< 1 Samuel 23 >

1 Davut'a, “Filistliler Keila Kenti'ne saldırıp harmanları yağmalıyorlar” diye haber verdiler.
Daudi alipoambiwa kuwa, “Tazama, Wafilisti wanapigana dhidi ya Keila nao wanapokonya nafaka katika sakafu za kupuria,”
2 Davut RAB'be, “Gidip şu Filistliler'e saldırayım mı?” diye danıştı. RAB, “Git, Filistliler'e saldır ve Keila Kenti'ni kurtar” diye yanıtladı.
akauliza kwa Bwana, akisema, “Je, niende na kuwashambulia hawa Wafilisti?” Bwana akamjibu, “Nenda, washambulie Wafilisti na uuokoe Keila.”
3 Ama adamları Davut'a, “Bak, biz burada Yahuda'dayken korkuyoruz” dediler, “Keila'ya Filist ordusuna karşı savaşmaya gidersek büsbütün korkarız.”
Lakini watu wa Daudi wakamwambia, “Hapa Yuda kwenyewe tunaogopa. Si zaidi sana, kama tukienda Keila dhidi ya majeshi ya Wafilisti!”
4 Bunun üzerine Davut RAB'be bir kez daha danıştı. RAB ona yine, “Kalk, Keila'ya git! Çünkü Filistliler'i senin eline ben teslim edeceğim” dedi.
Daudi akauliza kwa Bwana tena, naye Bwana akamjibu akamwambia, “Shuka uende Keila, kwa kuwa nitawatia Wafilisti mkononi mwako.”
5 Böylece Davut'la adamları Keila'ya gidip Filistliler'e karşı savaştılar. Davut onların hayvanlarını ele geçirdi. Filistliler'i ağır bir yenilgiye uğratarak Keila halkını kurtardı.
Basi Daudi na watu wake wakaenda Keila, wakapigana na Wafilisti na kutwaa wanyama wao wa kutosha. Daudi akawatia hasara kubwa Wafilisti na kuwaokoa watu wa Keila.
6 Ahimelek'in oğlu Aviyatar kaçıp Keila'da bulunan Davut'a gittiğinde, efodu da birlikte götürmüştü.
(Basi Abiathari mwana wa Ahimeleki alikuwa ameleta kisibau alipokimbilia kwa Daudi huko Keila.)
7 Saul, Davut'un Keila Kenti'ne gittiğini duyunca, “Tanrı Davut'u elime teslim etti” dedi, “Davut sürgülü kapıları olan bir kente girmekle kendini hapsetmiş oldu.”
Sauli akaambiwa kwamba Daudi alikuwa amekwenda Keila, naye akasema, “Mungu amemtia mkononi mwangu, kwa kuwa Daudi amejifunga mwenyewe kwa kuingia kwenye mji wenye malango na makomeo.”
8 Böylece Saul, Keila'ya yürüyüp Davut'la adamlarını kuşatmak amacıyla bütün halkı savaşa çağırdı.
Naye Sauli akayaita majeshi yake yote yaende vitani, kuishukia Keila ili kumzingira Daudi na watu wake kwa jeshi.
9 Davut, Saul'un kendisine bir düzen kurduğunu duyunca, Kâhin Aviyatar'a, “Efodu getir” dedi.
Daudi alipojua kuwa Sauli alikuwa ana hila dhidi yake, akamwambia Abiathari kuhani, “Leta kile kisibau.”
10 Sonra şöyle yakardı: “Ey İsrail'in Tanrısı RAB! Ben kulun yüzünden Saul'un gelip Keila'yı yıkmayı tasarladığına dair kesin haber aldım.
Daudi akasema, “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mtumishi wako amesikia kwa hakika kwamba Sauli anapanga kuja Keila na kuangamiza mji kwa ajili yangu.
11 Keila halkı beni onun eline teslim eder mi? Kulunun duymuş olduğu gibi Saul gelecek mi? Ey İsrail'in Tanrısı RAB, yalvarırım, kuluna bildir!” RAB, “Saul gelecek” yanıtını verdi.
Je, watu wa Keila watanisalimisha kwake? Je, Sauli atateremka, kama mtumishi wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mwambie mtumishi wako.” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, atashuka.”
12 Davut RAB'be, “Keila halkı beni ve adamlarımı Saul'un eline teslim edecek mi?” diye sordu. RAB, “Teslim edecek” dedi.
Daudi akauliza tena, “Je watu wa Keila watanisalimisha mimi pamoja na watu wangu kwa Sauli?” Naye Bwana akasema, “Ndiyo, watafanya hivyo.”
13 Bunun üzerine Davut ile yanındaki altı yüz kadar kişi Keila'dan ayrılıp oradan oraya yer değiştirmeye başladılar. Davut'un Keila'dan kaçtığını öğrenen Saul oraya gitmekten vazgeçti.
Basi Daudi na watu wake, wapatao 600, wakaondoka Keila wakawa wanakwenda sehemu moja hadi nyingine. Sauli alipoambiwa Daudi ametoroka kutoka Keila, hakwenda huko.
14 Davut kırsal bölgedeki sığınaklarda ve Zif Çölü'nün dağlık kesiminde kaldı. Saul her gün Davut'u aradığı halde, Tanrı onu Saul'un eline teslim etmedi.
Daudi akakaa katika ngome za jangwani na katika vilima vya Jangwa la Zifu. Siku baada ya siku Sauli aliendelea kumsaka, lakini Mungu hakumtia Daudi mikononi mwake.
15 Davut Zif Çölü'nde, Horeş'teyken, Saul'un kendisini öldürmek için yola çıktığını öğrendi.
Daudi alipokuwa huko Horeshi katika Jangwa la Zifu, akajua kuwa Sauli alikuwa amekuja ili amuue.
16 Bu arada Saul oğlu Yonatan kalkıp Horeş'e, Davut'un yanına gitti ve onu Tanrı'nın adıyla yüreklendirdi.
Naye Yonathani mwana wa Sauli akamwendea Daudi huko Horeshi na kumtia moyo kusimama imara katika imani yake kwa Mungu.
17 “Korkma!” dedi, “Babam Saul sana dokunmayacak. Sen İsrail Kralı olacaksın, ben de senin yardımcın olacağım. Babam Saul da bunu biliyor.”
Akamwambia, “Usiogope, Daudi; baba yangu Sauli hatakutia mkononi mwake. Utakuwa mfalme juu ya Israeli, nami nitakuwa wa pili wako. Hata baba yangu Sauli anajua hili.”
18 İkisi de RAB'bin önünde aralarındaki antlaşmayı yenilediler. Sonra Yonatan evine döndü, Davut ise Horeş'te kaldı.
Wote wawili wakaweka agano mbele za Bwana. Kisha Yonathani akaenda zake nyumbani, lakini Daudi akabaki Horeshi.
19 Zifliler Giva'ya gidip Saul'a, “Davut aramızda” dediler, “Yeşimon'un güneyinde, Hakila Tepesi'ndeki Horeş sığınaklarında gizleniyor.
Basi Wazifu wakakwea kwa Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu katika ngome huko Horeshi, katika kilima cha Hakila, kusini mwa Yeshimoni?
20 Ey kral, ne zaman gelmek istersen gel! Davut'u kralın eline teslim etmeyi ise bize bırak.”
Sasa, ee mfalme, uteremke wakati wowote unapoona vyema kufanya hivyo, sisi tutawajibika kumkabidhi kwa mfalme.”
21 Saul, “RAB sizi kutsasın! Bana acıdınız” dedi,
Sauli akajibu, “Bwana awabariki kwa kunifikiria.
22 “Gidin ve bir daha araştırın; Davut'un genellikle nerelerde gizlendiğini, orada onu kimin gördüğünü iyice öğrenin. Çünkü onun çok kurnaz olduğunu söylüyorlar.
Nendeni mkafanye maandalizi zaidi. Mkajue mahali ambapo Daudi huenda mara kwa mara na nani amepata kumwona huko. Wananiambia yeye ni mwerevu sana.
23 Gizlendiği yerlerin hepsini öğrenip bana kesin bir haber getirin. O zaman ben de sizinle gelirim. Eğer Davut o bölgedeyse, bütün Yahuda boyları içinde onu arayıp bulacağım.”
Jueni kila mahali anapojificha mrudi na kunipa taarifa kamili. Kisha nitakwenda pamoja nanyi; kama atakuwa katika eneo hilo, nitamsaka miongoni mwa koo zote za Yuda.”
24 Böylece Zifliler kalkıp Saul'dan önce Zif'e gittiler. O sırada Davut'la adamları Yeşimon'un güneyindeki Arava'da, Maon Çölü'ndeydiler.
Basi wakaondoka na kwenda mpaka Zifu wakimtangulia Sauli. Naye Daudi na watu wake walikuwa katika Jangwa la Maoni, katika Araba kusini mwa Yeshimoni.
25 Saul ile adamlarının kendisini aramaya geldiklerini öğrenince Davut aşağıya inip Maon Çölü'ndeki kayalığa sığındı. Saul bunu duyunca Davut'un ardından Maon Çölü'ne gitti.
Sauli na watu wake wakaanza msako, naye Daudi alipoelezwa hili, akateremka mpaka mwambani na kukaa katika Jangwa la Maoni. Sauli aliposikia hili, akaenda katika Jangwa la Maoni akimfuata Daudi.
26 Saul dağın bir yanından, Davut'la adamları ise öbür yanından ilerliyordu. Davut Saul'dan kaçıp kurtulmaya çalışıyordu. Saul'la askerleri Davut'la adamlarını yakalamak üzere yaklaşırken,
Sauli alikuwa akienda upande mmoja wa mlima, naye Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mlima, wakiharakisha kumkimbia Sauli. Wakati Sauli na majeshi yake walipokaribia kumkamata Daudi na watu wake,
27 bir ulak gelip Saul'a şöyle dedi: “Çabuk gel! Filistliler ülkeye saldırıyor.”
mjumbe alikuja kwa Sauli, akisema, “Njoo haraka! Wafilisti wanaishambulia nchi.”
28 Bunun üzerine Saul Davut'u kovalamayı bırakıp Filistliler'le savaşmaya gitti. Bu yüzden oraya Sela-Hammahlekot adı verildi.
Ndipo Sauli akarudi akaacha kumfuata Daudi na kwenda kukabiliana na Wafilisti. Ndiyo sababu wanaiita sehemu hii Sela-Hamalekothi.
29 Davut oradan ayrılıp Eyn-Gedi bölgesindeki sığınaklara gizlendi.
Naye Daudi akakwea kutoka huko na kuishi katika ngome za En-Gedi.

< 1 Samuel 23 >