< Misir'Dan Çikiş 35 >

1 Musa bütün İsrail topluluğunu çağırarak, “RAB'bin yapmanızı buyurduğu işler şunlardır” dedi,
Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
2 “Altı gün çalışacaksınız. Ama yedinci gün sizin için kutsal Şabat, RAB'be adanmış dinlenme günü olacaktır. O gün çalışan herkes öldürülecektir.
Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
3 Şabat Günü konutlarınızda ateş yakmayacaksınız.”
Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
4 Musa bütün İsrail topluluğuna seslenerek şöyle dedi: “RAB'bin buyruğu şudur:
Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
5 Aranızda armağanlar toplayıp RAB'be sunacaksınız. İstekli olan herkes RAB'be altın, gümüş, tunç; lacivert, mor, kırmızı iplik; ince keten, keçi kılı, deri, kırmızı boyalı koç derisi, akasya ağacı armağan etsin.
Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
6
nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
7
ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
8 Kandil için zeytinyağı; mesh yağı ve güzel kokulu buhur için baharat;
mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
9 başkâhinin efoduyla göğüslüğü için oniks ve öbür kakma taşları getirsin.
vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
10 “Aranızdaki bütün becerikli kişiler gelip RAB'bin buyurduğu her şeyi yapsın.
“Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
11 Konutu, çadırın iç ve dış örtüsünü, kopçalarını, çerçevelerini, kirişlerini, direklerini, tabanlarını;
Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
12 sandığı ve sırıklarını, Bağışlanma Kapağı'nı, bölme perdesini,
Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
13 masayla sırıklarını, bütün masa takımlarını, huzura konan ekmekleri;
meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
14 ışık için kandilliği ve takımlarını, kandilleri, kandiller için zeytinyağını;
kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
15 buhur sunağını ve sırıklarını, mesh yağını, güzel kokulu buhuru; konutun giriş bölümündeki perdeyi;
madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
16 yakmalık sunu sunağını ve tunç ızgarasını, sırıklarını, bütün takımlarını, kazanı ve kazan ayaklığını;
madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
17 avlunun çevresindeki perdeleri, direkleri, direk tabanlarını, avlu kapısındaki perdeyi,
pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
18 konutun ve avlunun kazıklarıyla iplerini;
vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
19 kutsal yerde hizmet etmek için dokunmuş giysileri –Kâhin Harun'un giysileriyle oğullarının kâhin giysilerini– yapsınlar.”
mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
20 İsrail topluluğu Musa'nın yanından ayrıldı.
Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
21 Her istekli, hevesli kişi Buluşma Çadırı'nın yapımı, hizmeti ve kutsal giysiler için RAB'be armağan getirdi.
na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
22 Kadın erkek herkes istekle geldi, RAB'be her çeşit altın takı, broş, küpe, yüzük, kolye getirdi. RAB'be armağan ettikleri bütün takılar altındı.
Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
23 Ayrıca kimde lacivert, mor, kırmızı iplik; ince keten, keçi kılı, deri, kırmızı boyalı koç derisi varsa getirdi.
Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
24 Gümüş ve tunç armağanlar sunan herkes onları RAB'be adadı. Herhangi bir işte kullanılmak üzere kimde akasya ağacı varsa getirdi.
Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
25 Bütün becerikli kadınlar elleriyle eğirdikleri lacivert, mor, kırmızı ipliği, ince keteni getirdiler.
Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
26 İstekli, becerikli kadınlar da keçi kılı eğirdiler.
Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
27 Önderler efod ve göğüslük için oniks, kakma taşlar,
Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
28 kandil, mesh yağı ve güzel kokulu buhur için baharat ve zeytinyağı getirdiler.
Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
29 Kadın erkek bütün istekli İsrailliler RAB'bin Musa aracılığıyla yapmalarını buyurduğu işler için RAB'be gönülden verilen sunu sundular.
Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
30 Musa İsrailliler'e, “Bakın!” dedi, “RAB Yahuda oymağından özellikle Hur oğlu Uri oğlu Besalel'i seçti.
Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
31 Beceri, anlayış, bilgi ve her türlü ustalık vermek için onu kendi Ruhu'yla doldurdu.
naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
32 Öyle ki, altın, gümüş, tunç işleyerek ustaca yapıtlar üretsin;
ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
33 taş kesme ve kakmada, ağaç oymacılığında, her türlü sanat dalında çalışsın.
kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
34 RAB ona ve Dan oymağından Ahisamak oğlu Oholiav'a öğretme yeteneği de verdi.
Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
35 Onlara üstün beceri verdi. Öyle ki, ustalık isteyen her türlü işte, oymacılıkta, lacivert, mor, kırmızı iplik ve ince keten yapmada, dokuma ve nakış işlerinde, her sanat dalında yaratıcı olsunlar.
Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.

< Misir'Dan Çikiş 35 >