< 2 до коринтян 3 >

1 Чи нам знов зачинати дору́чувати самих себе́? Чи ми потребуємо, як дехто, листів доруча́льних до вас чи від вас?
Je, tumeanza kujisifia wenyewe tena? Hatuhitaji barua ya mapendekezo kwenu au kutoka kwenu, kama baadhi ya watu, je twahitaji?
2 Ви наш лист, написаний у наших серцях, якого всі люди знають і читають!
Ninyi wenyewe ni barua yetu ya mapendekezo, iliyoandikwa kwenye mioyo yetu, inayojulikana na kusomwa na watu wote.
3 Виявляєте ви, що ви — лист Христів, нами вислужений, що написаний не чорнилом, але Духом Бога Живого, не на табли́цях камінних, але на тіле́сних табли́цях серця.
Na mnaonesha kwamba ninyi ni barua kutoka kwa Kristo, iliyotolewa na sisi. Iliandikwa siyo kwa wino bali kwa Roho wa Mungu aliye hai. Haikuandikwa juu ya vibao vya mawe, bali juu ya vibao vya mioyo ya wanadamu.
4 Таку ж певність до Бога ми маємо через Христа,
Na huu ndiyo ujasiri tulio nao katika Mungu kupitia Kristo.
5 не тому́, що ми здібні поми́слити щось із се́бе, як від себе, але наша здібність від Бога.
Hatujiamini wenyewe kwa kudai chochote kama kutoka kwetu. Badala yake, kujiamini kwetu kunatoka kwa Mungu.
6 І Він нас зробив бути здатними служи́телями Ново́го Заповіту, не букви, а Духа, — бо буква вбиває, а Дух оживля́є.
Ni Mungu ambaye alitufanya tuweze kuwa watumishi wa agano jipya. Hili ni agano sio la barua bali ni la Roho. Kwa kuwa barua huua, lakini roho inatoa uhai.
7 Коли ж служі́ння смерті, вирізане на каменях буквами, було таке славне, що Ізра́їлеві сини не могли дивитись на обличчя Мойсея, через славу мину́щу обличчя його,
Sasa kazi ya kifo iliyokuwa imechongwa katika herufi juu ya mawe ilikuja kwa namna ya utukufu kwamba watu wa Israeli hawakuangalia moja kwa moja kwenye uso wa Musa. Hii ni kwa sababu ya utukufu wa uso wake, utukufu ambao ulikuwa unafifia.
8 скільки ж більш буде в славі те служі́ння Духа!
Je, kazi ya Roho haitakuwa na utukufu zaidi?
9 Бо як служі́ння о́суду — слава, то служіння праведности тим більше багате на славу!
Kwa kuwa kama huduma ya hukumu ilikuwa na utukufu, ni mara ngapi zaidi huduma ya haki huzidi sana katika utukufu!
10 Не просла́вилося бо прославлене, у цій частині, ради слави, що вона переважує,
Ni kweli kwamba, kile kilichofanywa utukufu kwanza hakina utukufu tena katika heshima hii, kwa sababu ya utukufu unaouzidi.
11 бо коли славне те, що минає, то багато більш у славі те, що триває!
Kwa kuwa kama kile ambacho kilikuwa kinapita kilikuwa na utukufu, ni kwa kiasi gani zaidi kile ambacho ni cha kudumu kitakuwa na utukufu!
12 Тож, мавши надію таку, ми вживаємо великої сміли́вости,
Kwa kuwa tunajiamini hiyo, tunaujasiri sana.
13 а не як Мойсей, що покрива́ло клав на обличчя своє, щоб Ізраїлеві сини не дивилися на кінець того, що минає.
Hatuko kama Musa, aliyeweka utaji juu ya uso wake, ili kwamba watu wa Israel wasiweze kuangalia moja kwa moja kwenye mwisho wa utukufu ambao ulikuwa unatoweka.
14 Але засліпилися їхні думки́, бо те саме покрива́ло аж до сьогодні лишилось незняте в чита́нні Старо́го Заповіту, бо зникає воно Христо́м.
Lakini fahamu zao zilikuwa zimefungwa. Hata mpaka siku hii utaji uleule bado unabaki juu ya usomaji wa agano la kale. Haijawekwa wazi, kwa sababu ni katika Kristo pekee inaondolewa mbali.
15 Але аж до сьогодні, як читають Мойсея, на їхньому серці лежить покрива́ло,
Lakini hata leo, wakati wowote Musa asomwapo, utaji hukaa juu ya mioyo yao.
16 „коли ж вони наве́рнуться до Господа, тоді покрива́ло здіймається“.
Lakini mtu anapogeuka kwa Bwana, utaji unaondolewa.
17 Госпо́дь же — то Дух, а де Дух Господній, — там воля.
Sasa Bwana ni Roho. Palipo na Roho wa Bwana, kuna uhuru.
18 Ми ж відкритим обличчям, як у дзеркало, дивимося всі на славу Господню, і зміняємося в той же образ від слави на славу, як від Духа Господнього.
Sasa sisi sote, pamoja na nyuso zisizo wekewa utaji, huona utukufu wa Bwana. Tunabadilishwa ndani ya muonekano uleule wa utukufu kutoka shahada moja ya utukufu kwenda nyingine, kama ilivyo kutoka kwa Bwana, ambaye ni Roho.

< 2 до коринтян 3 >