< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, neno la Yahwe lilimjia nabii Zekaria, mwana wa Berekia mwana wa Ido, kusema,
IN THE eighth month, in the second year of Darius, came the word of the LORD unto Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying:
2 “Yawhe alikuwa na hasira sana juu ya baba zenu!
'The LORD hath been sore displeased with your fathers.
3 Wambie, 'Yahwe wa majeshi asema hivi: Nirudieni! - nami nitawarudia ninyi, asema Yahwe wa majeshi.
Therefore say thou unto them, Thus saith the LORD of hosts: Return unto Me, saith the LORD of hosts, and I will return unto you, saith the LORD of hosts.
4 Msiwe kama baba zenu ambao hapo zamani manabii waliwambia, wakisema, “Yahwe wa majeshi asema hivi: Geukeni kutoka katika njia zenu za mbaya na matendo yenu mabaya!” Lakini hawakuweza kusikia wala kunijari - asema Yahwe.'
Be ye not as your fathers, unto whom the former prophets proclaimed, saying: Thus saith the LORD of hosts: Return ye now from your evil ways, and from your evil doings; but they did not hear, nor attend unto Me, saith the LORD.
5 Wako wapi baba zenu? Na manabii, je wapo hapa daima?
Your fathers, where are they? and the prophets, do they live for ever?
6 Lakini maneno yangu na maagizo niliyowaamru watumishi wangu manabii, je hayakuwapata baba zenu? Hivyo walitubu na kusema, 'Kama vile Yahwe wa majeshi alivyokusudia kututenda kwa kadili zinavyostahili njia na matendo yetu, ndivyo alivyotutenda.”
But My words and My statutes, which I commanded My servants the prophets, did they not overtake your fathers? so that they turned and said: Like as the LORD of hosts purposed to do unto us, according to our ways, and according to our doings, so hath He dealt with us.'
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, ndiyo mwezi wa Shebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yahwe lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido, akasema,
Upon the four and twentieth day of the eleventh month, which is the month Shebat, in the second year of Darius, came the word of the LORD unto Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying —
8 “niliona wakati wa usiku, na tazama! mtu alikuwa amepanda farasi mwekundu, naye alikuwa kati ya miti ya mihadasi iliyoko bondeni; na nyuma yake kulikuwa na farasi mwekundu, farasi wa kijivu, na farasi mweupe.”
I saw in the night, and behold a man riding upon a red horse, and he stood among the myrtle-trees that were in the bottom; and behind him there were horses, red, sorrel, and white.
9 Nikauliza, “Bwana, hivi ni vitu gani?” Malaika aliyesema nami akaniambia, “Nitakueleza vitu hivi ni nini.”
Then said I: 'O my lord, what are these?' And the angel that spoke with me said unto me: 'I will show thee what these are.'
10 Kisha mtu aliyesimama kati ya miti ya mihadasi akajibu na kusema, “Hawa ndiyo Yahwe aliowatuma kuzunguka katika dunia yote.”
And the man that stood among the myrtle-trees answered and said: 'These are they whom the LORD hath sent to walk to and fro through the earth.'
11 Wakamjibu malaika wa Yahwe aliyekuwa amesimama kati ya miti ya mihadasi na kumwambia, “Tumekuwa tukizunguka duniani pote; tazama, dunia yote imekaa na kutulia.”
And they answered the angel of the LORD that stood among the myrtle-trees, and said: 'We have walked to and fro through the earth, and, behold, all the earth sitteth still, and is at rest.'
12 Ndipo malaika wa Yahwe alipojibu na kusema, “Yahwe wa majeshi, hata lini usiuhurumie Yerusalemu na miji ya Yuda ambayo imeteswa na kudhurumiwa miaka hii sabini?”
Then the angel of the LORD spoke and said: 'O LORD of hosts, how long wilt Thou not have compassion on Jerusalem and on the cities of Judah, against which Thou hast had indignation these threescore and ten years?
13 Yahwe akamjibu malaika aliyekuwa amesema nami, kwa maneno mazuri, maneno ya faraja.
And the LORD answered the angel that spoke with me with good words, even comforting words —
14 Hivyo malaika aliyekuwa anaongea nami akaniambia, “Ita kwa sauti na useme 'Yahwe wa majeshi asema: Nina wivu kwa ajili ya Yerusalemu yaani Sayuni kwa uchungu mkubwa!
so the angel that spoke with me said unto me: 'Proclaim thou, saying: Thus saith the LORD of hosts: I am jealous for Jerusalem and for Zion with a great jealousy;
15 Nami nina hasira juu ya mataifa yaliyo na utulivu. Kwa maana nilikasirika kidogo tu, lakini wao wakasababisha madhara mabaya.
and I am very sore displeased with the nations that are at ease; for I was but a little displeased, and they helped for evil.
16 Kwa hiyo Yahwe wa majeshi asema hivi: Nimeirudia Yerusalema kwa huruma. Hivyo nyumba yangu itajengwa ndani yake - asema Yahwe wa majeshi. Kipimo kitanyoshwa juu ya Yerusalemu!
Therefore thus saith the LORD: I return to Jerusalem with compassions: My house shall be built in it, saith the LORD of hosts, and a line shall be stretched forth over Jerusalem.
17 Ita tena, ukisema, 'Yahwe wa majeshi asema hivi: Miji yangu kwa mara nyingine itajawa na uzuri, na Yahwe ataifariji tena Sayuni, na kuichagua Yerusalemu kwa mara nyingine tena.”
Again, proclaim, saying: Thus saith the LORD of hosts: My cities shall again overflow with prosperity; and the LORD shall yet comfort Zion, and shall yet choose Jerusalem.'
18 Kisha nikainua macho na kuona pembe nne!
And I lifted up mine eyes, and saw, and behold four horns.
19 Nikaongea na malaika aliyesema nami, “Hivi ni vitu gani? Akanijibu “hizi ni pembe zilisosababisha kutawanyika kwa Yuda, Israeli, na Yerusalemu.”
And I said unto the angel that spoke with me: 'What are these?' And he said unto me: 'These are the horns which have scattered Judah, Israel, and Jerusalem.'
20 Kisha Yahwe akanionesha mafundi stadi wanne.
And the LORD showed me four craftsmen.
21 Nikasema, “Watu hawa wanakuja kufanya nini?” Akajibu na kusema, “Hizi ni pembe zililoitawanya Yuda na hakuna mtu angeweza kuinua kichwa chake. Lakini watu hawa wanakuja kuziondoa, kutupa chini pembe za mataifa yaliyoinua nguvu zao kinyume cha nchi ya Yuda na kuisambaza.”
Then said I: 'What come these to do?' And he spoke, saying: 'These — the horns which scattered Judah, so that no man did lift up his head — these then are come to frighten them, to cast down the horns of the nations, which lifted up their horn against the land of Judah to scatter it.'

< Zekaria 1 >