< Çölde Sayim 33 >

1 Musa'yla Harun önderliğinde birlikler halinde Mısır'dan çıkan İsrailliler sırasıyla aşağıdaki yolculukları yaptılar.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Musa RAB'bin buyruğu uyarınca sırasıyla yapılan yolculukları kayda geçirdi. Yapılan yolculuklar şunlardır:
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 İsrailliler Fısıh kurbanının ertesi günü –birinci ayın on beşinci günü– Mısırlılar'ın gözü önünde zafer havası içinde Ramses'ten yola çıktılar.
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 O sırada Mısırlılar RAB'bin yok ettiği ilk doğan çocuklarını gömüyorlardı; RAB onların ilahlarını yargılamıştı.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 İsrailliler Ramses'ten yola çıkıp Sukkot'ta konakladılar.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Sukkot'tan ayrılıp çöl kenarındaki Etam'da konakladılar.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Etam'dan ayrılıp Baal-Sefon'un doğusundaki Pi-Hahirot'a döndüler, Migdol yakınlarında konakladılar.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Pi-Hahirot'tan ayrılıp denizden çöle geçtiler. Etam Çölü'nde üç gün yürüdükten sonra Mara'da konakladılar.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Mara'dan ayrılıp on iki su kaynağı ve yetmiş hurma ağacı olan Elim'e giderek orada konakladılar.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Elim'den ayrılıp Kamış Denizi kıyısında konakladılar.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Kamış Denizi'nden ayrılıp Sin Çölü'nde konakladılar.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Sin Çölü'nden ayrılıp Dofka'da konakladılar.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Dofka'dan ayrılıp Aluş'ta konakladılar.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Aluş'tan ayrılıp Refidim'de konakladılar. Orada halk için içecek su yoktu.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Refidim'den ayrılıp Sina Çölü'nde konakladılar.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Sina Çölü'nden ayrılıp Kivrot-Hattaava'da konakladılar.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Kivrot-Hattaava'dan ayrılıp Haserot'ta konakladılar.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Haserot'tan ayrılıp Ritma'da konakladılar.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Ritma'dan ayrılıp Rimmon-Peres'te konakladılar.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Rimmon-Peres'ten ayrılıp Livna'da konakladılar.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Livna'dan ayrılıp Rissa'da konakladılar.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Rissa'dan ayrılıp Kehelata'da konakladılar.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Kehelata'dan ayrılıp Şefer Dağı'nda konakladılar.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Şefer Dağı'ndan ayrılıp Harada'da konakladılar.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Harada'dan ayrılıp Makhelot'ta konakladılar.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Makhelot'tan ayrılıp Tahat'ta konakladılar.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Tahat'tan ayrılıp Terah'ta konakladılar.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Terah'tan ayrılıp Mitka'da konakladılar.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Mitka'dan ayrılıp Haşmona'da konakladılar.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Haşmona'dan ayrılıp Moserot'ta konakladılar.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Moserot'tan ayrılıp Bene-Yaakan'da konakladılar.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Bene-Yaakan'dan ayrılıp Hor-Hagidgat'ta konakladılar.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Hor-Hagidgat'tan ayrılıp Yotvata'da konakladılar.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Yotvata'dan ayrılıp Avrona'da konakladılar.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Avrona'dan ayrılıp Esyon-Gever'de konakladılar.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Esyon-Gever'den ayrılıp Zin Çölü'nde –Kadeş'te– konakladılar.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Kadeş'ten ayrılıp Edom sınırındaki Hor Dağı'nda konakladılar.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Kâhin Harun RAB'bin buyruğu uyarınca Hor Dağı'na çıktı. İsrailliler'in Mısır'dan çıkışlarının kırkıncı yılı, beşinci ayın birinci günü orada öldü.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Hor Dağı'nda öldüğünde Harun 123 yaşındaydı.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Kenan ülkesinin Negev bölgesinde yaşayan Kenanlı Arat Kralı İsrailliler'in geldiğini duydu.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 İsrailliler Hor Dağı'ndan ayrılıp Salmona'da konakladılar.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Salmona'dan ayrılıp Punon'da konakladılar.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Punon'dan ayrılıp Ovot'ta konakladılar.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Ovot'tan ayrılıp Moav sınırındaki İye-Haavarim'de konakladılar.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 İyim'den ayrılıp Divon-Gad'da konakladılar.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Divon-Gad'dan ayrılıp Almon-Divlatayma'da konakladılar.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Almon-Divlatayma'dan ayrılıp Nevo yakınlarındaki Haavarim dağlık bölgesinde konakladılar.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Haavarim dağlık bölgesinden ayrılıp Şeria Irmağı yanında, Eriha karşısındaki Moav ovalarında konakladılar.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Şeria Irmağı boyunca Beythayeşimot'tan Avel-Haşşittim'e kadar Moav ovalarında konakladılar.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Orada, Şeria Irmağı yanında Eriha karşısındaki Moav ovalarında RAB Musa'ya şöyle dedi:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 “İsrailliler'e de ki, ‘Şeria Irmağı'ndan Kenan ülkesine geçince,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 ülkede yaşayan bütün halkı kovacaksınız. Oyma ve dökme putlarını yok edecek, tapınma yerlerini yıkacaksınız.
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Ülkeyi yurt edinecek, oraya yerleşeceksiniz; çünkü mülk edinesiniz diye orayı size verdim.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Ülkeyi boylarınız arasında kurayla paylaşacaksınız. Büyük boya büyük pay, küçük boya küçük pay vereceksiniz. Kurada kime ne çıkarsa, orası onun olacak. Dağıtımı atalarınızın oymaklarına göre yapacaksınız.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 “‘Ama ülkede yaşayanları kovmazsanız, orada bıraktığınız halk gözlerinizde kanca, böğürlerinizde diken olacak. Yaşayacağınız ülkede size sıkıntı verecekler.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 Ben de onlara yapmayı tasarladığımı size yapacağım.’”
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Çölde Sayim 33 >