwona alikuwepo, hayupo tena sasa, lakini yuko tayari kupanda kutoka katika shimo lisilo na mwisho. Kisha ataendelea na uharibifu. Wale wakaao juu ya nchi, wale ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu - watashangaa wamwonapo mnyama aliyekuwepo, kwamba hayupo sasa, lakini yupo karibu kuja. (Abyssos g12)
«اینجاست ذهنی که حکمت دارد. این هفت سر، هفت کوه می‌باشد که زن بر آنها نشسته است؛ ۹ 9
Wito huu ni kwa ajili ya akili zilizo na hekima. Vichwa saba ni milima saba ambapo mwanamke alikaa juu yake.
و هفت پادشاه هستند که پنج افتاده‌اند و یکی هست و دیگری هنوز نیامده است و چون آیدمی باید اندکی بماند. ۱۰ 10
Nayo pia ni wafalme saba. Wafalme watano wameanguka, mmoja yupo, na mwingine hajaja bado; wakati atakapokuja, atakaa kwa muda mfupi tu.
و آن وحش که بود ونیست، هشتمین است و از آن هفت است و به هلاکت می‌رود. ۱۱ 11
Mnyama aliyekuwepo, lakini sasa hayupo, yeye pia ni mfalme wa nane; lakini ni mmoja wa wale wafalme saba, na anaenda kwenye uharibifu.
و آن ده شاخ که دیدی، ده پادشاه هستند که هنوز سلطنت نیافته‌اند بلکه یک ساعت با وحش چون پادشاهان قدرت می‌یابند. ۱۲ 12
Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi ambao hawajapokea ufalme, lakini watapokea mamlaka kama wafalme kwa saa moja pamoja na mnyama.
اینها یک رای دارند و قوت و قدرت خود را به وحش می‌دهند. ۱۳ 13
Hawa wana shauri moja, na watampa nguvu zao na mamlaka yule mnyama.
ایشان با بره جنگ خواهندنمود و بره بر ایشان غالب خواهد آمد، زیرا که اورب‌الارباب و پادشاه پادشاهان است و آنانی نیز که با وی هستند که خوانده شده و برگزیده وامینند.» ۱۴ 14
Watafanya vita baina yao na Mwana kondoo. Lakini Mwana kondoo atawashinda kwa sababu ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme - na katika yeye tuliitwa, tulichaguliwa, waaminifu.”
و مرا می‌گوید: «آبهایی که دیدی، آنجایی که فاحشه نشسته است، قومها و جماعتها وامت‌ها و زبانها می‌باشد. ۱۵ 15
Malaika akaniambia, “Yale maji uliyoyaona, hapo alipoketi yule kahaba ni watu, makutano, mataifa na lugha.
و اما ده شاخ که دیدی و وحش، اینها فاحشه را دشمن خواهند داشت واو را بینوا و عریان خواهند نمود و گوشتش راخواهند خورد و او را به آتش خواهند سوزانید، ۱۶ 16
Zile pembe kumi ulizoziona - hizo na yule mnyama watamchukia yule kahaba. Nao watamfanya kuwa mpweke na uchi, watamla mwili wake, na watauteketeza kwa moto.
زیرا خدا در دل ایشان نهاده است که اراده او رابه‌جا آرند و یک رای شده، سلطنت خود را به وحش بدهند تا کلام خدا تمام شود. ۱۷ 17
Maana Mungu ameweka mioyoni mwao kubeba kusudi lake kwa makubaliano ya kumpa mnyama nguvu zao kumtawala mpaka maneno ya Mungu yatakapotimia.
و زنی که دیدی، آن شهر عظیم است که بر پادشاهان جهان سلطنت می‌کند.» ۱۸ 18
Yule mwanamke uliyemwona ni mji ule mkubwa utawalao juu ya wafalme wa nchi.”

< مکاشفهٔ یوحنا 17 >