< 1 Samuel 21 >

1 Davut Nov Kenti'ne, Kâhin Ahimelek'in yanına gitti. Ahimelek titreyerek Davut'u karşılamaya çıktı. “Neden yalnızsın? Neden yanında kimse yok?” diye sordu.
Daudi akaenda Nobu, kwa Ahimeleki kuhani. Ahimeleki akatetemeka alipokutana naye, akamuuliza, “Kwa nini uko peke yako? Kwa nini hukufuatana na mtu yeyote?”
2 Davut şöyle yanıtladı: “Kral bana bir görev verdi. ‘Sana verdiğim görevden ve buyruklardan kimsenin haberi olmasın’ dedi. Adamlarıma gelince, belli bir yere gitmelerini söyledim.
Daudi akamjibu Ahimeleki kuhani, akisema, “Mfalme ameniagiza shughuli fulani na kuniambia, ‘Mtu yeyote asijue chochote kuhusu kazi yako wala maagizo yako!’ Kuhusu watu wangu, nimewaambia tukutane mahali fulani.
3 Şu an elinde ne var? Bana beş somun ekmek ya da başka ne varsa ver.”
Sasa basi, una nini mkononi? Nipatie mikate mitano au chochote unachoweza kupata.”
4 Kâhin, “Taze ekmeğim yok” diye karşılık verdi, “Ama adamların kadından uzak kaldılarsa kutsanmış ekmek var.”
Lakini kuhani akamjibu Daudi, “Sina mkate wowote wa kawaida kwa sasa. Hata hivyo, ipo hapa mikate iliyowekwa wakfu, iwapo watu wamejitenga na wanawake.”
5 Davut, “Yola çıktığımızdan her zaman olduğu gibi, kadından uzak kaldık” dedi, “Sıradan bir yolculuğa çıktığımızda bile adamlarım kendilerini temiz tutarlar; özellikle bugün ne kadar daha çok temiz olacaklar.”
Daudi akajibu, “Hakika tumejitenga na wanawake kwa siku hizi chache kama kawaida ya ninapotoka kwenda kwenye shughuli. Navyo vyombo vya wale vijana huwa ni vitakatifu hata kwenye safari ya kawaida, si zaidi sana leo vyombo vyao vitakuwa ni vitakatifu?”
6 Bunun üzerine kâhin ona kutsanmış ekmek verdi; çünkü orada huzura konan ekmekten başka ekmek yoktu. Bu ekmek RAB'bin huzurundan alındığı gün yerine sıcak ekmek konurdu.
Hivyo kuhani akampa ile mikate iliyowekwa wakfu, kwa kuwa hapakuwepo mikate mingine isipokuwa hiyo ya Wonyesho iliyokuwa imeondolewa hapo mbele za Bwana na kubadilishwa na mingine yenye moto siku ile ilipoondolewa.
7 O gün Saul'un görevlilerinden Edomlu Doek adındaki baş çoban RAB'bin önünde dinsel görevini yerine getirmek üzere orada bulunuyordu.
Basi siku hiyo palikuwepo na mmoja wa watumishi wa Sauli, aliyezuiliwa mbele za Bwana; alikuwa Doegi Mwedomu, kiongozi wa wachunga wanyama wa Sauli.
8 Davut Ahimelek'e, “Yanında mızrak ya da kılıç yok mu?” diye sordu, “Kralın işi acele olduğundan, yanıma ne kılıcımı aldım, ne de başka bir silah.”
Daudi akamuuliza Ahimeleki, “Je, unao mkuki au upanga hapa? Sikuleta upanga wala silaha nyingine yoyote, kwa sababu shughuli ya mfalme ilikuwa ya haraka.”
9 Kâhin, “Ela Vadisi'nde öldürdüğün Filistli Golyat'ın kılıcı var” diye karşılık verdi, “Efodun arkasında beze sarılı duruyor. Burada başka silah yok. İstersen onu alabilirsin.” Davut, “Onun gibisi yoktur, onu bana ver” dedi.
Kuhani akajibu, “Upanga wa Goliathi Mfilisti, ambaye ulimuua katika Bonde la Ela, upo hapa, umefungiwa katika kitambaa nyuma ya kisibau. Kama unauhitaji, uchukue, hakuna upanga mwingine hapa ila huo tu.” Daudi akasema, “Hakuna upanga mwingine kama huo. Nipatie huo.”
10 Saul'dan kaçan Davut o gün Gat Kralı Akiş'e gitti.
Siku ile Daudi akamkimbia Sauli na kwenda kwa Akishi mfalme wa Gathi.
11 Akiş'in görevlileri, “Bu İsrail Kralı Davut değil mi?” dediler, “Çalıp oynarken, ‘Saul binlercesini öldürdü, Davut'sa on binlercesini’ diye hakkında ezgiler okudukları kişi bu değil mi?”
Lakini watumishi wa Akishi wakamwambia, “Je, huyu si ndiye Daudi mfalme wa nchi? Je, huyu si ndiye yule ambaye wanaimba katika ngoma zao wakisema: “‘Sauli amewaua elfu zake, naye Daudi makumi elfu yake’?”
12 Bu sözler Davut'u derin derin düşündürdü. Gat Kralı Akiş'ten çok korkan Davut, onların önünde tutumunu değiştirerek deli gibi davrandı. Kentin kapılarını tırmaladı, salyasını sakalına akıttı.
Daudi akayaweka maneno haya moyoni naye akamwogopa sana Akishi mfalme wa Gathi.
Basi akajifanya mwendawazimu mbele yao; naye alipokuwa mikononi mwao, alitenda kama kichaa, akikwaruza kwa kutia alama juu ya milango ya lango na kuachia udelele kutiririka kwenye ndevu zake.
14 Akiş görevlilerine, “Şu adama bakın!” dedi, “Delinin biri! Onu neden bana getirdiniz?
Akishi akawaambia watumishi wake, “Tazameni mtu huyu! Ana wazimu! Kwa nini mnamleta kwangu?
15 Bizde deliler eksik mi ki, önümde delilik yapsın diye bu adamı getirdiniz? Bu adamın sarayıma girmesi şart mı?”
Je, mimi nimepungukiwa na wenda wazimu kiasi kwamba mmeniletea mtu huyo hapa aendelee kufanya hivi mbele yangu? Je, ilikuwa ni lazima mtu huyo aje nyumbani kwangu?”

< 1 Samuel 21 >