< Levililer 1 >

1 RAB Musa'yı çağırıp Buluşma Çadırı'ndan ona şöyle seslendi:
Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
2 “İsrail halkıyla konuş, onlara de ki, ‘İçinizden biri RAB'be sunu olarak bir hayvan sunacağı zaman, sığır ya da davar sunmalı.
“Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
3 “‘Eğer yakmalık sunu sığırsa, kusursuz ve erkek olmalı. RAB'bin sunuyu kabul etmesi için onu Buluşma Çadırı'nın giriş bölümünde sunmalı.
“‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
4 Elini yakmalık sununun başına koymalı. Sunu kişinin günahlarının bağışlanması için kabul edilecektir.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
5 Boğayı RAB'bin önünde kesmeli. Harun soyundan gelen kâhinler boğanın kanını getirip Buluşma Çadırı'nın giriş bölümündeki sunağın her yanına dökecekler.
Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
6 Sonra kişi yakmalık sunuyu yüzüp parçalara ayırmalı.
Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
7 Kâhin Harun'un oğulları sunakta ateş yakıp üzerine odun dizecekler.
Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
8 Hayvanın başını, iç yağını, parçalarını sunakta yanan odunların üzerine yerleştirecekler.
Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
9 Kişi hayvanın işkembesini, bağırsaklarını ve ayaklarını yıkayacak. Kâhin de hepsini yakmalık sunu, yakılan sunu ve RAB'bi hoşnut eden koku olarak sunağın üzerinde yakacaktır.
Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
10 “‘Eğer kişi yakmalık sunu olarak davar, yani koyun ya da keçi sunmak istiyorsa, sunusu kusursuz ve erkek olmalı.
“‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
11 Onu sunağın kuzeyinde, RAB'bin önünde kesmeli. Harun soyundan gelen kâhinler kanı sunağın her yanına dökecekler.
Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
12 Kişi başını, iç yağını kesip hayvanı parçalara ayırmalı. Kâhin bunları sunakta yanan odunların üzerine yerleştirecek.
Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
13 Kişi hayvanın işkembesini, bağırsaklarını, ayaklarını yıkamalı. Kâhin bunları sunak üzerinde yakarak sunmalı. Bu yakmalık sunu, yakılan sunu ve RAB'bi hoşnut eden kokudur.
Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
14 “‘Eğer kişi yakmalık sunu olarak RAB'be kuş sunmak istiyorsa, kumru ya da güvercin sunmalı.
“‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
15 Kâhin sunuyu sunağa getirecek, başını ayırıp sunağın üzerinde yakacak. Kuşun kanı sunağın yan tarafından akıtılacak.
Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
16 Kâhin kuşun kursağını pisliğiyle birlikte çıkarıp sunağın doğusundaki küllüğe atacak.
Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
17 Kanatlarını tutarak kuşu ikiye bölecek, ama tümüyle ayırmayacak. Sonra kuşu sunakta yanan odunların üstünde yakmalı. Bu yakmalık sunu, yakılan sunu ve RAB'bi hoşnut eden kokudur.’”
Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.

< Levililer 1 >