< 1 Samuel 2 >

1 Hanna şöyle dua etti: “Yüreğim RAB'de bulduğum sevinçle coşuyor; Gücümü yükselten RAB'dir. Düşmanlarımın karşısında övünüyor, Kurtarışınla seviniyorum!
Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 Kutsallıkta RAB'bin benzeri yok, Evet, senin gibisi yok, ya RAB! Tanrımız gibi dayanak yok.
“Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
3 Artık büyük konuşmayın, Ağzınızdan küstahça sözler çıkmasın. Çünkü RAB her şeyi bilen Tanrı'dır; O'dur davranışları tartan.
“Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
4 Güçlülerin yayları kırılır; Güçsüzlerse güçle donatılır.
“Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
5 Toklar yiyecek uğruna gündelikçi olur, Açlar doyurulur. Kısır kadın yedi çocuk doğururken, Çok çocuklu kadın kimsesiz kalır.
Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
6 RAB öldürür de diriltir de, Ölüler diyarına indirir ve çıkarır. (Sheol h7585)
“Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
7 O kimini yoksul, kimini varsıl kılar; Kimini alçaltır, kimini yükseltir.
Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
8 Düşkünü yerden kaldırır, Yoksulu çöplükten çıkarır; Soylularla oturtsun Ve kendilerine onur tahtını miras olarak bağışlasın diye. Çünkü yeryüzünün temelleri RAB'bindir, O dünyayı onların üzerine kurmuştur.
Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
9 RAB sadık kullarının adımlarını korur, Ama kötüler karanlıkta susturulur. Çünkü güçle zafere ulaşamaz insan.
Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
10 RAB'be karşı gelenler paramparça olacak, RAB onlara karşı gökleri gürletecek, Bütün dünyayı yargılayacak, Kralını güçle donatacak, Meshettiği kralın gücünü yükseltecek.”
wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
11 Sonra Elkana Rama'ya, evine döndü. Küçük Samuel ise Kâhin Eli'nin gözetiminde RAB'bin hizmetinde kaldı.
Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
12 Eli'nin oğulları değersiz kişilerdi. RAB'bi ve kâhinlerin halkla ilgili kurallarını önemsemiyorlardı. Biri sunduğu kurbanın etini haşlarken, kâhinin hizmetkârı elinde üç dişli büyük bir çatalla gelir,
Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
14 çatalı kap, tencere, tava ya da kazana daldırırdı. Çatalla çıkarılan her şey kâhin için ayırılırdı. Şilo'ya gelen İsrailliler'in hepsine böyle davranırlardı.
Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
15 Üstelik kurbanın yağları yakılmadan önce, kâhinin hizmetkârı gelip kurban sunan adama, “Kâhine kızartmalık et ver. Senden haşlanmış et değil, çiğ et alacak” derdi.
Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
16 Kurban sunan, “Önce hayvanın yağları yakılmalı, sonra dilediğin kadar al” diyecek olsa, hizmetkâr, “Hayır, şimdi vereceksin, yoksa zorla alırım” diye karşılık verirdi.
Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
17 Gençlerin RAB'be karşı işledikleri günah çok büyüktü; çünkü RAB'be sunulan sunuları küçümsüyorlardı.
Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
18 Bu arada genç Samuel, keten efod giymiş, RAB'bin önünde hizmet ediyordu.
Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
19 Yıllık kurbanı sunmak için annesi her yıl kocasıyla birlikte oraya gider, diktiği cüppeyi oğluna getirirdi.
Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
20 Kâhin Eli de, Elkana ile karısına iyi dilekte bulunarak, “Dilediği ve RAB'be adadığı çocuğun yerine RAB sana bu kadından başka çocuklar versin” derdi. Bundan sonra evlerine dönerlerdi.
Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
21 RAB'bin lütfuna eren Hanna gebe kalıp üç erkek, iki kız daha doğurdu. Küçük Samuel ise RAB'bin hizmetinde büyüdü.
Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
22 Eli artık çok yaşlanmıştı. Oğullarının İsrailliler'e bütün yaptıklarını, Buluşma Çadırı'nın girişinde görevli kadınlarla düşüp kalktıklarını duymuştu.
Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
23 Onlara, “Neden böyle şeyler yapıyorsunuz?” dedi, “Yaptığınız kötülükleri herkesten işitiyorum.
Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
24 Olmaz bu, oğullarım! RAB'bin halkı arasında yayıldığını duyduğum haber iyi değil.
Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
25 İnsan insana karşı günah işlerse, Tanrı onun için aracılık eder. Ama RAB'be karşı günah işleyeni kim savunacak?” Ne var ki, onlar babalarının sözünü dinlemediler. Çünkü RAB onları öldürmek istiyordu.
Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
26 Bu arada giderek büyüyen genç Samuel RAB'bin de halkın da beğenisini kazanmaktaydı.
Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
27 O sıralarda bir Tanrı adamı Eli'ye gelip şöyle dedi: “RAB diyor ki, ‘Atan ve soyu Mısır'da firavunun halkına kölelik ederken kendimi onlara açıkça göstermedim mi?
Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
28 Sunağıma çıkması, buhur yakıp önümde efod giymesi için bütün İsrail oymakları arasından yalnız atanı kendime kâhin seçtim. Üstelik İsrailliler'in yakılan bütün sunularını da atanın soyuna verdim.
Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
29 Öyleyse neden konutum için buyurduğum kurbanı ve sunuyu küçümsüyorsunuz? Halkım İsrail'in sunduğu bütün sunuların en iyi kısımlarıyla kendinizi semirterek neden oğullarını benden daha çok önemsiyorsun?’
Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
30 “Bu nedenle İsrail'in Tanrısı RAB şöyle diyor: ‘Gerçekten, ailen ve atanın soyu sonsuza dek bana hizmet edecekler demiştim.’ Ama şimdi RAB şöyle buyuruyor: ‘Bu benden uzak olsun! Beni onurlandıranı ben de onurlandırırım. Ama beni saymayan küçük düşürülecek.
“Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
31 Soyundan hiç kimsenin yaşlanacak kadar yaşamaması için senin ve atanın soyunun gücünü kıracağım günler yaklaşıyor.
Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
32 İsrail'e yapılacak bütün iyiliğe karşın, sen konutumda sıkıntı göreceksin. Artık soyundan hiç kimse yaşlanacak kadar yaşamayacak.
nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
33 Sunağımdan bütün soyunu yok edeceğim, yalnız bir kişiyi esirgeyeceğim. Gözleri ağlamaktan kör olacak, yüreği yanacak. Ama soyundan gelenlerin hepsi kılıçla ölecekler.
Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
34 İki oğlun Hofni ile Pinehas'ın başına gelecek olay senin için bir belirti olacak: İkisi de aynı gün ölecek.
“‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
35 İsteklerimi ve amaçlarımı yerine getirecek güvenilir bir kâhin çıkaracağım kendime. Onun soyunu sürdüreceğim; o da meshettiğim kişinin önünde sürekli hizmet edecek.
Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
36 Ailenden sağ kalan herkes bir parça gümüş ve bir somun ekmek için gelip ona boyun eğecek ve, Ne olur, karın tokluğuna beni herhangi bir kâhinlik görevine ata! diye yalvaracak.’”
Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”

< 1 Samuel 2 >