< Çölde Sayim 28 >

1 RAB Musa'ya şöyle dedi:
Bwana akamwambia Mose,
2 “İsrailliler'e buyur ve de ki, ‘Bana sunacağınız sunuyu –yakılan sunu ve beni hoşnut eden koku olarak sunacağınız yiyeceği– belirlenen zamanda sunmaya dikkat edeceksiniz.’
“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
3 Onlara de ki, ‘RAB'be sunacağınız yakılan sunu şudur: Günlük yakmalık sunu olarak her gün bir yaşında kusursuz iki erkek kuzu sunacaksınız.
Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
4 Kuzunun birini sabah, öbürünü akşamüstü sunun.
Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
5 Kuzuyla birlikte tahıl sunusu olarak dörtte bir hin sıkma zeytinyağıyla yoğrulmuş onda bir efa ince un sunacaksınız.
kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
6 Günlük yakmalık sunu, Sina Dağı'nda başlatılan, RAB'bi hoşnut eden koku olarak yakılan sunudur.
Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
7 Kuzuyla birlikte dökmelik sunu olarak dörtte bir hin içki sunacaksınız. Dökmelik sunuyu RAB için kutsal yerde dökeceksiniz.
Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
8 Öbür kuzuyu akşamüstü, yakılan sunu ve RAB'bi hoşnut eden koku olarak, sabahki gibi tahıl sunusu ve dökmelik sunuyla birlikte bana sunacaksınız.’”
Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
9 “‘Şabat Günü bir yaşında kusursuz iki erkek kuzuyla birlikte tahıl sunusu olarak zeytinyağıyla yoğrulmuş onda iki efa ince un ve onun dökmelik sunusunu sunacaksınız.
“‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
10 Günlük yakmalık sunuyla dökmelik sunusu dışında, her Şabat Günü sunulan yakmalık sunu budur.’”
Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
11 “‘Her ayın ilk günü, RAB'be yakmalık sunu olarak iki boğa, bir koç ve bir yaşında kusursuz yedi erkek kuzu sunacaksınız.
“‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
12 Her boğayla birlikte tahıl sunusu olarak zeytinyağıyla yoğrulmuş onda üç efa ince un; koçla birlikte tahıl sunusu olarak zeytinyağıyla yoğrulmuş onda iki efa ince un;
Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
13 her kuzuyla da tahıl sunusu olarak zeytinyağıyla yoğrulmuş onda bir efa ince un sunacaksınız. Bu, yakmalık sunu, RAB'bi hoşnut eden koku, yakılan sunu olacaktır.
pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
14 Her boğayla dökmelik sunu olarak yarım hin, koçla üçte bir hin, her kuzuyla dörtte bir hin şarap sunacaksınız. Yıl boyunca her Yeni Ay'da yapılacak yakmalık sunu budur.
Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
15 Günlük yakmalık sunuyla dökmelik sunusu dışında, RAB'be günah sunusu olarak bir teke sunulacak.’”
Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
16 “‘RAB'bin Fısıh kurbanı birinci ayın on dördüncü günü kesilmelidir.
“‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
17 On beşinci gün bayram olacaktır; yedi gün mayasız ekmek yiyeceksiniz.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
18 İlk gün kutsal toplantı düzenleyecek, gündelik işlerinizi yapmayacaksınız.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
19 RAB için yakılan sunu, yakmalık sunu olarak iki boğa, bir koç ve bir yaşında yedi erkek kuzu sunacaksınız. Sunacağınız hayvanlar kusursuz olmalı.
Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
20 Her boğayla birlikte tahıl sunusu olarak zeytinyağıyla yoğrulmuş onda üç efa, koçla onda iki efa, her kuzuyla onda bir efa ince un sunacaksınız;
Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
22 günahlarınızı bağışlatmak için de günah sunusu olarak bir teke sunacaksınız.
Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 Her sabah sunacağınız günlük yakmalık sunuya ek olarak bunları da sunacaksınız.
Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
24 Böylece her gün RAB'bi hoşnut eden koku olarak yakılan yiyecek sunusunu yedi gün sunacaksınız. Bunu günlük yakmalık sunuyla dökmelik sunusuna ek olarak sunacaksınız.
Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
25 Yedinci gün kutsal toplantı düzenleyecek, gündelik işlerinizi yapmayacaksınız.’”
Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
26 “‘İlk ürünleri kutlama günü, Haftalar Bayramı'nda RAB'be yeni tahıl sunusu sunduğunuzda kutsal toplantı düzenleyecek, gündelik işlerinizi yapmayacaksınız.
“‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
27 RAB'bi hoşnut eden koku, yakmalık sunu olarak iki boğa, bir koç ve bir yaşında yedi erkek kuzu sunacaksınız.
Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
28 Her boğayla birlikte tahıl sunusu olarak zeytinyağıyla yoğrulmuş onda üç efa, koçla birlikte onda iki efa, her kuzuyla da onda bir efa ince un sunacaksınız;
Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
30 günahlarınızı bağışlatmak için de bir teke sunacaksınız.
Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 Günlük yakmalık sunuyla tahıl sunusuna ek olarak bunları dökmelik sunuyla birlikte sunacaksınız. Sunacağınız hayvanlar kusursuz olmalı.’”
Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

< Çölde Sayim 28 >