< Çölde Sayim 18 >

1 RAB Harun'a, “Sen, oğulların ve ailen kutsal yere ilişkin suçtan sorumlu tutulacaksınız” dedi, “Kâhinlik görevinizle ilgili suçtan da sen ve oğulların sorumlu tutulacaksınız.
Bwana akamwambia Aroni, “Wewe, wanao na jamaa ya baba yako mtawajibika kwa makosa dhidi ya mahali patakatifu, na wewe na wanao peke yenu ndio mtakaowajibika kwa makosa dhidi ya ukuhani.
2 Sen ve oğulların Levha Sandığı'nın bulunduğu çadırın önünde hizmet ederken, atanız Levi'nin oymağından kardeşlerinizin de size katılıp yardım etmelerini sağlayın.
Walete Walawi wenzako kutoka kabila la baba zako ili waungane nanyi na kuwasaidia wakati wewe na wanao mnapohudumu mbele ya Hema la Ushuhuda.
3 Senin sorumluluğun altında çadırda hizmet etsinler. Ancak, siz de onlar da ölmeyesiniz diye kutsal yerin eşyalarına ya da sunağa yaklaşmasınlar.
Watawajibika kwenu na watafanya kazi zote za Hema, lakini kamwe wasisogelee vifaa vya patakatifu au madhabahu, la sivyo wao na ninyi mtakufa.
4 Seninle çalışacak ve Buluşma Çadırı'yla ilgili bütün hizmetlerden sorumlu olacaklar. Levililer dışında hiç kimse bulunduğunuz yere yaklaşmayacak.
Watajiunga nanyi na watawajibika kwa utunzaji wa Hema la Kukutania, yaani kazi zote kwenye Hema, wala hakuna mtu mwingine yeyote atakayeweza kusogea karibu hapo mlipo.
5 “Bundan sonra İsrail halkına öfkelenmemem için kutsal yerin ve sunağın hizmetinden sizler sorumlu olacaksınız.
“Mtawajibika katika utunzaji wa mahali patakatifu na madhabahu, ili kwamba ghadhabu isiwaangukie Waisraeli tena.
6 Ben İsrailliler arasından Levili kardeşlerinizi size bir armağan olarak seçtim. Buluşma Çadırı'yla ilgili hizmeti yapmaları için onlar bana adanmıştır.
Mimi mwenyewe nimewachagua Walawi wenzenu kutoka miongoni mwa Waisraeli kama zawadi kwenu, waliowekwa wakfu kwa Bwana ili kufanya kazi katika Hema la Kukutania.
7 Ama sunaktaki ve perdenin ötesindeki kâhinlik görevini sen ve oğulların üstleneceksiniz. Kâhinlik görevini size armağan olarak veriyorum. Sizden başka kutsal yere kim yaklaşırsa öldürülecektir.”
Lakini ni wewe tu na wanao mtakaoweza kutumika kama makuhani kuhusiana na kila kitu kwenye madhabahu na ndani ya pazia. Ninawapa utumishi wa ukuhani kama zawadi. Mtu mwingine yeyote atakayekaribia mahali patakatifu ni lazima auawe.”
8 RAB Harun'la konuşmasını şöyle sürdürdü: “Bana sunulan kutsal sunuların bağış kısımlarını sana veriyorum. Bunları sonsuza dek pay olarak sana ve oğullarına veriyorum.
Kisha Bwana akamwambia Aroni, “Mimi mwenyewe nimekuweka kuwa mwangalizi wa sadaka zote zitakazotolewa kwangu; matoleo yote matakatifu Waisraeli wanayonipa ninakupa wewe na wanao kama sehemu yenu na fungu lenu la kawaida.
9 Sunakta tümüyle yakılmayan, bana sunulan en kutsal sunulardan şunlar senin olacak: Tahıl, suç ve günah sunuları. En kutsal sunular senin ve oğullarının olacak.
Mtachukua sehemu ya yale matoleo matakatifu sana ambayo hayateketezwi kwa moto. Kutoka kwa matoleo yote wanayoniletea kama sadaka takatifu sana, ziwe za nafaka, au za dhambi, au za makosa, sehemu ile itakuwa yako na wanao.
10 Bunları en kutsal sunu olarak yiyeceksin. Her erkek onlardan yiyebilir. Onları kutsal sayacaksın.
Mtaila kama kitu kilicho kitakatifu sana; kila mwanaume ataila. Ni lazima mtaiheshimu kama takatifu.
11 “Ayrıca şunlar da senin olacak: İsrailliler'in sunduğu sallamalık sunuların bağış kısımlarını sonsuza dek pay olarak sana, oğullarına ve kızlarına veriyorum. Ailende dinsel açıdan temiz olan herkes onları yiyebilir.
“Hiki pia ni chako: chochote kilichotengwa kutoka kwenye matoleo yote ya sadaka za kuinuliwa za Waisraeli. Ninakupa wewe haya, wana na binti zako kama sehemu yenu ya kawaida. Kila mmoja wa nyumba yako ambaye ni safi kwa taratibu za ibada anaweza kuyala.
12 “RAB'be verdikleri ilk ürünleri –zeytinyağının, yeni şarabın, tahılın en iyisini– sana veriyorum.
“Ninawapa mafuta ya zeituni yaliyo bora kuliko yote, na divai mpya iliyo bora kuliko zote na nafaka wanazompa Bwana kama malimbuko katika mavuno yao.
13 Ülkede yetişen ilk ürünlerden RAB'be getirdiklerinin tümü senin olacak. Ailende dinsel açıdan temiz olan herkes onları yiyebilir.
Malimbuko yote ya nchi ambayo wanamletea Bwana yatakuwa yenu. Kila mmoja nyumbani kwako ambaye ni safi kwa taratibu za Ibada anaweza kula.
14 “İsrail'de RAB'be koşulsuz adanan her şey senin olacak.
“Kila kitu katika Israeli ambacho kimetolewa kwa Bwana ni chenu.
15 İnsan olsun hayvan olsun RAB'be adanan her rahmin ilk ürünü senin olacak. Ancak ilk doğan her çocuk ve kirli sayılan hayvanların her ilk doğanı için kesinlikle bedel alacaksın.
Kila mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa mnyama, ambaye ametolewa kwa Bwana ni wenu. Lakini ni lazima mtamkomboa kila mwana mzaliwa wa kwanza na kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wasio safi.
16 İlk doğanlar bir aylıkken, kendi biçeceğin değer uyarınca, yirmi geradan oluşan kutsal yerin şekeline göre beş şekel gümüş bedel alacaksın.
Watakapokuwa na umri wa mwezi mmoja, ni lazima mtawakomboa kwa bei ya ukombozi iliyowekwa, kwa shekeli tano za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, yenye uzito wa gera ishirini.
17 “Ancak sığırın, koyunun ya da keçinin ilk doğanı için bedel almayacaksın. Onlar benim için ayrılmıştır. Kanlarını sunağın üzerine dökeceksin, yağlarını RAB'bi hoşnut eden koku olsun diye yakılan bir sunu olarak yakacaksın.
“Lakini kamwe usimkomboe mzaliwa wa kwanza wa maksai, kondoo au mbuzi; hawa ni watakatifu. Nyunyizia damu yao juu ya madhabahu na uchome mafuta yao kama sadaka itolewayo kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
18 Sallamalık sununun göğsü ve sağ budu senin olduğu gibi eti de senin olacak.
Nyama zao zitakuwa chakula chenu, kama ilivyokuwa kidari cha kuinuliwa na paja la mguu wa kulia.
19 İsrailliler'in bana sundukları kutsal sunuların bağış kısımlarını sonsuza dek pay olarak sana, oğullarına ve kızlarına veriyorum. Senin ve soyun için bu RAB'bin önünde sonsuza dek sürecek bozulmaz bir antlaşmadır.”
Chochote kitakachotengwa kutoka sadaka takatifu ambazo Waisraeli wanamtolea Bwana, ninakupa wewe, wanao na binti zako kama fungu lenu la kawaida. Ni Agano la milele la chumvi mbele za Bwana kwako na watoto wako.”
20 RAB Harun'la konuşmasını şöyle sürdürdü: “Onların ülkesinde mirasın olmayacak, aralarında hiçbir payın olmayacak. İsrailliler arasında payın ve mirasın benim.
Bwana akamwambia Aroni, “Hutakuwa na urithi wowote katika nchi yao, wala hutakuwa na sehemu miongoni mwao; Mimi ni fungu lako na urithi wako miongoni mwa Waisraeli.
21 “Buluşma Çadırı'yla ilgili yaptıkları hizmete karşılık, İsrail'de toplanan bütün ondalıkları pay olarak Levililer'e veriyorum.
“Ninawapa Walawi zaka yote katika Israeli kama urithi wao kuwa kama malipo kwa kazi wanayoifanya wakati wanapohudumu katika Hema la Kukutania.
22 Bundan böyle öbür İsrailliler Buluşma Çadırı'na yaklaşmamalı. Yoksa günahlarının bedelini canlarıyla öderler.
Kuanzia sasa, kamwe Waisraeli wasisogelee karibu na Hema la Kukutania, la sivyo watabeba matokeo ya dhambi zao, nao watakufa.
23 Buluşma Çadırı'yla ilgili hizmeti Levililer yapacak, çadıra karşı işlenen suçtan onlar sorumlu olacak. Gelecek kuşaklarınız boyunca kalıcı bir kural olacak bu. İsrailliler arasında onların payı olmayacak.
Ni Walawi watakaofanya kazi katika Hema la Kukutania na kubeba wajibu wa makosa dhidi yake. Hili ni agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo. Hawatapokea urithi wowote miongoni mwa Waisraeli.
24 Bunun yerine İsrailliler'in RAB'be armağan olarak verdiği ondalığı miras olarak Levililer'e veriyorum. Bu yüzden Levililer için, ‘İsrailliler arasında onların mirası olmayacak’ dedim.”
Badala yake, ninawapa Walawi zaka zote zinazotolewa na Waisraeli kama sadaka kwa Bwana kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu nimesema hivi kuhusu wao: ‘Hawatakuwa na urithi miongoni mwa Waisraeli.’”
25 RAB Musa'ya şöyle dedi:
Bwana akamwambia Mose,
26 “Levililer'e de ki, ‘Pay olarak size verdiğim ondalıkları İsrailliler'den alınca, aldığınız ondalığın ondalığını RAB'be armağan olarak sunacaksınız.
“Sema na Walawi na uwaambie: ‘Mtakapopokea zaka kutoka kwa Waisraeli ambayo ninawapa kama urithi wenu kutoka kwao, ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya hiyo zaka kama sadaka kwa Bwana, iwe zaka ya hiyo zaka.
27 Armağanınız harmandan tahıl ya da üzüm sıkma çukurundan bir armağan sayılacaktır.
Sadaka yenu itahesabiwa kwenu kama nafaka kutoka sakafu ya kupuria, au divai kutoka kwenye shinikizo la kukamulia zabibu.
28 Böylelikle siz de İsrailliler'den aldığınız bütün ondalıklardan RAB'be armağan sunacaksınız. Bu ondalıklardan RAB'bin armağanını Kâhin Harun'a vereceksiniz.
Kwa njia hii, ninyi pia mtatoa sadaka kwa Bwana kutoka zaka zote mtakazopokea kutoka kwa Waisraeli. Kutoka kwenye zaka hizi, ni lazima mtoe sehemu ya Bwana kwa Aroni, kuhani.
29 Aldığınız bütün armağanlardan RAB için bir armağan ayıracaksınız; hepsinin en iyisini, en kutsalını ayıracaksınız.’
Ni lazima mtoe kama sehemu ya Bwana iliyo nzuri sana tena ile sehemu iliyo takatifu sana kuliko zote ya kile kitu mlichopewa.’
30 “Levililer'e şöyle de: ‘En iyisini sunduğunuzda, geri kalanı harman ya da asma ürünü olarak size sayılacaktır.
“Waambie Walawi: ‘Mtakapotoa sehemu zilizo bora sana, itahesabiwa kwenu kama mazao ya sakafu ya kupuria nafaka, au ya shinikizo la kukamulia zabibu.
31 Siz ve aileniz her yerde ondan yiyebilirsiniz. Buluşma Çadırı'nda yaptığınız hizmete karşılık size verilen ücrettir bu.
Ninyi na watu wa nyumbani mwenu mnaweza kula sehemu iliyobaki mahali popote, kwani ndio ujira wenu kwa ajili ya kazi yenu katika Hema la Kukutania.
32 En iyisini sunarsanız, bu konuda günah işlememiş olursunuz. Ölmemek için İsrailliler'in sunduğu kutsal sunuları kirletmeyeceksiniz.’”
Kwa kutoa sehemu zake zilizo bora sana, hamtakuwa na hatia katika jambo hili; ndipo hamtatia unajisi sadaka takatifu za Waisraeli, nanyi hamtakufa.’”

< Çölde Sayim 18 >