< Yeşaya 40 >

1 “Avutun halkımı” diyor Tanrınız, “Avutun!
Wafarijini, wafarijini watu wangu, asema Mungu wenu.
2 Yeruşalim halkına dokunaklı sözler söyleyin. Angaryanın bittiğini, Suçlarının cezasını ödediklerini, Günahlarının cezasını RAB'bin elinden İki katıyla aldıklarını ilan edin.”
Sema na Yerusalemu kwa upole, umtangazie kwamba kazi yake ngumu imekamilika, kwamba dhambi yake imefanyiwa fidia, kwamba amepokea kutoka mkononi mwa Bwana maradufu kwa ajili ya dhambi zake zote.
3 Şöyle haykırıyor bir ses: “Çölde RAB'bin yolunu hazırlayın, Bozkırda Tanrımız için düz bir yol açın.
Sauti ya mtu aliaye: “Itengenezeni jangwani njia ya Bwana, nyoosheni njia kuu nyikani kwa ajili ya Mungu wetu.
4 Her vadi yükseltilecek, Her dağ, her tepe alçaltılacak. Böylelikle engebeler düzleştirilecek, Sarp yerler ovaya dönüştürülecek.
Kila bonde litainuliwa, kila mlima na kilima kitashushwa; penye mabonde patanyooshwa, napo palipoparuza patasawazishwa.
5 O zaman RAB'bin yüceliği görünecek, Bütün insanlar hep birlikte onu görecek. Bunu söyleyen RAB'dir.”
Utukufu wa Bwana utafunuliwa, nao wanadamu wote watauona pamoja. Kwa maana kinywa cha Bwana kimenena.”
6 Ses, “Duyur” diyor. “Neyi duyurayım?” diye soruyorum. “İnsan soyu ota benzer, Bütün vefası kır çiçeği gibidir.
Sauti husema, “Piga kelele.” Nami nikasema, “Nipige kelele gani?” “Wanadamu wote ni kama majani, nao utukufu wao wote ni kama maua ya kondeni.
7 RAB'bin soluğu esince üzerlerine, Ot kurur, çiçek solar. Gerçekten de halk ottan farksızdır.
Majani hunyauka na maua huanguka, kwa sababu pumzi ya Bwana huyapuliza. Hakika wanadamu ni majani.
8 Ot kurur, çiçek solar, Ama Tanrımız'ın sözü sonsuza dek durur.”
Majani hunyauka na maua huanguka, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.”
9 Ey Siyon'a müjde getiren, Yüksek dağa çık! Ey Yeruşalim'e müjde getiren, Yükselt sesini, bağır, Sesini yükselt, korkma. Yahuda kentlerine, “İşte, Tanrınız!” de.
Wewe uletaye habari njema Sayuni, panda juu ya mlima mrefu. Wewe uletaye habari njema Yerusalemu, inua sauti yako kwa kupiga kelele, inua sauti, usiogope; iambie miji ya Yuda, “Yuko hapa Mungu wenu!”
10 İşte Egemen RAB gücüyle geliyor, Kudretiyle egemenlik sürecek. Ücreti kendisiyle birlikte, Ödülü önündedir.
Tazameni, Bwana Mwenyezi anakuja na nguvu, nao mkono wake ndio utawalao kwa ajili yake. Tazameni, ujira wake u pamoja naye, nayo malipo yake yanafuatana naye.
11 Sürüsünü çoban gibi güdecek, Kollarına alacak kuzuları, Bağrında taşıyacak; Usul usul yol gösterecek emziklilere.
Huchunga kundi lake kama mchungaji wa mifugo: Hukusanya wana-kondoo katika mikono yake na kuwachukua karibu na moyo wake, huwaongoza taratibu wale wanyonyeshao.
12 Kim denizleri avucuyla, Gökleri karışıyla ölçebildi? Yerin toprağını ölçeğe sığdıran, Dağları kantarla, Tepeleri teraziyle tartabilen var mı?
Ni nani aliyepima maji ya bahari kwenye konzi ya mkono wake, au kuzipima mbingu kwa shibiri yake? Ni nani aliyeyashika mavumbi ya dunia katika kikapu, au kupima milima kwenye kipimio na vilima kwenye mizani?
13 RAB'bin düşüncesine kim akıl erdirebildi? O'na öğüt verip öğretebilen var mı?
Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana, au kumfundisha akiwa kama mshauri wake?
14 Akıl almak, adalet yolunu öğrenmek için RAB kime danıştı ki? O'na bilgi veren, anlayış yolunu bildiren var mı?
Ni nani ambaye Bwana ametaka shauri kwake ili kumwelimisha, naye ni nani aliyemfundisha njia iliyo sawa? Ni nani aliyemfundisha maarifa au kumwonyesha mapito ya ufahamu?
15 RAB için uluslar kovada bir damla su, Terazideki toz zerreciği gibidir. Adaları ince toz gibi tartar.
Hakika mataifa ni kama tone ndani ya ndoo, ni kama vumbi jembamba juu ya mizani, huvipima visiwa kana kwamba vilikuwa vumbi laini.
16 Adakları yakmaya yetmez Lübnan ormanı, Yakmalık sunu için az gelir hayvanları.
Lebanoni hautoshi kwa moto wa madhabahuni, wala wanyama wake hawatoshi kwa sadaka za kuteketezwa.
17 RAB'bin önünde bütün uluslar bir hiç gibidir, Hiçten bile aşağı, değersiz sayılır.
Mbele yake mataifa yote ni kama si kitu, yanaonekana yasio na thamani na zaidi ya bure kabisa.
18 Öyleyse Tanrı'yı kime benzeteceksiniz? Neyle karşılaştıracaksınız O'nu?
Basi, utamlinganisha Mungu na nani? Utamlinganisha na kitu gani?
19 Putu döküm işçisi yapar, Kuyumcu altınla kaplar, Gümüş zincirler döker.
Kwa habari ya sanamu, fundi huisubu, naye mfua dhahabu huifunika kwa dhahabu na kuitengenezea mikufu ya fedha.
20 Böyle bir sunuya gücü yetmeyen yoksul kişi Çürümez bir ağaç parçası seçer. Yerinden kımıldamaz bir put yapsın diye Usta bir işçi arar.
Mtu aliye maskini sana asiyeweza kuleta sadaka kama hii huuchagua mti usiooza. Humtafuta fundi stadi wa kusimamisha sanamu ambayo haitatikisika.
21 Bilmiyor musunuz, duymadınız mı? Başlangıçtan beri size bildirilmedi mi? Dünyanın temelleri atılalı beri anlamadınız mı?
Je, hujui? Je, hujasikia? Je, hujaambiwa tangu mwanzo? Je, hujafahamu tangu kuumbwa kwa dunia?
22 Gökkubbenin üstünde oturan RAB'dir, Yeryüzünde yaşayanlarsa çekirge gibidir. Gökleri perde gibi geren, Oturmak için çadır gibi kuran O'dur.
Anakaa kwenye kiti cha enzi juu ya duara ya dunia, nao watu wakaao ndani yake ni kama panzi. Huzitandaza mbingu kama chandarua, na kuzitandaza kama hema la kuishi.
23 O'dur önderleri bir hiç eden, Dünyanın egemenlerini sıfıra indirgeyen.
Huwafanya wakuu kuwa si kitu, na kuwashusha watawala wa dunia hii kuwa kitu bure.
24 O önderler ki, yeni dikilmiş, yeni ekilmiş ağaç gibi, Gövdeleri yere yeni kök salmışken RAB'bin soluğu onları kurutuverir, Kasırga saman gibi savurur.
Mara baada ya kupandwa, mara baada ya kutiwa ardhini, mara baada ya kutoa mizizi yao ardhini, ndipo huwapulizia nao wakanyauka, nao upepo wa kisulisuli huwapeperusha kama makapi.
25 “Beni kime benzeteceksiniz ki, Eşitim olsun?” diyor Kutsal Olan.
“Utanilinganisha mimi na nani? Au ni nani anayelingana nami?” asema yeye Aliye Mtakatifu.
26 Başınızı kaldırıp göklere bakın. Kim yarattı bütün bunları? Yıldızları sırayla görünür kılıyor, Her birini adıyla çağırıyor. Büyük kudreti, üstün gücü sayesinde hepsi yerli yerinde duruyor.
Inueni macho yenu mtazame mbinguni: Ni nani aliyeumba hivi vyote? Ni yeye aletaye nje jeshi la nyota moja baada ya nyingine na kuziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu ya uweza wake mkuu na nguvu zake kuu, hakuna hata mojawapo inayokosekana.
27 Ey Yakup soyu, ey İsrail! Neden, “RAB başıma gelenleri görmüyor, Tanrı hakkımı gözetmiyor?” diye yakınıyorsun?
Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa Bwana asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?”
28 Bilmiyor musun, duymadın mı? Ebedi Tanrı, RAB, bütün dünyayı yaratan, Ne yorulur ne de zayıflar, O'nun bilgisi kavranamaz.
Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? Bwana ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake.
29 Yorulanı güçlendirir, Takati olmayanın kudretini artırır.
Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu.
30 Gençler bile yorulup zayıf düşer, Yiğitler tökezleyip düşerler.
Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,
31 RAB'be umut bağlayanlarsa taze güce kavuşur, Kanat açıp yükselirler kartallar gibi. Koşar ama zayıf düşmez, Yürür ama yorulmazlar.
bali wale wamtumainio Bwana atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

< Yeşaya 40 >