< Matendo 8 >

1 Saulo naye alikiona kitendo hicho cha kumwua Stefano kuwa sawa. Siku hiyo kanisa la Yerusalemu lilianza kuteswa vibaya. Waumini wote, isipokuwa tu wale mitume, walilazimika kutawanyika katika sehemu za mashambani za Yudea na Samaria.
But Saul was consentynge to his deth. And greet persecucioun was maad that dai in the chirche, that was in Jerusalem. And alle men weren scatered bi the cuntrees of Judee and Samarie, outakun the apostlis.
2 Watu wamchao Mungu, walimzika Stefano na kumfanyia maombolezo makubwa.
But good men birieden Steuene, and maden greet mornyng on hym.
3 Wakati huohuo, Saulo alijaribu kuliangamiza kanisa. Alikwenda katika kila nyumba, akawatoa nje waumini, wanaume kwa wanawake, akawatia gerezani.
But Saul greetli distruyede the chirche, and entryde bi housis, and drowe men and wymmen, and bitook hem in to prisoun.
4 Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.
And thei that weren scaterid, passiden forth, prechynge the word of God.
5 Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.
And Filip cam doun in to a citee of Samarie, and prechide to hem Crist.
6 Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.
And the puple yaf tent to thes thingis that weren seid of Filip, with o wille herynge and seynge the signes that he dide.
7 Maana pepo wachafu waliokuwa wamewapagaa watu wengi waliwatoka wakipiga kelele kubwa; na pia watu wengi waliokuwa wamepooza viungo na waliolemaa waliponywa.
For manye of hem that hadden vnclene spirits, crieden with a greet vois, and wenten out.
8 Kukawa na furaha kubwa katika mji ule.
And manye sijk in the palsi, and crokid, weren heelid.
9 Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Simoni ambaye alikuwa amekwisha fanya uchawi wake katika mji huo kwa muda na kuwashangaza watu wa Samaria, akijiona kuwa yeye ni mtu maarufu.
Therfor greet ioye was maad in that citee. But there was a man in that citee, whos name was Symount, a witche, that hadde disseyued the folc of Samarie, seiynge, that him silf was sum greet man.
10 Watu wote, wadogo na wakubwa, walimsikiliza kwa makini wakisema, “Simoni ndiye ile nguvu ya kimungu inayoitwa Nguvu Kubwa.”
Whom alle herkeneden, fro the leest to the moost, and seiden, This is the vertu of God, which is clepid greet.
11 Walivutiwa sana naye kwa vile alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake kwa muda mrefu.
And thei leueden hym, for long tyme he hadde maddid hem with his witche craftis.
12 Lakini walipouamini ujumbe wa Filipo juu ya Habari Njema ya Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanawake na wanaume.
But whanne thei hadden bileued to Filip, `that prechide of the kingdom of God, men and wymmen weren baptisid in the name of Jhesu Crist.
13 Hata Simoni aliamini; baada ya kubatizwa ilikuwa akiandamana na Filipo, akastaajabia maajabu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
And thanne also Symount him silf bileued; and whanne he was baptisid, he drouy to Filip; and he sai also that signes and grete vertues weren don, he was astonyed, and wondride.
14 Wale mitume waliokuwa kule Yerusalemu walipopata habari kwamba wenyeji wa Samaria nao wamelipokea neno la Mungu, waliwatuma kwao Petro na Yohane.
But whanne the apostlis that weren at Jerusalem, hadden herd that Samarie hadde resseyued the word of God, thei senten to hem Petre and Joon.
15 Walipofika waliwaombea hao waumini ili wampokee Roho Mtakatifu;
And whanne thei camen, thei preieden for hem, that thei schulden resseyue the Hooli Goost;
16 maana wakati huo Roho Mtakatifu hakuwa ameshukia yeyote kati yao; walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu.
for he cam not yit in to ony of hem, but thei weren baptisid oonli in the name of the Lord Jhesu.
17 Basi, Petro na Yohane wakawawekea mikono hao waumini, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Thanne thei leiden hoondis on hem, and thei resseyueden the Hooli Goost.
18 Hapo Simoni aling'amua kwamba kwa kuwekewa mikono ya mitume waumini walipewa Roho Mtakatifu. Hivyo aliwapa Petro na Yohane fedha akisema,
And whanne Symount hadde seyn, that the Hooly Goost was youun bi leiyng on of the hoondis of the apostlis, and he proferide to hem money, and seide,
19 “Nipeni na mimi uwezo huo ili yeyote nitakayemwekea mikono, apokee Roho Mtakatifu.”
Yyue ye also to me this power, that whom euere Y schal leye on myn hoondis, that he resseyue the Hooli Goost.
20 Lakini Petro akamjibu, “Potelea mbali na fedha zako kwa vile unafikiri kwamba unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
But Petir seide to hym, Thi money be with thee into perdicioun, for thou gessidist the yifte of God schulde be had for monei.
21 Huna sehemu yoyote wala haki katika kazi hiyo kwa maana moyo wako hauko sawa mbele ya macho ya Mungu.
Ther is no part, ne sort to thee, in this word, for thin herte is not riytful bifor God.
22 Kwa hiyo, tubu ubaya wako huu na umwombe Bwana naye anaweza kukusamehe fikira kama hizo.
Therfor do thou penaunce for this wickidnesse of thee, and preie God, if perauenture this thouyt of thin herte be foryouun to thee.
23 Ni dhahiri kwangu kwamba umejaa wivu mkali na mfungwa wa dhambi!”
For Y se that thou art in the gall of bitternesse and in the boond of wickidnesse.
24 Simoni akajibu, “Tafadhali, niombeeni kwa Bwana lisije likanipata lolote kati ya hayo mliyosema.”
And Symount answeride, and seide, Preie ye for me to the Lord, that no thing of these thingis that ye han seid, com on me.
25 Baada ya Petro na Yohane kutoa ushuhuda wao na kuutangaza ujumbe wa Bwana, walirudi Yerusalemu. Walipokuwa wanarudi walihubiri Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.
And thei witnessiden, and spaken the word of the Lord, and yeden ayen to Jerusalem, and prechiden to many cuntrees of Samaritans.
26 Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Jitayarishe uende kusini kupitia njia inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza.” (Njia hiyo hupita jangwani.)
And an aungel of the Lord spak to Filip, and seide, Ryse thou, and go ayens the south, to the weie that goith doun fro Jerusalem in to Gasa; this is desert.
27 Basi, Filipo akajiweka tayari, akaanza safari. Wakati huohuo kulikuwa na Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa anasafiri kuelekea nyumbani. Huyo mtu alikuwa ofisa maarufu wa hazina ya Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa amekwenda huko Yerusalemu kuabudu na wakati huo alikuwa anarudi akiwa amepanda gari la kukokotwa.
And he roos, and wente forth. And lo! a man of Ethiopie, a myyti man seruaunt, a yelding of Candace, the queen of Ethiopiens, which was on alle her richessis, cam to worschipe in Jerusalem.
28 Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.
And he turnede ayen, sittinge on his chare, and redinge Isaie, the profete.
29 Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo.”
And the spirit seide to Filip, Neiye thou, and ioyne thee to this chare.
30 Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, “Je, unaelewa hayo unayosoma?”
And Filip `ran to, and herde hym redynge Ysaie, the prophete. And he seide, Gessist thou, whether thou vndirstondist, what thingis thou redist?
31 Huyo mtu akamjibu, “Ninawezaje kuelewa bila mtu kunielewesha?” Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.
And he seide, How may Y, if no man schewe to me? And he preiede Filip, that he schulde come vp, and sitte with hym.
32 Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii: “Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa; kimya kama vile mwana kondoo anaponyolewa manyoya, yeye naye hakutoa sauti hata kidogo.
And the place of the scripture that he redde, was this, As a scheep he was led to sleyng, and as a lomb bifor a man that scherith him is doumb with out vois, so he openyde not his mouth.
33 Alifedheheshwa na kunyimwa haki. Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake, kwa maana maisha yake yameondolewa duniani.”
In mekenesse his dom was takun vp; who schal telle out the generacioun of hym? For his lijf schal be takun awei fro the erthe.
34 Huyo Mwethiopia akamwambia Filipo, “Niambie, huyu nabii anasema juu ya nani? Anasema mambo haya juu yake yeye mwenyewe au juu ya mtu mwingine?”
And the gelding answeride to Filip, and seide, Y biseche thee, of `what profete seith he this thing? of him silf, ethir of ony othere?
35 Basi, Filipo akianzia na sehemu hiyo ya Maandiko Matakatifu, akamweleza Habari Njema juu ya Yesu.
And Filip openyde his mouth, and bigan at this scripture, and prechide to him Jhesu.
36 Walipokuwa bado wanaendelea na safari walifika mahali penye maji na huyo ofisa akasema, “Mahali hapa pana maji; je, kuna chochote cha kunizuia nisibatizwe?”
And the while thei wenten bi the weie, thei camen to a water. And the gelding seide, Lo! watir; who forbedith me to be baptisid?
37 Filipo akasema, “Kama unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Naye akajibu, “Naam, ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”
And Filip seide, If thou bileuest of al the herte, it is leueful. And he answeride, and seide, Y bileue that Jhesu Crist is the sone of God.
38 Basi, huyo ofisa akaamuru lile gari lisimame; na wote wawili, Filipo na huyo ofisa wakashuka majini, naye Filipo akambatiza.
And he comaundide the chare to stonde stille. And thei wenten doun bothe into the watir, Filip and the gelding, and Filip baptiside hym.
39 Walipotoka majini Roho wa Bwana akamfanya Filipo atoweke. Na huyo Mwethiopia hakumwona tena; lakini akaendelea na safari yake akiwa amejaa furaha.
And whanne thei weren come vp of the watir, the spirit of the Lord rauyschide Filip, and the gelding say hym no more.
40 Filipo akajikuta yuko Azoto, akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema mpaka alipofika Kaisarea.
And Filip was foundun in Azotus; and he passide forth, and prechide to alle citees, til he cam to Cesarie.

< Matendo 8 >