< Sefania 2 >

1 Kusanyikeni pamoja ninyi wenyewe mkutano wa hadhara na kusanyikeni, taifa lisilokuwa na aibu -
Be ashamed within yourselves, be ashamed,
2 kabla amri kuchukua madhara na siku hiyo kupita kama makapi, kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahwe kuja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana kuja juu yenu.
before you become as the drifting chaff, before the anger of the Lord comes upon you, before the day of the Lord’s wrath comes upon you.
3 Mtafuteni Yahwe, ninyi watu wote wanyenyekevu duniani mnaozitii amri zake! Tafuteni haki yake. Tafuteni unyenyekevu, na labda mtalindwa katika siku ya ghadhabu ya Yahwe.
Seek the Lord all you meek of the earth, you who obey his law; Seek righteousness, seek meekness; perhaps you may be hidden in the day of the Lord’s wrath.
4 hivyo Gaza utatelekezwa, na Ashkeloni utageuka kuwa uharibifu. Watauondoshea mbali Ashdodi wakati wa mchana, na wataung'oa Ekroni!
For Gaza will be forsaken; Ashkelon a desolation; Ashdod – by noon will they rout her and Ekron be torn up!
5 Ole kwa wanaokaa kando ya bahari, taifa la Wakerethi! Yahwe amesema dhidi yenu, Kanaani, nchi ya Wafilisiti. Nitawaangamiza hakuna mkazi atakayebakia.
Woe to those who live by the sea coast, people of the Cherethites! The word of the Lord is against you, Canaan, land of the Philistines! I will destroy you so that you will be without inhabitants,
6 Hiyo nchi ya kando ya bahari itakuwa malisho kwa wachungaji na kwa mazizi ya kondoo.
and you will become shepherds’ cots and folds for flocks.
7 Nchi ya kando ya bahari itakuwa mali ya mabaki ya watu wa nyumba ya Yuda, watakaochungia makundi yao huko. Watu wao watalala jioni katika nyumba ya Ashikeloni, kwa kuwa Yahwe Mungu wao atawatunza na kurejesha wafungwa wao.
The sea coast will belong to the survivors of the house of Judah. They will pasture their flocks there. In the house of Ashkelon they will lie down at evening. The Lord their God will be with them and restore their fortunes.
8 Nilizisikia dhihaka za Moabu na wakiwatukana watu wa Amoni wakati walipowadhihaki watu wangu na kujitukuza mipakani mwao.
I have heard the taunts of Moab, and the revilings of the Ammonites, how they have taunted my people, and spoken boastfully concerning their border.
9 Kwa hiyo, kama ninavyoishi - hili ni tamko la Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, - Moabu itakuja kuwa kama Sodoma, na watu wa Amoni kama Gomora; mahali pa viwavi na shimo la chumvi, jangwa la daima. Lakini watu wangu waliosalia watawateka mateka, na watu wa taifa langu waliobaki watachukua umiliki wao.'
Therefore as I live, says the Lord of hosts, the God of Israel: Moab will be like Sodom, and the Ammonites like Gomorrah, a pile of nettles and saltpits, and a desolation, forever. The residue of my people will plunder them, and the survivors of my nation will inherit them.
10 Hili litatokea kwa Moabu na Amoni kwa sababu ya kiburi chao, tangu walipowadhihaki na kuwatukana watu wa Yahwe wa majeshi.
This will they have for their pride, because they have taunted and spoken boastfully against the people of the Lord of hosts.
11 Ndipo watamwogopa Yahwe, kwa kuwa ataidhihaki miungu yote ya dunia. Kila mmoja atamwabudu yeye, kila mmoja kutoka mahali pake, kutoka kila upande wa pwani.
The Lord will terrify them; he will reduce all the gods of the earth; then all the peoples of the nations will worship him, each in their own land.
12 Ninyi Wakushi pia mtakufa kwa upanga wangu,
You, also, Ethiopians, slain by his sword are you!
13 na mkono wa Mungu utaishambulia kaskazini na kuiangamiza Ashuru, Kwa hiyo Ninawi utatelekezwa kwa kuteketezwa, kuwa pakavu kama jangwa.
And he will stretch out his hand against the north and destroy Assyria; And he will make Nineveh a desolation, dry as the wilderness.
14 Ndipo makundi ya wanyama yatalala pale, kila mnyama wa mataifa, wote kirukanjia na nungunungu watapumzika juu ya safu zao. Sauti itasikika kutoka madirishani; kifusi kitakuwa milangoni; nakshi za mwerezi wao mihimili itakuwa imeifunua.
Herds will lie down in it, every beast of the earth, Desert owl and screech owl will lodge in its capitals. The owl will hoot in the window, the raven on the doorstep, all stripped bare of cedar.
15 huu ni mji wa kushangiliwa ambao umekaa pasipo hofu, ambaye husema moyoni mwake, “Mimi niko, na hakuna mwingine wa kufanana na Mimi”. Kwa namna ulivyokuwa wa kutisha, mahali pa kulala wanyama ndani yake. Kila mmoja ambaye hupitia kwake huuhisia na kutingisha ngumi kwake.
This is the exultant city which sat secure. The city who said to herself, I am and there is none else! How has she become a desolation! A lair of beasts! Every passerby hisses at her, shakes their hand.

< Sefania 2 >