< Misir'Dan Çikiş 39 >

1 Kutsal yerde hizmet için lacivert, mor, kırmızı iplikten özenle dokunmuş giysiler yaptılar. Ayrıca RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi Harun'a kutsal giysiler yapıldı.
Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
2 Efodu altın sırmayla lacivert, mor, kırmızı iplikle, özenle dokunmuş ince ketenden yaptılar.
Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
3 Altını ince tabakalar halinde dövüp lacivert, mor, kırmızı iplik ve ince keten arasına ustaca işlemek için tel tel kestiler.
Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
4 Efodun iki köşesine tutturulmuş omuzluklar yaparak birleştirdiler.
Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
5 Efodun üzerindeki ustaca dokunmuş şerit efodun bir parçası gibi altın sırmayla lacivert, mor, kırmızı iplikle, özenle dokunmuş ince ketendendi; tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibiydi.
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
6 Altın yuvalar içine kakılmış, üzerine İsrailoğulları'nın adları mühür gibi oyulmuş oniksi işleyip
Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
7 İsrailliler'in anılması için efodun omuzluklarına taktılar. Tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi yaptılar.
Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
8 Efod gibi altın sırmayla lacivert, mor, kırmızı iplikle, özenle dokunmuş ince ketenden usta işi bir göğüslük yaptılar.
Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
9 Dört köşe, eni ve boyu birer karıştı, ikiye katlanmıştı.
Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
10 Üzerine dört sıra taş yuvası kaktılar. Birinci sırada yakut, topaz, zümrüt;
Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
11 ikinci sırada firuze, laciverttaşı, aytaşı;
safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
12 üçüncü sırada gökyakut, agat, ametist;
safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
13 dördüncü sırada sarı yakut, oniks, yeşim vardı. Taşlar altın yuvalara kakılmıştı.
katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
14 On iki taş vardı. Üzerlerine mühür oyar gibi İsrailoğulları'nın adları bir bir oyulmuştu. Bu taşlar İsrail'in on iki oymağını simgeliyordu.
Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
15 Göğüslük için saf altından örme zincirler yaptılar.
Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
16 İkişer tane altın yuva ve halka yaptılar. Göğüslüğün üst iki köşesine birer halka koydular.
Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
17 İki örme altın zinciri göğüslüğün köşelerindeki halkalara taktılar.
Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
18 Zincirlerin öteki iki ucunu iki yuvanın üzerinden geçirerek efodun ön tarafına, omuzlukların üzerine bağladılar.
nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
19 İki altın halka yaparak göğüslüğün alt iki köşesine, efoda bitişik iç kenarına taktılar.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
20 İki altın halka daha yaparak efodun önündeki omuzluklara alttan, dikişe yakın, ustaca dokunmuş şeridin yukarısına taktılar.
Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
21 Göğüslüğün halkalarıyla efodun halkalarını lacivert kordonla birbirine bağladılar. Öyle ki, göğüslük efodun ustaca dokunmuş şeridinin yukarısında kalsın ve efoddan ayrılmasın. Tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi yaptılar.
Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
22 Efodun altına giyilen kaftanı ustaca dokunmuş salt lacivert iplikten yaptılar.
Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
23 Ortasında baş geçecek kadar bir boşluk bıraktılar. Yırtılmaması için boşluğun kenarlarını yaka gibi dokuyarak çevirdiler.
na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
24 Kaftanın kenarını lacivert, mor, kırmızı iplikle, özenle dokunmuş ince ketenden nar motifleriyle bezediler.
Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
25 Saf altından çıngıraklar yaptılar ve hizmet için kullanılan kaftanın eteğinin ucundaki narların arasına, bir çıngırak bir nar, bir çıngırak bir nar olmak üzere çepeçevre koydular. Tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi yaptılar.
Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
27 Harun'la oğulları için ince ketenden ustaca dokunmuş mintanlar, sarıklar, süslü başlıklar, ince keten donlar, lacivert, mor, kırmızı iplikle, özenle dokunmuş ince ketenden nakışlı kuşak yaptılar; tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi.
Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
30 Kutsal tacın levhasını saf altından yaparak üzerine mühür oyar gibi ‘RAB'be adanmıştır’ sözünü yazdılar.
Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
31 Üstüne bağlanmak üzere sarığa lacivert bir kordon taktılar; tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi.
Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Böylece konutun, yani Buluşma Çadırı'nın bütün işleri tamamlandı. İsrailliler her şeyi tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi yaptılar.
Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
33 Konutu, çadırla bütün takımlarını, kopçalarını, çerçevelerini, kirişlerini, direklerini, tabanlarını; kırmızı boyalı koç derisinden örtüyü, deri örtüyü, bölme perdesini; Levha Sandığı'yla sırıklarını, Bağışlanma Kapağı'nı; masayla takımlarını, Tanrı'nın huzuruna konan ekmekleri; saf altın kandilliği, üstüne dizilecek kandillerle takımlarını, kandil için zeytinyağını; altın sunağı, mesh yağını, güzel kokulu buhuru, çadırın giriş bölümünün perdesini; tunç sunakla ızgarasını, sırıklarını, bütün takımlarını, kazanı, kazan ayaklığını; avlunun perdelerini, direklerini, direk tabanlarını, avlu girişinin perdesini, iplerini, kazıklarını, konutta, yani Buluşma Çadırı'ndaki hizmet için gerekli bütün aletleri; kutsal yerdeki hizmet için dokunmuş giysileri, Kâhin Harun'un kutsal giysilerini, oğullarının kâhin giysilerini Musa'ya gösterdiler.
Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
42 Her şeyi tıpkı RAB'bin Musa'ya buyurduğu gibi yaptılar.
Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
43 Musa baktı, bütün işlerin RAB'bin buyurduğu gibi yapılmış olduğunu görünce onları kutsadı.
Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

< Misir'Dan Çikiş 39 >