< 2 Wathesalonike 1 >

1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
Paul and Silvanus and Timothy, to the congregation of Thessalonians in God our Father and the Lord Jesus Christ:
2 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
3 Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
We are indebted to thank God always about you, brothers, as it is fitting, because your faith is increasing greatly, and the love of each one of you all toward each other abounds.
4 Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
So as for us ourselves to have pride in you in the congregations of God, for your perseverance and faith in all your persecutions and in the tribulations that ye endure,
5 Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
being evidence of the righteous judgment of God, for you to be considered worthy of the kingdom of God, for which also ye suffer.
6 Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
Since it is a righteous thing according to God to repay restriction to those who restrict you,
7 na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
and relief with us, to you who are restricted, at the revealing of the Lord Jesus from heaven with his agents of power
8 na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
in a fire of flame rendering vengeance to those who have not known God, and to those not obeying the good news of our Lord Jesus Christ.
9 Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, (aiōnios g166)
Men who will suffer punishment, a penalty of eternal destruction from the presence of the Lord and from the glory of his might, (aiōnios g166)
10 wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
when he comes to be glorified in his sanctified, and to be marveled in that day by all those who believe (because our testimony among you was believed).
11 Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
For which also we pray always about you, so that our God will make you worthy of the calling, and will fulfill every desire of goodness and work of faith with power.
12 Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
So that the name of our Lord Jesus Christ may be glorified in you and ye in him, according to the grace of our God and the Lord Jesus Christ.

< 2 Wathesalonike 1 >