< 2 Wathesalonike 2 >

1 Sasa yahusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa kwetu pamoja tukae naye. Ndugu, tunawaombeni sana
Now we ask you, brothers, on behalf of the coming of our Lord Jesus Christ and our gathering together to him,
2 msifadhaike upesi moyoni, na wala msitiwe wasiwasi kwa sababu ya madai kwamba Siku ya Bwana imekwisha fika. Labda inadhaniwa kwamba jambo hili limetokana na uaguzi fulani, mahubiri au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu.
for ye not to be quickly shaken from your mind, nor to be alarmed, neither by spirit, nor by word, nor by a letter as by us, as that the day of the Christ has come.
3 Msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa namna yoyote ile. Maana Siku hiyo haitakuja mpaka kwanza ule Uasi Mkuu utokee na yule Mwovu aonekane ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa.
Let not any man deceive you in any way, because if not, the defection may come first, and he may be revealed-the man of sin, the son of destruction,
4 Yeye atapinga kila kitu wanachokiona watu kuwa ni mungu, au wanachokiabudu. Naam, hata ataingia na kuketi ndani ya Hekalu la Mungu akijidai kuwa Mungu.
who opposes and exalts himself against all that is called God or an object of worship, so as for him to sit in the temple of God, as God, displaying himself that he is God.
5 Je, hamkumbuki kwamba niliwaambieni haya yote wakati nilipokuwa pamoja nanyi?
Do ye not remember that when I was yet with you I told you these things?
6 Lakini kuna kitu kinachomzuia sasa, nanyi mwakijua kitu hicho. Basi, huyo Mwovu ataonekana wakati wake ufaao.
And now ye know that which restrains, for him to be revealed in his own time.
7 Hata hivyo, Mwovu huyo aliyefichika anafanya kazi sasa, lakini hataonekana mpaka yule anayemzuia aondolewe.
For the mystery of lawlessness is already working, only he who restrains it until now will develop from the midst.
8 Hapo ndipo Mwovu atakapotokea; lakini Bwana Yesu anapokuja atamuua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kwa mng'ao wa kuja kwake.
And then the lawless will be revealed, whom the Lord will consume with the spirit of his mouth, and will neutralize at the appearance of his coming.
9 Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,
Whose coming is according to the working of Satan with all power and signs and marvels of deceit,
10 na kutumia udanganyifu wa kila namna kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea. Hao watapotea kwa sababu hawakuupokea na kuupenda ule ukweli ili waokolewe.
and in all deception of unrighteousness in those who are perishing, in return for which, they did not accept the love of the truth in order for them to be saved.
11 Ndiyo maana Mungu amewaweka chini ya nguvu ya upotovu, wauamini uongo.
And because of this God will send them the force of a delusion, for them to believe a lie,
12 Matokeo yake ni kwamba wote wasioamini ukweli, ila wafurahia dhambi, watahukumiwa.
so that they might be condemned-all those who did not believe the truth, but who delighted in unrighteousness.
13 Tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi ndugu, ninyi mnaopendwa na Bwana, kwa maana Mungu amewateua tangu mwanzo mpate kuokolewa kwa nguvu ya Roho mfanywe watu wake watakatifu kwa imani yenu katika ukweli.
But we are indebted to express thanks to God always about you, brothers, beloved by the Lord, because God chose you from the beginning for salvation, in sanctification of spirit and belief of truth,
14 Mungu aliwaitieni jambo hili kwa njia ya Habari Njema tuliyowahubirieni; aliwaiteni mpate kupokea sehemu yenu katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
for which he called you, through our good news, for an acquired possession of glory of our Lord Jesus Christ.
15 Basi, ndugu, simameni imara na zingatieni yale mafundisho tuliyowafundisheni kwa mahubiri yetu na barua zetu.
So then, brothers, stand firm and hold to the traditions that ye were taught, whether by word or by letter from us.
16 Tunamwomba Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu ambaye alitupenda, na kwa neema yake akatujalia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios g166)
And may our Lord Jesus Christ himself, and our God and Father who loved us and gave eternal encouragement and good hope through grace, (aiōnios g166)
17 aifariji mioyo yenu na kuwaimarisheni ili mweze daima kutenda na kusema yaliyo mema.
encourage your hearts and establish you in every good word and work.

< 2 Wathesalonike 2 >