< 1 Tarihler 7 >

1 İssakar'ın dört oğlu vardı: Tola, Pua, Yaşuv, Şimron.
Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
2 Tola'nın oğulları: Uzzi, Refaya, Yeriel, Yahmay, Yivsam, Samuel. Bunlar Tola boyunun başlarıydı. Soy kütüğüne göre yiğit savaşçılardı. Davut döneminde sayıları 22 600'dü.
Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
3 Uzzi'nin oğlu: Yizrahya. Yizrahya'nın oğulları: Mikael, Ovadya, Yoel, Yişşiya. Beşi de boy başıydı.
Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
4 Soy kütüğüne göre, aralarında savaşa hazır 36 000 kişi vardı. Hepsinin çok sayıda karısı ve çocuğu vardı.
Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
5 Soy kütüğüne göre İssakar boylarına bağlı akrabalarından savaşacak durumda olanların sayısı 87 000'di.
Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
6 Benyamin'in üç oğlu vardı: Bala, Beker, Yediael.
Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
7 Bala'nın beş oğlu vardı: Esbon, Uzzi, Uzziel, Yerimot, İyri. Bunlar boy başıydı. Soy kütüğüne kayıtlı yiğit savaşçıların sayısı 22 034 kişiydi.
Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
8 Beker'in oğulları: Zemira, Yoaş, Eliezer, Elyoenay, Omri, Yeremot, Aviya, Anatot, Alemet. Hepsi Beker'in oğullarıydı.
Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
9 Bunların soy kütüğüne kayıtlı aile başlarının ve yiğit savaşçıların sayısı 20 200'dü.
Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
10 Yediael'in oğlu: Bilhan. Bilhan'ın oğulları: Yeuş, Benyamin, Ehut, Kenaana, Zetan, Tarşiş, Ahişahar.
Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
11 Yediael'in bütün oğulları boy başlarıydı. Aralarında savaşa hazır 17 200 yiğit savaşçı vardı.
Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
12 Şuppim ve Huppim İr'in, Huşim ise Aher'in oğluydu.
Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
13 Naftali'nin oğulları: Yahasiel, Guni, Yeser, Şallum. Bunlar Bilha'nın soyundandı.
Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
14 Manaşşe'nin oğulları: Aramlı cariyenin doğurduğu Asriel, Makir. Makir Gilat'ın babasıydı.
Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
15 Makir Huppim'le Şuppim'in kızkardeşi Maaka'yı karı olarak aldı. Makir'in ikinci oğlunun adı Selofhat'tı. Selofhat'ın yalnız kızları oldu.
Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
16 Makir'in karısı Maaka, Pereş ve Şereş adında iki oğul doğurdu. Şereş'in de Ulam ve Rekem adında iki oğlu oldu.
Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
17 Ulam'ın oğlu: Bedan. Manaşşe oğlu Makir oğlu Gilat'ın oğulları bunlardır.
Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
18 Gilat'ın kızkardeşi Hammoleket İşhot'u, Aviezer'i, Mahla'yı doğurdu.
Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
19 Şemida'nın oğulları: Ahyan, Şekem, Likhi, Aniam.
Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
20 Efrayim'in oğulları: Şutelah, Ezer ve Elat. Beret Şutelah'ın, Tahat Beret'in, Elada Tahat'ın, Tahat Elada'nın, Zavat Tahat'ın, Şutelah da Zavat'ın oğluydu. Ülkede doğup büyüyen Gatlılar Ezer'le Elat'ı öldürdüler. Çünkü onların sürülerini çalmaya gitmişlerdi.
Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
22 Babaları Efrayim günlerce yas tuttu. Akrabaları onu avutmaya geldiler.
Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
23 Efrayim karısıyla yine yattı. Kadın gebe kalıp bir oğul doğurdu. Evinde talihsizlik var diye babası oğlana Beria adını verdi.
Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
24 Kızı Aşağı ve Yukarı Beythoron'u, Uzzen-Şeera'yı kuran Şeera'ydı.
Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
25 Beria'nın Refah adında bir oğlu vardı. Refah Beria'nın, Reşef Refah'ın, Telah Reşef'in, Tahan Telah'ın, Ladan Tahan'ın, Ammihut Ladan'ın, Elişama Ammihut'un, Nun Elişama'nın, Yeşu da Nun'un oğluydu.
Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
28 Efrayimliler'in yerleştikleri topraklar Beytel'i ve çevresindeki köyleri, doğuda Naaran'ı, batıda Gezer'i ve köylerini, Şekem, Aya ve köylerini kapsıyordu.
Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
29 Manaşşe oymağının sınırında Beytşean, Taanak, Megiddo, Dor ve bunlara ait köyler vardı. İsrail oğlu Yusuf'un soyu buralarda yaşadı.
Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
30 Aşer'in oğulları: Yimna, Yişva, Yişvi, Beria; kızkardeşleri Serah.
Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
31 Beriaoğulları: Hever ve Birzayit'in kurucusu Malkiel.
Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
32 Hever Yaflet, Şomer, Hotam ve kızkardeşleri Şua'nın babasıydı.
Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
33 Yafletoğulları: Pasak, Bimhal, Aşvat. Yaflet'in oğulları bunlardı.
Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
34 Şomeroğulları: Ahi, Rohga, Yehubba, Aram.
Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
35 Kardeşi Helem'in oğulları: Sofah, Yimna, Şeleş, Amal.
Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
36 Sofahoğulları: Suah, Harnefer, Şual, Beri, Yimra,
Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
37 Beser, Hod, Şamma, Şilşa, Yitran, Beera.
Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
38 Yeteroğulları: Yefunne, Pispa, Ara.
Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
39 Ulla'nın oğulları: Arah, Hanniel, Risya.
Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
40 Bunların hepsi Aşer soyundandı. Boy başları, seçkin kişiler, yiğit savaşçılar ve tanınmış önderlerdi. Soy kütüğüne kayıtlı savaşa hazır olanların sayısı yirmi altı bindi.
Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.

< 1 Tarihler 7 >