< 2 Samuel 23 >

1 Davut'un son sözleri şunlardır: “İşay oğlu Davut, Tanrı'nın yükselttiği adam, Yakup'un Tanrısı'nın meshettiği, İsrail'in sevilen ezgi okuyucusu şöyle diyor:
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
2 RAB'bin Ruhu benim aracılığımla konuşuyor, Sözü dilimin ucundadır.
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 İsrail'in Tanrısı konuştu, İsrail'in kayası bana dedi ki, ‘İnsanları doğrulukla Ve Tanrı korkusuyla yöneten kişi,
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
4 Bulutsuz bir sabah, Şafakta görünen gün ışığı gibidir, Parlaklığı yağmurdan sonra topraktan ot bitirir.’
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
5 Soyum da Tanrı'yla böyle değil mi? O benimle sonsuza dek kalıcı, Her yönüyle düzenli ve güvenilir bir antlaşma yaptı. Kesin kurtuluşa ve her dileğime kavuşmamı O sağlamayacak mı?
“Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
6 Kötülere gelince, Elle tutulamayan dikenler gibi Tümü bir yana atılacak.
Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
7 Dikenlere dokunan kişi, Demir bir araçla Ya da mızrağın sapıyla dokunur. Dikenler oldukları yerde bütünüyle yakılacak.”
Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
8 Davut'un yiğit askerlerinin adları şunlardır: Esnili Adino diye de bilinen üç kişinin önderi Tahkemonlu Yoşeb-Başşevet bir saldırıda sekiz yüz kişiyi öldürdü.
Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
9 İkincisi, Ahohlu Dodo oğlu Elazar. Pas-Dammim'de savaşmak için toplanan Filistliler'e meydan okuyan Davut'un yanındaki üç yiğitten biriydi. İsrailliler o sırada geri çekilmişlerdi.
Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
10 Ama Elazar yerinde durdu; eli yorulup kılıca yapışıncaya dek Filistliler'i öldürdü. O gün RAB büyük bir zafer sağladı. İsrailliler yalnız yere serilenleri yağmalamak üzere Elazar'a döndüler.
lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
11 Üçüncüsü, Hararlı Age oğlu Şamma'ydı. Filistliler Lahay'daki bir mercimek tarlasının yanında toplandıklarında, İsrailli askerler onların önünden kaçmıştı.
Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
12 Ama Şamma tarlanın ortasında durup orayı savunmuş, Filistliler'i öldürmüştü. RAB büyük bir zafer sağlamıştı.
Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
13 Biçme zamanı Otuzlar'dan üçü Davut'un yanına, Adullam Mağarası'na gittiler. Bir Filist birliği Refaim Vadisi'nde ordugah kurmuştu.
Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
14 Bu sırada Davut hisarda, ikinci Filist birliğiyse Beytlehem'deydi.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
15 Davut özlemle, “Keşke biri Beytlehem'de kapının yanındaki kuyudan bana su getirse!” dedi.
Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
16 Bu Üçler Filist ordugahının ortasından geçerek Beytlehem'de kapının yanındaki kuyudan su çekip Davut'a getirdiler. Ama Davut içmek istemedi; suyu yere dökerek RAB'be sundu.
Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
17 “Ya RAB, bunu yapmak benden uzak olsun!” dedi, “Canlarını tehlikeye atıp giden bu üç kişinin kanını mı içeyim?” Bu yüzden suyu içmek istemedi. Bu üç kişinin yiğitliği işte böyleydi.
Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
18 Yoav'ın kardeşi, Seruya oğlu Avişay Üçler'in önderiydi. Mızrağını kaldırıp üç yüz kişiyi öldürdü. Bu yüzden Üçler kadar ünlendi.
Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
19 Üçler'in en saygın kişisiydi ve onların önderi oldu. Ama Üçler'den sayılmadı.
Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
20 Yehoyada oğlu Kavseelli Benaya yürekli bir savaşçıydı. Büyük işler başardı. Aslan yürekli iki Moavlı'yı öldürdü. Ayrıca karlı bir gün çukura inip bir aslan öldürdü.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
21 İri yarı bir Mısırlı'yı da öldürdü. Mısırlı'nın elinde mızrak vardı. Benaya sopayla onun üzerine yürüdü. Mızrağı elinden kaptığı gibi onu kendi mızrağıyla öldürdü.
Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
22 Yehoyada oğlu Benaya'nın yaptıkları bunlardır. Bu sayede o da üç yiğitler kadar ünlendi.
Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
23 Benaya Otuzlar arasında saygın bir yer edindiyse de, Üçler'den sayılmadı. Davut onu muhafız birliği komutanlığına atadı.
Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
24 Otuzlar'ın arasında sayılan ötekiler şunlardır: Yoav'ın kardeşi Asahel, Beytlehemli Dodo oğlu Elhanan,
Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
25 İkisi de Harotlu olan Şamma ve Elika,
Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
26 Paletli Heles, Tekoalı İkkeş oğlu İra,
Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
27 Anatotlu Aviezer, Huşalı Mevunnay,
Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
28 Ahohlu Salmon, Netofalı Mahray,
Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
29 Netofalı Baana oğlu Helev, Benyaminoğulları'ndan Givalı Rivay oğlu İttay,
Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
30 Piratonlu Benaya, Gaaş vadilerinden Hidday,
Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
31 Arvalı Avialvon, Barhumlu Azmavet,
Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
32 Şaalbonlu Elyahba, Yaşan'ın oğulları ve Yonatan,
Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
33 Hararlı Şamma, Hararlı Şarar oğlu Ahiam,
mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
34 Maakalı Ahasbay oğlu Elifelet, Gilolu Ahitofel oğlu Eliam,
Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
35 Karmelli Hesray, Aravlı Paaray,
Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
36 Sovalı Natan oğlu Yigal, Gatlı Bani,
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
37 Ammonlu Selek, Seruya oğlu Yoav'ın silah taşıyıcısı Beerotlu Nahray,
Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
38 Yattirli İra ve Garev,
Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
39 Hititli Uriya. Tümü otuz yedi kişiydi.
na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.

< 2 Samuel 23 >