< 2 Samuel 24 >

1 RAB İsrail halkına yine öfkelendi. Davut'u onlara karşı kışkırtarak, “Git, İsrail ve Yahuda halkını say” dedi.
Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
2 Kral, yanında bulunan ordu komutanı Yoav'a şu buyruğu verdi: “Dan'dan Beer-Şeva'ya dek İsrail'in bütün oymaklarına gidip halkı sayın ki, halkın sayısını bileyim.”
Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
3 Ama Yoav, “RAB Tanrın halkını yüz kat daha çoğaltsın, efendim kralım da bunu görsün!” diye karşılık verdi, “Ancak, efendim kralım neden bunu istiyor?”
Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
4 Gelgelelim kralın sözü Yoav'la birlik komutanlarının sözünden baskın çıktı. Böylece kralın yanından ayrılıp İsrail'de sayım yapmaya gittiler.
Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
5 Şeria Irmağı'ndan geçerek Aroer yakınında, vadinin ortasındaki kentin güneyinde konakladılar. Oradan Gat'ı, Yazer'i, Gilat'ı, Tahtim-Hodşi topraklarını, Dan-Yaan'ı geçip Sayda'ya vardılar.
Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
6
Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
7 Sonra Sur Kalesi'ne, Hivliler'le Kenanlılar'ın bütün kentlerine uğradılar. Sonunda Yahuda ülkesinin Negev bölgesindeki Beer-Şeva'ya ulaştılar.
Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
8 Dokuz ay yirmi gün ülkeyi baştan başa dolaştıktan sonra Yeruşalim'e döndüler.
Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
9 Yoav sayımın sonucunu krala bildirdi: İsrail'de kılıç kuşanabilen sekiz yüz bin, Yahuda'daysa beş yüz bin kişi vardı.
Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
10 Davut sayım yaptıktan sonra kendisini suçlu buldu ve RAB'be, “Bunu yapmakla büyük günah işledim!” dedi, “Ya RAB, lütfen kulunun suçunu bağışla. Çünkü çok akılsızca davrandım.”
Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
11 Ertesi sabah Davut uyandığında, RAB Davut'un bilicisi Peygamber Gad'a şöyle dedi: “Gidip Davut'a de ki, ‘RAB şöyle diyor: Önüne üç seçenek koyuyorum. Bunlardan birini seç de sana onu yapayım.’”
Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
“Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
13 Gad Davut'a gidip durumu anlattı ve şöyle dedi: “Ülkende yedi yıl kıtlık mı olsun? Yoksa seni kovalayan düşmanlarının önünden üç ay kaçmak mı istersin? Ya da ülkende üç gün salgın hastalık mı olsun? Beni gönderene ne yanıt vereyim, şimdi iyice düşün.”
Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
14 Davut, “Sıkıntım büyük” diye yanıtladı, “İnsan eline düşmektense, RAB'bin eline düşelim. Çünkü O'nun acıması büyüktür.”
Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
15 Bunun üzerine RAB o sabahtan belirlenen zamana dek İsrail ülkesine salgın hastalık gönderdi. Dan'dan Beer-Şeva'ya dek halktan yetmiş bin kişi öldü.
Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
16 Melek Yeruşalim'i yok etmek için elini uzatınca, RAB göndereceği yıkımdan vazgeçti. Halkı yok eden meleğe, “Yeter artık! Elini çek” dedi. RAB'bin meleği Yevuslu Aravna'nın harman yerinde duruyordu.
Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
17 Davut, halkı öldüren meleği görünce, RAB'be, “Günah işleyen benim, ben suç işledim” dedi, “Bu koyunlar ne yaptı ki? Ne olur beni ve babamın soyunu cezalandır.”
Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
18 O gün Gad Davut'a gitti. Ona, “Gidip Yevuslu Aravna'nın harman yerinde RAB'be bir sunak kur” dedi.
Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
19 Davut Gad'ın sözü uyarınca RAB'bin buyurduğu gibi gitti.
Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
20 Aravna bakınca kralla görevlilerinin kendisine doğru yaklaştıklarını gördü. Varıp kralın önünde yüzüstü yere kapandı.
Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
21 Sonra, “Efendim kral niçin kulunun yanına geldi?” diye sordu. Davut, “RAB'be bir sunak kurmak üzere harman yerini senden satın almak için” diye yanıtladı, “Öyle ki, salgın hastalık halkın üzerinden kalksın.”
Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
22 Aravna, “Efendim kral uygun gördüğünü alıp RAB'be sunsun” dedi, “İşte yakmalık sunu için öküzler ve odun için düvenlerle öküzlerin takımları!
Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
23 Ey kral, Aravna bütün bunları sana veriyor.” Sonra ekledi: “RAB Tanrın senden hoşnut olsun!”
Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
24 Ne var ki kral, “Olmaz!” dedi, “Senden malını kesinlikle bir ücret karşılığında satın alacağım. Çünkü Tanrım RAB'be karşılığını ödemeden yakmalık sunular sunmam.” Böylece Davut harman yerini ve öküzleri elli şekel gümüş karşılığında satın aldı.
Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
25 Davut orada RAB'be bir sunak kurup yakmalık sunuları ve esenlik sunularını sundu. RAB de ülkeyle ilgili yakarıyı yanıtladı ve salgın hastalık İsrail'den kaldırıldı.
Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.

< 2 Samuel 24 >