< 1 Krallar 3 >

1 Süleyman, Mısır Firavunu'nun kızıyla evlendi. Böylece firavunla müttefik oldu. Eşini Davut Kenti'ne götürdü. Kendi sarayı, RAB'bin Tapınağı ve Yeruşalim'in çevre surları tamamlanıncaya kadar orada yaşadılar.
Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu la Bwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu.
2 Halk, hâlâ çeşitli tapınma yerlerinde RAB'be kurban sunuyordu. Çünkü o güne dek RAB'bin adına yapılmış bir tapınak yoktu.
Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.
3 Süleyman babası Davut'un kurallarına uyarak RAB'be olan sevgisini gösterdi. Ancak hâlâ çeşitli tapınma yerlerinde kurban sunuyor, buhur yakıyordu.
Solomoni akaonyesha upendo wake kwa Bwana kwa kuenenda sawasawa na amri za Daudi baba yake, ila yeye alitoa dhabihu na kufukiza uvumba huko mahali pa juu.
4 Tapınma yerlerinin en ünlüsü Givon'daydı. Kral Süleyman oraya giderek sunakta bin yakmalık sunu sundu.
Mfalme akaenda Gibeoni kutoa dhabihu, kwa maana ndipo palipokuwa mahali pa juu pa kuabudia, naye Solomoni akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya hayo madhabahu.
5 RAB Tanrı, Givon'da o gece rüyada Süleyman'a görünüp, “Sana ne vermemi istersin?” diye sordu.
Bwana akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, “Omba lolote utakalo nikupe.”
6 Süleyman, “Kulun babam Davut'a büyük iyilikler yaptın” diye karşılık verdi, “O sana bağlı, doğru, bütün yüreğiyle dürüst biri olarak yolunda yürüdü. Bugün tahtına oturacak bir oğul vermekle ona büyük bir iyilik daha yapmış oldun.
Solomoni akajibu, “Umemfanyia mtumishi wako, baba yangu Daudi, fadhili nyingi, kwa kuwa alikuwa mwaminifu kwako na mwenye haki, tena mnyofu wa moyo. Nawe umemzidishia fadhili hii kuu kwani umempa mwana wa kuketi kwenye kiti chake cha ufalme, kama ilivyo leo.
7 “Ya RAB Tanrım! Ben henüz çocuk denecek bir yaşta, yöneticilik nedir bilmezken bu kulunu babam Davut'un yerine kral atadın.
“Sasa, Ee Bwana Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako mfalme badala ya baba yangu Daudi. Lakini mimi ni mtoto mdogo tu, wala sijui jinsi ya kutekeleza wajibu wangu.
8 İşte kulun kendi seçtiğin kalabalık halkın, sayılamayacak kadar büyük bir kalabalığın ortasındadır.
Mtumishi wako yuko hapa miongoni mwa watu uliowachagua: taifa kubwa, watu wengi wasioweza kuhesabika wala kutoa idadi yao.
9 Bu yüzden bana öyle sezgi dolu bir yürek ver ki, iyi ile kötüyü ayırt edip halkını yönetebileyim. Başka türlü senin bu büyük halkını kim yönetebilir!”
Hivyo mpe mtumishi wako moyo wa ufahamu ili kutawala watu wako na kupambanua kati ya mema na mabaya. Kwa maana, ni nani awezaye kutawala watu wako hawa walio wengi hivi?”
10 Süleyman'ın bu isteği Rab'bi hoşnut etti.
Bwana akapendezwa kwamba Solomoni ameliomba jambo hili.
11 Tanrı ona şöyle dedi: “Madem kendin için uzun ömür, zenginlik ve düşmanlarının ölümünü istemedin, bunların yerine adil bir yönetim için bilgelik istedin; isteğini yerine getireceğim. Sana öyle bir bilgelik ve sezgi dolu bir yürek vereceğim ki, benzeri ne senden öncekilerde görülmüştür, ne de senden sonrakilerde görülecektir.
Basi Mungu akamwambia, “Kwa kuwa umeomba neno hili na hukuomba maisha marefu au upate utajiri kwa nafsi yako, wala adui zako wafe, bali umeomba ufahamu katika kutoa haki,
nitafanya lile uliloomba. Nitakupa moyo wa hekima na wa ufahamu, kiasi kwamba hajakuwepo mtu mwingine kama wewe, wala kamwe hatakuwepo baada yako.
13 Sana istemediklerini de vereceğim: Yaşadığın sürece öbür kralların erişemeyeceği bir zenginlik ve onura ulaşacaksın.
Zaidi ya hayo, nitakupa yale ambayo hukuomba, yaani utajiri na heshima, ili kwamba maisha yako yote hapatakuwa na mtu kama wewe miongoni mwa wafalme.
14 Eğer sen de baban Davut gibi kurallarıma ve buyruklarıma uyup yollarımda yürürsen, sana uzun ömür de vereceğim.”
Nawe kama ukienenda katika njia zangu na kutii sheria na amri zangu kama baba yako Daudi alivyofanya, nitakupa maisha marefu.”
15 Süleyman uyanınca bunun bir rüya olduğunu anladı. Sonra Yeruşalim'e gitti, Rab'bin Antlaşma Sandığı'nın önünde durup yakmalık sunular ve esenlik sunuları sundu. Ayrıca bütün görevlilerine de bir şölen verdi.
Ndipo Solomoni akaamka, akatambua kuwa ilikuwa ndoto. Akarudi Yerusalemu, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Bwana, naye akatoa dhabihu za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha akawafanyia watumishi wake wote karamu.
16 Bir gün iki fahişe gelip kralın önünde durdu.
Basi wanawake wawili makahaba walikuja kwa mfalme na kusimama mbele yake.
17 Kadınlardan biri krala şöyle dedi: “Efendim, bu kadınla ben aynı evde kalıyoruz. Birlikte kaldığımız sırada ben bir çocuk doğurdum.
Mmojawapo akasema, “Bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi kwenye nyumba moja. Nilikuwa nimezaa alipokuwa pamoja nami.
18 İki gün sonra da o doğurdu. Evde yalnızdık, ikimizden başka kimse yoktu.
Siku ya tatu baada ya mtoto wangu kuzaliwa, mwanamke huyu pia naye akazaa mtoto. Tulikuwa peke yetu, hapakuwa na mtu mwingine yeyote katika nyumba isipokuwa sisi wawili.
19 Bu kadın geceleyin çocuğunun üzerine yattığı için çocuk ölmüş.
“Wakati wa usiku mwana wa huyu mwanamke akafa kwa sababu alimlalia.
20 Gece yarısı, ben kulun uyurken, kalkıp çocuğumu almış, koynuna yatırmış, kendi ölü çocuğunu da benim koynuma koymuş.
Hivyo akaondoka katikati ya usiku na kumchukua mwanangu kutoka ubavuni pangu wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa nimelala. Akamweka kifuani mwake na kumweka mwanawe aliyekufa kifuani mwangu.
21 Sabahleyin oğlumu emzirmek için kalktığımda, onu ölmüş buldum. Ama sabah aydınlığında dikkatle bakınca, onun benim doğurduğum çocuk olmadığını anladım.”
Asubuhi yake, nikaamka ili kumnyonyesha mwanangu, naye alikuwa amekufa! Lakini nilipomwangalia sana katika nuru ya asubuhi, niliona kuwa hakuwa yule mwana niliyekuwa nimemzaa.”
22 Öbür kadın, “Hayır! Yaşayan çocuk benim, ölü olan senin!” diye çıkıştı. Birinci kadın, “Hayır! Ölen çocuk senin, yaşayan çocuk benim!” diye diretti. Kralın önünde böyle tartışıp durdular.
Huyo mwanamke mwingine akasema, “Hapana! Mwana aliye hai ndiye wangu, aliyekufa ni wako.” Lakini yule wa kwanza akasisitiza, “Hapana! Mwana aliyekufa ni wako, aliye hai ni wangu.” Hivi ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme.
23 Kral, “Biri, ‘Yaşayan çocuk benim, ölü olan senin’ diyor, öbürü, ‘Hayır! Ölen çocuk senin, yaşayan benim’ diyor.
Mfalme akasema, “Huyu anasema, ‘Mwanangu ndiye aliye hai, na aliyekufa ndiye mwanao,’ maadamu yule anasema, ‘Hapana! Aliyekufa ni wako, na aliye hai ni wangu.’”
24 O halde bana bir kılıç getirin!” dedi. Kılıç getirilince,
Kisha mfalme akasema, “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga.
25 kral, “Yaşayan çocuğu ikiye bölüp yarısını birine, yarısını öbürüne verin!” diye buyurdu.
Ndipo mfalme akatoa amri: “Mkate mtoto aliye hai vipande viwili; mpe huyu nusu na mwingine nusu.”
26 Yüreği oğlunun acısıyla sızlayan, çocuğun gerçek annesi krala, “Aman efendim, sakın çocuğu öldürmeyin! Ona verin!” dedi. Öbür kadınsa, “Çocuk ne benim, ne de senin olsun, onu ikiye bölsünler!” dedi.
Mwanamke ambaye mwanawe alikuwa hai akajawa na huruma kwa ajili ya mwanawe na kumwambia mfalme, “Tafadhali, bwana wangu, mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue!” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Mkate vipande viwili. Asiwe wangu au wake!”
27 O zaman kral kararını verdi: “Sakın çocuğu öldürmeyin! Birinci kadına verin, çünkü gerçek annesi odur.”
Kisha mfalme akatoa uamuzi wake: “Mpeni mama wa kwanza mtoto aliye hai. Msimuue; ndiye mama yake.”
28 Kralın verdiği bu kararı duyan bütün İsrailliler hayranlık içinde kaldı. Herkes adil bir yönetim için Süleyman'ın Tanrı'dan gelen bilgeliğe sahip olduğunu anladı.
Wakati Israeli yote iliposikia hukumu aliyotoa mfalme, wakamwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa alikuwa na hekima kutoka kwa Mungu kwa kutoa haki.

< 1 Krallar 3 >