< Yeşaya 41 >

1 RAB diyor ki, “Susun karşımda, ey kıyı halkları! Halklar güçlerini tazelesin, Öne çıkıp konuşsunlar. Yargı için bir araya gelelim.
“Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
2 “Doğudan adaleti harekete geçiren, Hizmete koşan kim? Ulusları önüne katıyor, krallara baş eğdiriyor. Kılıcıyla toz ediyor onları, Yayıyla savrulan samana çeviriyor.
“Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
3 Kovalıyor onları, Ayak basmadığı bir yoldan esenlikle geçiyor.
Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
4 Bunları yapıp gerçekleştiren, Kuşakları başlangıçtan beri çağıran kim? Ben RAB, ilkim; sonuncularla da yine Ben olacağım.”
Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
5 Kıyı halkları bunu görüp korktu. Dünyanın dört bucağı titriyor. Yaklaşıyor, geliyorlar.
Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
6 Herkes komşusuna yardım ediyor, Kardeşine, “Güçlü ol” diyor.
kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
7 Zanaatçı kuyumcuyu yüreklendiriyor, Madeni çekiçle düzleyen, “Lehim iyi oldu” diyerek örse vuranı yüreklendiriyor. Kımıldamasın diye putu yerine çiviliyor.
Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
8 “Ama sen, ey kulum İsrail, Seçtiğim Yakup soyu, Dostum İbrahim'in torunları!
“Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
9 Sizleri dünyanın dört bucağından topladım, En uzak yerlerden çağırdım. Dedim ki, ‘Sen kulumsun, seni seçtim, Seni reddetmedim.’
nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
10 Korkma, çünkü ben seninleyim, Yılma, çünkü Tanrın benim. Seni güçlendireceğim, evet, sana yardım edeceğim; Zafer kazanan sağ elimle sana destek olacağım.
Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
11 “Sana öfkelenenlerin hepsi utanacak, rezil olacak. Sana karşı çıkanlar hiçe sayılıp yok olacak.
“Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
12 Seninle çekişenleri arasan da bulamayacaksın. Seninle savaşanlar hiçten beter olacak.
Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
13 Çünkü sağ elinden tutan, ‘Korkma, sana yardım edeceğim’ diyen Tanrın RAB benim.
Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
14 “Ey Yakup soyu, toprak kurdu, Ey İsrail halkı, korkma! Sana yardım edeceğim” diyor RAB, Seni kurtaran İsrail'in Kutsalı.
Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
15 “İşte, seni dişli, keskin, yepyeni bir harman düveni yaptım. Harman edip ufalayacaksın dağları, Tepeleri samana çevireceksin.
“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
16 Onları savurduğunda rüzgar alıp götürecek, Darmadağın edecek hepsini kasırga. Sense RAB'de sevinç bulacak, İsrail'in Kutsalı'yla övüneceksin.
Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
17 “Düşkünlerle yoksullar su arıyor, ama yok. Dilleri kurumuş susuzluktan. Ben RAB, onları yanıtlayacağım, Ben, İsrail'in Tanrısı, onları bırakmayacağım.
“Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
18 Çıplak tepeler üzerinde ırmaklar, Vadilerde su kaynakları yapacağım. Çölü havuza, Kurak toprağı pınara çevireceğim.
Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
19 Çölü sedir, akasya, Mersin ve iğde ağaçlarına kavuşturacağım. Bozkıra çam, köknar Ve selviyi bir arada dikeceğim.
Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
20 Öyle ki, insanlar görüp bilsinler, Hep birlikte düşünüp anlasınlar ki, Bütün bunları RAB'bin eli yapmış, İsrail'in Kutsalı yaratmıştır.”
ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
21 “Davanızı sunun” diyor RAB, “Kanıtlarınızı ortaya koyun” diyor Yakup'un Kralı,
Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
22 “Putlarınızı getirin de olacakları bildirsinler bize. Olup bitenleri bildirsinler ki düşünelim, Sonuçlarını bilelim. Ya da gelecekte olacakları duyursunlar bize.
“Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
23 Ey putlar, bundan sonra olacakları bize bildirin de, İlah olduğunuzu bilelim! Haydi bir iyilik ya da kötülük edin de, Hepimiz korkup dehşete düşelim.
tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
24 Siz de yaptıklarınız da hiçten betersiniz, Sizi yeğleyen iğrençtir.
Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
25 “Kuzeyden birini harekete geçirdim, geliyor, Gün doğusundan beni adımla çağıran biri. Çömlekçinin balçığı çiğnediği gibi, Önderleri çamur gibi çiğneyecek ayağıyla.
“Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
26 Hanginiz bunu başlangıçtan bildirdi ki, bilelim, Kim önceden bildirdi ki, ‘Haklısın’ diyelim? Konuştuğunuzu bildiren de Duyuran da Duyan da olmadı hiç.
Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
27 Siyon'a ilk, ‘İşte, geldiler’ diyen benim. Yeruşalim'e müjdeci gönderdim.
Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
28 Bakıyorum, aralarında öğüt verebilecek kimse yok ki, Onlara danışayım, onlar da yanıtlasınlar.
Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
29 Hepsi bomboş, yaptıkları da bir hiç. Halkın putları yalnızca yeldir, sıfırdır.”
Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.

< Yeşaya 41 >