< Sefania 3 >

1 Ole kwa mji ulioasi! Mji wenye vurugu umenajisiwa.
Woe to her that is filthy and polluted, to the oppressing city!
2 Haukuisikiliza sauti ya Mungu, wala haukupokea masahihisho kutoka kwa Yahwe. Hakumtumaini Yahwe na hatamkaribia Mungu wake.
She hearkened not to the voice, she received not correction; she trusted not in the LORD, she drew not near to her God.
3 Wafalme wao ni simba wanaounguruma miongoni mwao. Waamuzi wao ni mbwa mwitu wa jioni wasiobakiza kitu ambacho kitakuwa kimemung'unywa asubuhi yake.
Her princes in the midst of her are roaring lions; her judges are wolves of the desert, they leave not a bone for the morrow.
4 Manabii wake wanakiburi na wanaume wasaliti. Makuhani wake wamepanajisi mahali patakatifu na wameifanyia vurugu sheria.
Her prophets are wanton and treacherous persons; her priests have profaned that which is holy, they have done violence to the law.
5 Yahwe ni mwenye haki miongoni mwao. Hawezi kufanya makosa. Kila asubuhi husimamia haki yake! Haitafichika nuruni, hata hivyo watu wasio wenye haki hawajui kuona aibu.
The LORD who is righteous is in the midst of her, He will not do unrighteousness; every morning doth He bring His right to light, it faileth not; but the unrighteous knoweth no shame.
6 Nimeyaharibu mataifa; ngome zao zimeharibiwa. Nimeifanya mitaa yao magofu, hivyo hakuna hata mmoja anayepitia kwake. Miji yao imeharibiwa kwa hiyo hakuna mtu anayeikaa.
I have cut off nations, their corners are desolate; I have made their streets waste, so that none passeth by; their cities are destroyed, so that there is no man, so that there is no inhabitant.
7 Nikasema, 'Hakika mtaniogopa mimi. Pokeeni masahihisho na msikatiliwe mbali kutoka kwenye miji yenu kwa yote yale niliyokuwa nimeyapanga kuyafanya kwenu.' Lakini walikuwa na shauku kuanza kila siku kwa kuharibu matendo yao yote.
I said: 'Surely thou wilt fear Me, thou wilt receive correction; so her dwelling shall not be cut off, despite all that I have visited upon her'; but they betimes corrupted all their doings.
8 Kwa hiyo ningojeni - hili ni tamko la Yahwe - mpaka siku ambayo nitainuka kwa ajili ya waathirika. Uaamuzi wangu nikuwakusanya mataifa, kuzikusanya falme, na kumwaga juu yao hasira yangu, uchungu wangu wote mkali, hivyo nchi yote itamezwa kwa moto wa hasira yangu.
Therefore wait ye for Me, saith the LORD, until the day that I rise up to the prey; for My determination is to gather the nations, that I may assemble the kingdoms, to pour upon them Mine indignation, even all My fierce anger; for all the earth shall be devoured with the fire of My jealousy.
9 Ndipo nitawapa midomo safi watu, kuwaita wote kwa jina la Bwana kunitumikia wakisimama bega kwa bega.
For then will I turn to the peoples a pure language, that they may all call upon the name of the LORD, to serve Him with one consent.
10 Kutoka ng'ambo ya mto Ethiopia waniabuduo - watu wangu waliotawanyika - wataleta dhabihu kwa sababu yangu.
From beyond the rivers of Ethiopia shall they bring My suppliants, even the daughter of My dispersed, as Mine offering.
11 Katika siku hiyo hamtawekwa kwenye woga kwa matendo yenu yote ambayo mmeyafanya dhidi yangu, tangu wakati ule nitaondoa kutoka kwenu wale waliosherehekea fahari yenu, na kwa sababu hamtakuwa na muda mrefu kufanya majivuno juu ya mlima wangu mtakatifu.
In that day shalt thou not be ashamed for all thy doings, wherein thou hast transgressed against Me; for then I will take away out of the midst of thee thy proudly exulting ones, and thou shalt no more be haughty in My holy mountain.
12 Lakini nitawaacha kama wa chini zaidi na watu masikini, na mtapata kimbilio katika jina la Yahwe.
And I will leave in the midst of thee an afflicted and poor people, and they shall take refuge in the name of the LORD.
13 Mkazi wa Israeli si muda mrefu hatafanya udhalimu au kusema uongo, na hakuna ulimi wa udanganyifu utakaoonekana mdomoni mwao; hivyo watalisha na kulala chini, na hakuna hata mmoja atakayewafanya kuogopa.”
The remnant of Israel shall not do iniquity, nor speak lies, neither shall a deceitful tongue be found in their mouth; for they shall feed and lie down, and none shall make them afraid.
14 Imba, binti Sayuni! Piga kelele, Israeli. Ufurahi na kushangilia kwa moyo wako wote, binti wa Yerusalemu.
Sing, O daughter of Zion, shout, O Israel; be glad and rejoice with all the heart, O daughter of Jerusalem.
15 Yahwe ameiondoa hukumu yako; amewafukuzia mbali adui zako! Yahwe ni mfalme wa Israeli miongoni mwenu. Kamwe hamtamwogopa tena mwovu!
The LORD hath taken away thy judgments, He hath cast out thine enemy; The King of Israel, even the LORD, is in the midst of thee; thou shalt not fear evil any more.
16 Katika siku hizo watasema kwa Yerusalemi, “Usiogope, Sayuni. Usiiache mikono yako ilegee.
In that day it shall be said to Jerusalem: 'Fear thou not; O Zion, let not thy hands be slack.
17 Yahwe Mungu wako yuko katikati yenu, mwenye nguvu wa kuwaokoa. Atasherehekea juu yenu na kwa furaha atakuwa kimya juu yenu kwa upendo wake. Atakuwa na furaha juu yenu na atashangilia kwa furaha,
The LORD thy God is in the midst of thee, a Mighty One who will save; He will rejoice over thee with joy, He will be silent in His love, He will joy over thee with singing.'
18 katika siku maalumu ya sherehe. Nitaondoa maafa kutoka kwenu; si muda mrefu hamtabeba aibu kwa ajili yake.
I will gather them that are far from the appointed season, who are of thee, that hast borne the burden of reproach.
19 Tazama, Niko tayari kuwashughulikia watesi wenu wote. Katika wakati ule, Nitawaokoa waliolemaa na kuwakusanya waliotupiliwa mbali. Nitawafanya kuwa sifa, na nitaibadilisha aibu yao iwe sifa katika dunia yote.
Behold, at that time I will deal with all them that afflict thee; and I will save her that is lame, and gather her that was driven away; and I will make them to be a praise and a name, whose shame hath been in all the earth.
20 Katika wakati ule nitawaongoza; katika wakati ule nitawakusanya pamoja. Nitawafanya mataifa yote ya dunia kuwaheshimu na kuwasifu, wakati mtakapoona hivyo, Nitakuwa nimewarudisha”, asema Yahwe.
At that time will I bring you in, and at that time will I gather you; for I will make you to be a name and a praise among all the peoples of the earth, when I turn your captivity before your eyes, saith the LORD.

< Sefania 3 >