< 1 Krallar 10 >

1 Saba Kraliçesi, RAB'bin adından ötürü Süleyman'ın artan ününü duyunca, onu çetin sorularla sınamaya geldi.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
2 Çeşitli baharat, çok miktarda altın ve değerli taşlarla yüklü büyük bir kervan eşliğinde Yeruşalim'e gelen kraliçe, aklından geçen her şeyi Süleyman'la konuştu.
Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
3 Süleyman onun bütün sorularına karşılık verdi. Kralın ona yanıt bulmakta güçlük çektiği hiçbir konu olmadı.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
4 Süleyman'ın bilgeliğini, yaptırdığı sarayı, sofrasının zenginliğini, görevlilerinin oturup kalkışını, hizmetkârlarının özel giysileriyle yaptığı hizmeti, sakilerini ve RAB'bin Tapınağı'nda sunduğu yakmalık sunuları gören Saba Kraliçesi hayranlık içinde kaldı.
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
5
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
6 Krala, “Ülkemdeyken yaptıklarınla ve bilgeliğinle ilgili duyduklarım doğruymuş” dedi,
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
7 “Ama gelip kendi gözlerimle görünceye dek inanmamıştım. Bunların yarısı bile bana anlatılmadı. Bilgeliğin de, zenginliğin de duyduklarımdan kat kat fazla.
Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
8 Ne mutlu adamlarına! Ne mutlu sana hizmet eden görevlilere! Çünkü sürekli bilgeliğine tanık oluyorlar.
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
9 Senden hoşnut kalan, seni İsrail tahtına oturtan Tanrın RAB'be övgüler olsun! RAB İsrail'e sonsuz sevgi duyduğundan, adaleti ve doğruluğu sağlaman için seni kral yaptı.”
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
10 Saba Kraliçesi krala 120 talant altın, çok büyük miktarda baharat ve değerli taşlar armağan etti. Krala o kadar baharat armağan etti ki, bir daha bu kadar çok baharat görülmedi.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
11 Bu arada Hiram'ın gemileri Ofir'den altın ve büyük miktarda almug kerestesiyle değerli taşlar getirdiler.
(Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
12 Kral, RAB'bin Tapınağı'yla sarayın tırabzanlarını, çalgıcıların lirleriyle çenklerini bu almug kerestesinden yaptırdı. Bugüne dek o kadar almug ağacı ne gelmiş, ne de görülmüştür.
Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
13 Kral Süleyman Saba Kraliçesi'nin her isteğini, her dileğini yerine getirdi. Ayrıca ona gönülden kopan birçok armağan verdi. Bundan sonra kraliçe adamlarıyla birlikte oradan ayrılıp kendi ülkesine döndü.
Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
14 Süleyman'a bir yılda gelen altının miktarı 666 talantı buluyordu.
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
15 Alım satımla uğraşanlarla tüccarların kazançlarından ve Arabistan'ın bütün krallarıyla İsrail valilerinden gelenler bunun dışındaydı.
mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
16 Kral Süleyman her biri altı yüz şekel ağırlığında dövme altından iki yüz büyük kalkan yaptırdı.
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
17 Ayrıca her biri üç mina ağırlığında dövme altından üç yüz küçük kalkan yaptırdı. Kral bu kalkanları Lübnan Ormanı adındaki saraya koydu.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
18 Kral fildişinden büyük bir taht yaptırıp saf altınla kaplattı.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
19 Tahtın altı basamağı, arka kısmında yuvarlak bir başlığı vardı. Oturulan yerin iki yanında kollar, her kolun yanında birer aslan heykeli bulunuyordu.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
20 Altı basamağın iki yanında on iki aslan heykeli vardı. Hiçbir krallıkta böylesi yapılmamıştı.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
21 Kral Süleyman'ın kadehleriyle Lübnan Ormanı adındaki sarayın bütün eşyaları saf altından yapılmış, hiç gümüş kullanılmamıştı. Çünkü Süleyman'ın döneminde gümüşün değeri yoktu.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
22 Hiram'ın gemilerinin yanısıra, kralın da denizde ticaret gemileri vardı. Bu gemiler üç yılda bir altın, gümüş, fildişi ve türlü maymunlarla yüklü olarak dönerlerdi.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
23 Kral Süleyman dünyanın bütün krallarından daha zengin, daha bilgeydi.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
24 Tanrı'nın Süleyman'a verdiği bilgeliği dinlemek için bütün dünya onu görmek isterdi.
Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
25 Onu görmeye gelenler her yıl armağan olarak altın ve gümüş eşya, giysi, silah, baharat, at, katır getirirlerdi.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
26 Süleyman savaş arabalarıyla atlarını topladı. Bin dört yüz savaş arabası, on iki bin atı vardı. Bunların bir kısmını savaş arabaları için ayrılan kentlere, bir kısmını da kendi yanına, Yeruşalim'e yerleştirdi.
Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
27 Krallığı döneminde Yeruşalim'de gümüş taş değerine düştü. Sedir ağaçları Şefela'daki yabanıl incir ağaçları kadar bollaştı.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Süleyman'ın atları Mısır ve Keve'den getirilirdi. Kralın tüccarları atları Keve'den satın alırdı.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
29 Mısır'dan bir savaş arabası altı yüz, bir at yüz elli şekel gümüşe getirilirdi. Bunları bütün Hitit ve Aram krallarına satarlardı.
Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.

< 1 Krallar 10 >