< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
Je vous exhorte donc, frères, par la miséricorde de Dieu, à offrir votre corps en sacrifice vivant, saint, agréable à Dieu, ce qui est votre service spirituel.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
Ne vous conformez pas au monde présent, mais soyez transformés par le renouvellement de votre intelligence, afin que vous discerniez quelle est la volonté de Dieu, ce qui est bon, agréable et parfait. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
Car je dis, par la grâce qui m'a été donnée, à tous ceux qui sont parmi vous, de ne pas avoir de vous-mêmes une opinion trop élevée, mais de penser raisonnablement, selon que Dieu a donné à chacun une mesure de foi.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
Car, de même que nous avons plusieurs membres dans un seul corps, et que tous les membres n'ont pas la même fonction,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
ainsi, nous qui sommes plusieurs, nous formons un seul corps en Christ, et nous sommes tous membres les uns des autres,
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
ayant des dons différents selon la grâce qui nous a été accordée: Si nous prophétisons, prophétisons selon la mesure de notre foi;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
si nous servons, donnons-nous au service; si nous enseignons, donnons-nous à l'enseignement;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
si nous exhortons, donnons-nous à l'exhortation; si nous donnons, faisons-le avec générosité; si nous gouvernons, faisons-le avec diligence; si nous faisons preuve de miséricorde, faisons-le avec joie.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Que l'amour soit sans hypocrisie. Ayez en horreur ce qui est mauvais. Attachez-vous à ce qui est bon.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
Dans l'amour des frères, ayez les uns pour les autres une tendre affection; dans l'honneur, préférez-vous les uns aux autres,
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
ne tardez pas à vous appliquer, avec un esprit fervent, à servir le Seigneur,
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
réjouissez-vous dans l'espérance, supportez les tribulations, persévérez dans la prière,
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
contribuez aux besoins des saints, et donnez l'hospitalité.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Bénissez ceux qui vous persécutent; bénissez, et ne maudissez pas.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Réjouissez-vous avec ceux qui se réjouissent. Pleurez avec ceux qui pleurent.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Ayez les mêmes sentiments les uns envers les autres. N'ayez pas la prétention de vous élever, mais associez-vous aux humbles. Ne sois pas sage dans tes propres idées.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Ne rends à personne le mal pour le mal. Respecte ce qui est honorable aux yeux de tous les hommes.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
Si cela est possible, autant que cela dépend de toi, sois en paix avec tous les hommes.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Ne cherchez pas vous-mêmes à vous venger, bien-aimés, mais laissez agir la colère de Dieu. Car il est écrit: « A moi la vengeance, à moi la rétribution, dit le Seigneur. »
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
C'est pourquoi « Si ton ennemi a faim, donne-lui à manger. S'il a soif, donnez-lui à boire; car en faisant cela, tu amasseras des charbons ardents sur sa tête. »
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Ne vous laissez pas vaincre par le mal, mais vainquez le mal par le bien.

< Warumi 12 >