< 2 Petro 1 >

1 Mimi Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo, nawaandikia ninyi ambao, kwa wema wake Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo, mmejaliwa imani ileile ya thamani kuu tuliyojaliwa sisi.
Simon Peter, a bondman and apostle of Jesus Christ, to those who have received an equally precious faith with us in the righteousness of our God and Savior Jesus Christ:
2 Nawatakieni neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
Grace to you and peace be multiplied in the knowledge of God and of Jesus our Lord,
3 Kwa uwezo wake wa kimungu, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji, ili tuishi maisha ya kumcha Mungu kwa kumjua yeye aliyetuita tuushiriki utukufu na wema wake yeye mwenyewe.
as all things of his divine power to us, things toward life and piety, which were granted through the knowledge of him who called us through glory and virtue.
4 Kwa namna hiyo ametujalia zawadi kuu na za thamani ambazo alituahidia, ili kwa zawadi hizo mpate kuziepa kabisa tamaa mbaya zilizomo duniani, na mpate kuishiriki hali yake ya kimungu.
Because of which, the precious and greatest promises have been given to us, so that through these ye might become companions of the divine nature, having escaped from the corruption in the world in lust.
5 Kwa sababu hiyo, fanyeni bidii ya kuongeza fadhila katika imani yenu: ongezeni elimu katika fadhila yenu,
Now this same thing also, having applied all eagerness, furnish in your faith, virtue, and in virtue, knowledge,
6 kuwa na kiasi katika elimu yenu, uvumilivu katika kuwa na kiasi, uchaji wa Mungu katika uvumilivu wenu,
and in knowledge, self-control, and in self-control, perseverance, and in perseverance, piety,
7 udugu katika uchaji wenu, na mapendo katika udugu wenu.
and in piety, brotherly affection, and in brotherly affection, love.
8 Mkiwa na sifa hizo zote kwa wingi, zitawawezesheni kuwa watendaji na kupata faida katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
For these things existing in you and abounding, it leads to not being idle nor unfruitful in the knowledge of our Lord Jesus Christ.
9 Lakini mtu asiye na sifa hizo ni kipofu, hawezi kuona na amesahau kwamba alikwisha takaswa dhambi zake za zamani.
For he in whom these things are not present is blind, being near-sighted, having deliberately forgotten the purification of his former sins.
10 Kwa hiyo basi, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuufanya huo wito wenu mlioitiwa na Mungu uwe jambo la kudumu katika maisha yenu; kama mkiishi namna hiyo hamtaanguka kamwe.
Therefore, brothers, instead be diligent to make your calling and selection sure, for doing these things, ye would, no, not ever stumble.
11 Kwa namna hiyo mtafaulu kupewa haki kamili ya kuingia katika Utawala wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios g166)
For so the entrance will be furnished to you abundantly into the eternal kingdom of our Lord and Savior Jesus Christ. (aiōnios g166)
12 Kwa hiyo nitaendelea kuwakumbusheni daima mambo haya, ingawa mmekwisha yafahamu, na mko imara katika ukweli mlioupokea.
Therefore I will not neglect to always remind you about these things, although having known them, and having been established in the present truth.
13 Nadhani ni jambo jema kwangu, muda wote niishio hapa duniani, kuwapeni moyo na kuwakumbusheni juu ya mambo haya.
But I think it right, inasmuch as I am in this tent, to arouse you in memory.
14 Najua kwamba karibu nitauweka kando mwili huu wenye kufa, kama Bwana alivyoniambia waziwazi.
Knowing that the putting off of my tent is imminent, even as also our Lord Jesus Christ indicated to me.
15 Basi, nitajitahidi kuwapatieni njia ya kuyakumbuka mambo haya kila wakati, baada ya kufariki kwangu.
And also I will endeavor for you to always have, after my departure, the memory of these things to apply.
16 Wakati tulipowafundisheni juu ya ukuu wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hatukutegemea hadithi tupu zisizo na msingi. Sisi tuliuona utukufu wake kwa macho yetu wenyewe.
For we revealed to you the power and presence of our Lord Jesus Christ, not men who followed in cunningly devised myths, but men who became eyewitnesses of the majesty of that man.
17 Sisi tulikuwapo wakati alipopewa heshima na kutukuzwa na Mungu Baba, wakati sauti ilipomjia kutoka kwake yeye aliye Utukufu Mkuu, ikisema: “Huyu ni Mwanangu mpenzi, nimependezwa naye.”
For having received from God the Father honor and glory from a voice of such kind brought to him from the Majestic Glory, This is my Son, the beloved in whom I am well pleased.
18 Tena, sisi wenyewe tulisikia sauti hiyo kutoka mbinguni wakati tulipokuwa pamoja naye juu ya ule mlima mtakatifu.
And we heard this voice, which was brought out of heaven, being with him on the holy mountain.
19 Tena, ujumbe wa manabii watuthibitishia jambo hilo; nanyi mwafanya vema kama mkiuzingatia, maana ni kama taa inayoangaza mahali penye giza mpaka Siku ile itakapopambazuka na mwanga wa nyota ya asubuhi utakapong'ara mioyoni mwenu.
And we have the prophetic word sure, to which ye do well giving heed, as to a lamp shining in a dark place, until the day dawns, and the daystar arises in your hearts.
20 Zaidi ya hayo, lakini, kumbukeni kwamba hakuna mtu yeyote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu.
Knowing this first, that no prophecy of scripture comes to pass of a personal interpretation.
21 Maana hakuna ujumbe wa kinabii unaotokana na matakwa ya binadamu, bali watu walinena ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
For no prophecy was ever brought by a will of man, but holy men of God spoke, being led by the Holy Spirit.

< 2 Petro 1 >