< Warumi 9 >

1 Nasema ukweli katika Kristo. Sisemi uongo, na dhamira yangu hushuhudia pamoja nami katika Roho Mtakatifu,
Je dis la vérité en Christ. Je ne mens pas, ma conscience m'attestant par le Saint-Esprit
2 kwamba kuna huzuni kubwa na maumivu yasiyo koma ndani ya moyo wangu.
que j'ai dans le cœur une grande tristesse et une douleur incessante.
3 Kwamba ningetamani mimi mwenyewe kulaaniwa na kutengwa mbali na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, wale wa jamii yangu katika mwili.
Car je voudrais être moi-même maudit du Christ à cause de mes frères, mes parents selon la chair
4 Wao ni Waisraeli. Walio na hali ya kufanyika watoto, wa utukufu, wa maagano, na zawadi ya sheria, kumwabudu Mungu, na ahadi.
qui sont Israélites; à qui appartiennent l'adoption, la gloire, les alliances, le don de la loi, le service et les promesses;
5 Wao ni watangulizi ambako Kristo amekuja kwa heshima kuvaa mwili huu - ambaye yeye ni Mungu wa vyote. Naye asifiwe milele. Amina. (aiōn g165)
dont sont les pères, et dont est issu le Christ selon la chair, qui est au-dessus de tout, Dieu, béni éternellement. Amen. (aiōn g165)
6 Lakini si kwamba ahadi za Mungu zimeshindwa kutimia. Maana si kila mtu aliye Israeli ni Mwiisraeli halisi.
Mais ce n'est pas comme si la parole de Dieu était restée sans effet. Car ce n'est pas tout Israël qui est d'Israël.
7 Sivyo hata kwa uzao wa Abrahamu kuwa ni watoto wake halisi. Lakini, “ni kupitia Isaka uzao wako utaitwa.”
Ils ne sont pas non plus tous des enfants, puisqu'ils sont la descendance d'Abraham. Mais « votre descendance sera comptée comme celle d'Isaac ».
8 Hii ni kwamba, watoto wa mwili si watoto wa Mungu. Lakini watoto wa ahadi wanatazamwa kuwa kama uzao.
C'est-à-dire que ce ne sont pas les enfants de la chair qui sont enfants de Dieu, mais les enfants de la promesse qui sont comptés comme héritiers.
9 Maana hili ndilo neno la ahadi: “Katika majira haya nitakuja, na Sara atapewa mtoto.”
Car voici la parole de la promesse: « Au temps fixé, je viendrai, et Sara aura un fils. »
10 Si hili tu, lakini baada ya Rebeka kupata mimba kwa mtu mmoja, Isaka baba yetu-
Non seulement cela, mais Rebecca aussi a conçu par un seul, par notre père Isaac.
11 kwamba watoto walikuwa bado hawajazaliwa na alikuwa hajafanya jambo lolote zuri au baya, ili kwamba kusudi la Mungu kulingana na uchaguzi lisimame, wala si kwa matendo, lakini ni kwa sababu ya yule aitae.
Car, n'étant pas encore née, et n'ayant rien fait de bon ni de mauvais, afin que subsiste le dessein de Dieu selon l'élection, non des œuvres, mais de celui qui appelle,
12 Ilinenwa kwake, “Mkubwa atamtumikia mdogo.”
il lui fut dit: « L'aîné servira le cadet. »
13 Kama ilivyo kwisha andikwa: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
Selon qu'il est écrit: « J'ai aimé Jacob, mais j'ai haï Ésaü. »
14 Basi tena tutasema nini? Je kuna udhalimu kwa Mungu? La hasha.
Que dirons-nous donc? Y a-t-il de l'injustice devant Dieu? Qu'il n'y en ait jamais!
15 Kwa kuwa anasema kwa Musa, “nitakuwa na rehema kwa yule nitakayemrehemu, na nitakuwa na huruma kwa yule nitakayemhurumia.”
Car il a dit à Moïse: « J'aurai pitié de qui j'aurai pitié, et j'aurai compassion de qui j'aurai compassion. »
16 Kwa hiyo basi, si kwa sababu ya yeye atakaye, wala si kwa sababu ya yeye ambaye hukimbia, lakini kwa sababu ya Mungu, ambaye huonesha rehema.
Ainsi donc, ce n'est pas à celui qui veut, ni à celui qui court, mais à Dieu qui fait miséricorde.
17 Kwa kuwa maandiko husema kwa Farao, “Kwa kusudi hili maalumu nilikuinua, ili kwamba nioneshe nguvu zangu katika wewe, na ili kwamba jina langu litangazwe katika nchi yote.”
Car l'Écriture dit à Pharaon: « C'est dans ce but que je t'ai suscité, afin de montrer en toi ma puissance et de proclamer mon nom par toute la terre. »
18 Hivyo basi, Mungu huwa na rehema kwa yeyote ampendaye, na kwa ambaye humpenda, humfanya kuwa mkaidi.
Ainsi donc, il fait miséricorde à qui il veut, et il endurcit qui il veut.
19 Kisha utasema kwangu, “Kwa nini bado anaona kosa? Ni yupi ambaye alikwisha kustahimili matakwa yake?”
Vous me direz alors: « Pourquoi trouve-t-il encore à redire? Car qui résiste à sa volonté? »
20 Kinyume chake, mwanadamu, wewe ni nani ujibue kinyume na Mungu? Kuna uwezekano wowote wa kilichofinyangwa kusema kwa mfinyanzi, “Kwanini ulinifanya hivi mimi?”
Mais en vérité, ô homme, qui es-tu pour répondre contre Dieu? La chose formée demandera-t-elle à celui qui l'a formée: « Pourquoi m'as-tu fait ainsi? ».
21 Je mfinyazi huwa hana haki juu ya udongo kutengeneza chombo kwa matumizi maalumu kutokana na bonge lile lile, na chombo kingine kwa matumizi ya kila siku?
Ou bien le potier n'a-t-il pas un droit sur l'argile, à partir de la même masse, pour faire d'une partie un vase pour l'honneur, et d'une autre pour le déshonneur?
22 Vipi kama Mungu, ambaye ana utayari wa kuonesha gadhabu yake na kufanya nguvu yake kujulikana, alistahimili kwa uvumilivu wa kutosha vyombo vya gadhabu vilivyoandaliwa kwa kuangamiza?
Et si Dieu, voulant montrer sa colère et faire connaître sa puissance, a supporté avec beaucoup de patience des vases de colère préparés pour la destruction,
23 Vipi kama alifanya hivi ili kwamba aoneshe wingi wa utukufu wake juu ya vyombo vya rehema, ambavyo alikwisha kuviandaa kwa ajili ya utukufu?
et qu'il a voulu faire connaître les richesses de sa gloire sur des vases de miséricorde, qu'il a préparés d'avance pour la gloire -
24 Vipi kama alifanya hii pia kwetu, ambaye pia alituita, si tu kutoka kwa Wayahudi, lakini pia kutoka kwa watu wa Mataifa?
nous, qu'il a aussi appelés, non seulement des Juifs, mais aussi des païens?
25 Kama asemavyo pia katika Hosea: “Nitawaita watu wangu ambao hawakuwa watu wangu, na mpendwa wake ambaye hakupendwa.
Comme il le dit aussi dans Osée, « Je les appellerai 'mon peuple', eux qui n'étaient pas mon peuple; et sa « bien-aimée », qui n'était pas bien-aimée. »
26 Na itakuwa kwamba pale iliposemwa kwao, 'Ninyi si watu wangu,' pale wataitwa 'wana wa Mungu aliye hai.”'
« Dans le lieu où il leur a été dit: « Vous n'êtes pas mon peuple ». ils seront appelés « enfants du Dieu vivant ». »
27 Isaya analia kuhusiana na Israeli, “Kama hesabu ya wana wa Israeli ingekuwa kama mchanga wa bahari, itakuwa ni masalia ambao wataokolewa.
Ésaïe crie à propos d'Israël, « Si le nombre des enfants d'Israël est comme le sable de la mer, c'est le reste qui sera sauvé;
28 Kwa kuwa Bwana atalichukua neno lake juu ya nchi, mapema na kwa utimilifu.
car il achèvera l'œuvre et la coupera dans la justice, parce que l'Éternel fera une courte œuvre sur la terre. »
29 Na kama jinsi Isaya alivyosema awali, “Kama Bwana wa majeshi hakutuachia nyuma uzao kwa ajili yetu, tungekuwa kama Sodoma, na tungefanywa kama Gomora.
Comme l'a déjà dit Ésaïe, « A moins que le Seigneur des Armées ne nous ait laissé une graine, nous serions devenus comme Sodome, et aurait été rendu comme Gomorrah. »
30 Tutasema nini basi? kwamba watu wa Mataifa ambao walikuwa hawatafuti haki, walipata haki, haki kwa imani.
Que dirons-nous donc? Que les païens, qui ne cherchaient pas la justice, sont parvenus à la justice, à la justice de la foi;
31 Lakini Israeli, ambaye alitafuta sheria ya haki, hakuifikia.
mais qu'Israël, qui cherchait une loi de justice, n'est pas parvenu à la loi de justice.
32 Kwanini si hivyo? Kwa sababu hawakuitafuta kwa imani, bali kwa matendo. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa,
Pourquoi? Parce qu'ils ne l'ont pas cherchée par la foi, mais pour ainsi dire par les œuvres de la loi. Ils ont trébuché sur la pierre d'achoppement,
33 kama ilivyo kwisha andikwa, “Tazama, nimelaza jiwe la kujikwaa katika Sayuni na mwamba wa kukosa. Yeye ambaye huamini katika hili hataaibika.”
selon qu'il est écrit, « Voici que je pose en Sion une pierre d'achoppement et un rocher de scandale; et aucun de ceux qui croient en lui ne sera déçu. »

< Warumi 9 >