< Çölde Sayim 26 >

1 Ölümcül hastalık son bulunca RAB, Musa'yla Kâhin Harun oğlu Elazar'a, “İsrail topluluğunun ailelerine göre sayımını yapın” dedi, “Savaşabilecek durumdaki yirmi ve daha yukarı yaştaki bütün erkekleri sayın.”
Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
2
“Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
3 Bunun üzerine Musa'yla Kâhin Elazar, Şeria Irmağı'nın yanında, Eriha karşısındaki Moav ovalarında halka, “RAB'bin Musa'ya verdiği buyruk uyarınca, yirmi ve daha yukarı yaştaki erkekleri sayın” dediler. Mısır'dan çıkan İsrailliler şunlardı:
Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
4
“Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
5 İsrail'in ilk doğanı Ruben'in soyundan gelen Rubenoğulları: Hanok soyundan Hanok boyu, Pallu soyundan Pallu boyu,
Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
6 Hesron soyundan Hesron boyu, Karmi soyundan Karmi boyu.
kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
7 Ruben boyları bunlardı, sayıları 43 730 kişiydi.
Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
8 Pallu'nun oğlu Eliav,
Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
9 Eliav'ın oğulları Nemuel, Datan ve Aviram'dı. Bunlar topluluğun seçtiği, Musa'yla Harun'a, dolayısıyla RAB'be başkaldırarak Korah'ın yandaşlarına katılan Datan'la Aviram'dı.
nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
10 Yer yarılıp onları Korah'la birlikte yutunca yok oldular. Ateş Korah'ın iki yüz elli yandaşını yakıp yok etti. Böylece başkalarına bir uyarı oldular.
Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
11 Korah'ın oğulları ise ölmedi.
Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
12 Boylarına göre Şimonoğulları şunlardı: Nemuel soyundan Nemuel boyu, Yamin soyundan Yamin boyu, Yakin soyundan Yakin boyu,
Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
13 Zerah soyundan Zerah boyu, Şaul soyundan Şaul boyu.
kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
14 Şimon boyları bunlardı, sayıları 22 200 kişiydi.
Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
15 Boylarına göre Gadoğulları şunlardı: Sefon soyundan Sefon boyu, Hagi soyundan Hagi boyu, Şuni soyundan Şuni boyu,
Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
16 Ozni soyundan Ozni boyu, Eri soyundan Eri boyu,
kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
17 Arot soyundan Arot boyu, Areli soyundan Areli boyu.
kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
18 Gad boyları bunlardı, sayıları 40 500 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
19 Yahuda'nın iki oğlu Er'le Onan Kenan ülkesinde ölmüşlerdi.
Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
20 Boylarına göre Yahudaoğulları şunlardı: Şela soyundan Şela boyu, Peres soyundan Peres boyu, Zerah soyundan Zerah boyu.
Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
21 Peres soyundan gelenler şunlardı: Hesron soyundan Hesron boyu, Hamul soyundan Hamul boyu.
Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
22 Yahuda boyları bunlardı, sayıları 76 500 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
23 Boylarına göre İssakaroğulları şunlardı: Tola soyundan Tola boyu, Puvva soyundan Puvva boyu,
Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
24 Yaşuv soyundan Yaşuv boyu, Şimron soyundan Şimron boyu.
kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
25 İssakar boyları bunlardı, sayıları 64 300 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
26 Boylarına göre Zevulunoğulları şunlardı: Seret soyundan Seret boyu, Elon soyundan Elon boyu, Yahleel soyundan Yahleel boyu.
Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
27 Zevulun boyları bunlardı, sayıları 60 500 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
28 Boylarına göre Yusuf'un oğulları: Manaşşe ve Efrayim.
Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
29 Manaşşe soyundan gelenler: Makir soyundan Makir boyu –Makir Gilat'ın babasıydı– Gilat soyundan Gilat boyu.
Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
30 Gilat soyundan gelenler şunlardı: İezer soyundan İezer boyu, Helek soyundan Helek boyu,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
31 Asriel soyundan Asriel boyu, Şekem soyundan Şekem boyu,
kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
32 Şemida soyundan Şemida boyu, Hefer soyundan Hefer boyu.
kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
33 Hefer oğlu Selofhat'ın oğulları olmadı; yalnız Mahla, Noa, Hogla, Milka ve Tirsa adında kızları vardı.
(Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
34 Manaşşe boyları bunlardı, sayıları 52 700 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
35 Boylarına göre Efrayim soyundan gelenler şunlardı: Şutelah soyundan Şutelah boyu, Beker soyundan Beker boyu, Tahan soyundan Tahan boyu.
Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
36 Şutelah soyundan gelenler şunlardı: Eran soyundan Eran boyu.
Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
37 Efrayim boyları bunlardı, sayıları 32 500 kişiydi. Boylarına göre Yusuf'un soyundan gelenler bunlardı.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
38 Boylarına göre Benyamin soyundan gelenler: Bala soyundan Bala boyu, Aşbel soyundan Aşbel boyu, Ahiram soyundan Ahiram boyu,
Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
39 Şufam soyundan Şufam boyu, Hufam soyundan Hufam boyu.
kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
40 Bala'nın oğulları Ard'la Naaman'dı. Ard soyundan Ard boyu, Naaman soyundan Naaman boyu.
Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
41 Boylarına göre Benyamin soyundan gelenler bunlardı, sayıları 45 600 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
42 Boylarına göre Dan soyundan gelenler şunlardı: Şuham soyundan Şuham boyu. Dan boyu buydu.
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
43 Hepsi Şuham boyundandı, sayıları 64 400 kişiydi.
Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
44 Boylarına göre Aşer soyundan gelenler: Yimna soyundan Yimna boyu, Yişvi soyundan Yişvi boyu, Beria soyundan Beria boyu.
Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
45 Beria soyundan gelenler: Hever soyundan Hever boyu, Malkiel soyundan Malkiel boyu.
kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
46 Aşer'in Serah adında bir kızı vardı.
(Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
47 Aşer boyları bunlardı, sayıları 53 400 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
48 Boylarına göre Naftali soyundan gelenler: Yahseel soyundan Yahseel boyu, Guni soyundan Guni boyu,
Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
49 Yeser soyundan Yeser boyu, Şillem soyundan Şillem boyu.
kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
50 Boylarına göre Naftali boyları bunlardı, sayıları 45 400 kişiydi.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
51 Sayılan İsrailliler'in toplamı 601 730 erkekti.
Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
52 RAB Musa'ya şöyle dedi:
Bwana akamwambia Mose,
53 “Adlarının sayısına göre ülke bunlara pay olarak bölüştürülecek.
“Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
54 Sayıca çok olana büyük, sayıca az olana küçük pay vereceksin. Her oymağa kişi sayısına göre pay verilecek.
Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
55 Ancak ülke kura ile dağıtılacak. Herkesin payı, ata oymağının adına göre olacak.
Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
56 Küçük, büyük her oymağın payı kurayla dağıtılacak.”
Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
57 Boylarına göre sayılan Levililer şunlardı: Gerşon soyundan Gerşon boyu, Kehat soyundan Kehat boyu, Merari soyundan Merari boyu.
Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
58 Şunlar da Levili boylardı: Livni boyu, Hevron boyu, Mahli boyu, Muşi boyu, Korah boyu. Kehat Amram'ın babasıydı.
Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
59 Amram'ın karısı Mısır'da doğan, Levi soyundan gelme Yokevet'ti. Amram'a Harun'u, Musa'yı ve kızkardeşleri Miryam'ı doğurdu.
jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
60 Harun Nadav, Avihu, Elazar ve İtamar'ın babasıydı.
Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
61 Nadav'la Avihu RAB'bin önünde kurallara aykırı bir ateş sunarken öldüler.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
62 Levililer'den sayılan bir aylık ve daha yukarı yaştaki bütün erkekler 23 000 kişiydi. Bunlar öbür İsrailliler'le birlikte sayılmadılar. Çünkü öbür İsrailliler arasında onlara pay verilmemişti.
Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
63 Şeria Irmağı yanında, Eriha karşısındaki Moav ovalarında Musa'yla Kâhin Elazar'ın saydıkları İsrailliler bunlardı.
Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
64 Ancak, bu sayılanların arasında Musa'yla Kâhin Harun'un Sina Çölü'nde saymış olduğu İsrailliler'den kimse yoktu.
Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
65 Çünkü RAB o dönemde sayımı yapılan İsrailliler'in kesinlikle çölde öleceğini söylemişti. Onlardan Yefunne oğlu Kalev'le Nun oğlu Yeşu'dan başka kimse sağ kalmamıştı.
Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.

< Çölde Sayim 26 >