< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja ninyi wenyewe mkutano wa hadhara na kusanyikeni, taifa lisilokuwa na aibu -
Gather yourselves together, yea, gather together, O shameless nation;
2 kabla amri kuchukua madhara na siku hiyo kupita kama makapi, kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahwe kuja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana kuja juu yenu.
Before the decree bring forth the day when one passeth as the chaff, before the fierce anger of the LORD come upon you, before the day of the LORD'S anger come upon you.
3 Mtafuteni Yahwe, ninyi watu wote wanyenyekevu duniani mnaozitii amri zake! Tafuteni haki yake. Tafuteni unyenyekevu, na labda mtalindwa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe.
Seek ye the LORD, all ye humble of the earth, that have executed His ordinance; seek righteousness, seek humility. It may be ye shall be hid in the day of the LORD'S anger.
4 hivyo Gaza utatelekezwa, na Ashkeloni utageuka kuwa uharibifu. Watauondoshea mbali Ashdodi wakati wa mchana, na wataung'oa Ekroni!
For Gaza shall be forsaken, and Ashkelon a desolation; they shall drive out Ashdod at the noonday, and Ekron shall be rooted up.
5 Ole kwa wanaokaa kando ya bahari, taifa la Wakerethi! Yahwe amesema dhidi yenu, Kanaani, nchi ya Wafilisiti. Nitawaangamiza hakuna mkazi atakayebakia.
Woe unto the inhabitants of the sea-coast, the nation of the Cherethites! the word of the LORD is against you, O Canaan, the land of the Philistines; I will even destroy thee, that there shall be no inhabitant.
6 Hiyo nchi ya kando ya bahari itakuwa malisho kwa wachungaji na kwa mazizi ya kondoo.
And the sea-coast shall be pastures, even meadows for shepherds, and folds for flocks.
7 Nchi ya kando ya bahari itakuwa mali ya mabaki ya watu wa nyumba ya Yuda, watakaochungia makundi yao huko. Watu wao watalala jioni katika nyumba ya Ashikeloni, kwa kuwa Yahwe Mungu wao atawatunza na kurejesha wafungwa wao.
And it shall be a portion for the remnant of the house of Judah, whereon they shall feed; in the houses of Ashkelon shall they lie down in the evening; for the LORD their God will remember them, and turn their captivity.
8 Nilizisikia dhihaka za Moabu na wakiwatukana watu wa Amoni wakati walipowadhihaki watu wangu na kujitukuza mipakani mwao.
I have heard the taunt of Moab, and the revilings of the children of Ammon, wherewith they have taunted My people, and spoken boastfully concerning their border.
9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, - Moabu itakuja kuwa kama Sodoma, na watu wa Amoni kama Gomora; mahali pa viwavi na shimo la chumvi, jangwa la daima. Lakini watu wangu waliosalia watawateka mateka, na watu wa taifa langu waliobaki watachukua umiliki wao.'
Therefore as I live, saith the LORD of hosts, the God of Israel: Surely Moab shall be as Sodom, and the children of Ammon as Gomorrah, even the breeding-place of nettles, and saltpits, and a desolation, for ever; the residue of My people shall spoil them, and the remnant of My nation shall inherit them.
10 Hili litatokea kwa Moabu na Amoni kwa sababu ya kiburi chao, tangu walipowadhihaki na kuwatukana watu wa Yahwe wa majeshi.
This shall they have for their pride, because they have taunted and spoken boastfully against the people of the LORD of hosts.
11 Ndipo watamwogopa Yahwe, kwa kuwa ataidhihaki miungu yote ya dunia. Kila mmoja atamwabudu yeye, kila mmoja kutoka mahali pake, kutoka kila upande wa pwani.
The LORD will be terrible unto them; for He will famish all the gods of the earth; then shall all the isles of the nations worship Him, every one from its place.
12 Ninyi Wakushi pia mtakufa kwa upanga wangu,
Ye Ethiopians also, ye shall be slain by My sword.
13 na mkono wa Mungu utaishambulia kaskazini na kuiangamiza Ashuru, Kwa hiyo Ninawi utatelekezwa kwa kuteketezwa, kuwa pakavu kama jangwa.
And He will stretch out His hand against the north, and destroy Assyria; and will make Nineveh a desolation, and dry like the wilderness.
14 Ndipo makundi ya wanyama yatalala pale, kila mnyama wa mataifa, wote kirukanjia na nungunungu watapumzika juu ya safu zao. Sauti itasikika kutoka madirishani; kifusi kitakuwa milangoni; nakshi za mwerezi wao mihimili itakuwa imeifunua.
And all beasts of every kind shall lie down in the midst of her in herds; both the pelican and the bittern shall lodge in the capitals thereof; voices shall sing in the windows; desolation shall be in the posts; for the cedar-work thereof shall be uncovered.
15 huu ni mji wa kushangiliwa ambao umekaa pasipo hofu, ambaye husema moyoni mwake, “Mimi niko, na hakuna mwingine wa kufanana na Mimi”. Kwa namna ulivyokuwa wa kutisha, mahali pa kulala wanyama ndani yake. Kila mmoja ambaye hupitia kwake huuhisia na kutingisha ngumi kwake.
This is the joyous city that dwelt without care, that said in her heart: 'I am, and there is none else beside me'; how is she become a desolation, a place for beasts to lie down in! Every one that passeth by her shall hiss, and wag his hand.

< Sefania 2 >