< Ufunuo 8 >

1 Wakati Mwanakondoo alipofungua muhuri ya saba, kukawa na ukimya mbinguni takribani nusu saa.
Lorsqu'il ouvrit le septième sceau, il y eut un silence dans le ciel pendant environ une demi-heure.
2 Kisha nikaona malaika saba wasimamao mbele za Mungu, na wakapewa tarumbeta saba.
Je vis les sept anges qui se tiennent devant Dieu, et sept trompettes leur furent données.
3 Malaika mwingine akaja, ameshikilia bakuli ya dhahabu yenye uvumba, amesimama madhabahuni. Akapewa uvumba mwingi ili kwamba autoe pamoja na maombi ya waamini wote katika madhabahu ya dhahabu mbele ya kiti cha enzi.
Un autre ange vint et se tint au-dessus de l'autel, ayant un encensoir d'or. On lui donna beaucoup de parfums, afin qu'il les ajoute aux prières de tous les saints sur l'autel d'or qui était devant le trône.
4 Moshi wa ule uvumba, pamoja na maombi ya waamini, ukapanda juu mbele za Mungu kutoka mkononi mwa malaika.
La fumée des parfums, avec les prières des saints, montait devant Dieu de la main de l'ange.
5 Malaika akatwaa bakuli la uvumba na akalijaza moto kutoka kwenye madhabahu. Kisha akalitupa chini juu ya nchi, na kukatokea sauti za radi, miale ya radi na tetemeko la nchi.
L'ange prit l'encensoir, le remplit du feu de l'autel, puis le jeta sur la terre. Des tonnerres, des sons, des éclairs et un tremblement de terre suivirent.
6 Wale malaika saba ambao walikuwa na tarumbeta saba wakawa tayari kuzipiga.
Les sept anges qui tenaient les sept trompettes se préparèrent à en sonner.
7 Malaika wa kwanza akaipiga tarumbeta yake, na kukatokea mvua ya mawe na moto uliochanganyikana na damu. Vikatupwa chini katika nchi ili kwamba theluthi yake iungue, theluthi ya miti ikaungua na nyasi zote za kijani zikaungua.
Le premier coup sonna, et il s'ensuivit de la grêle et du feu, mêlés de sang, qui furent jetés sur la terre. Un tiers de la terre fut brûlé, un tiers des arbres fut brûlé, et toute herbe verte fut brûlée.
8 Malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake, na kitu kama mlima mkubwa uliokuwa unaungua kwa moto ukatupwa baharini. Theluthi ya bahari ikawa damu,
Le second ange sonna de la trompette, et quelque chose comme une grande montagne embrasée fut jeté dans la mer. Un tiers de la mer devint du sang,
9 theluthi ya viumbe hai katika bahari vikafa, na theluthi ya meli zikaharibiwa.
et un tiers des êtres vivants qui étaient dans la mer moururent. Le tiers des navires fut détruit.
10 Malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake, na nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, ikimulika kama kurunzi, juu ya theluthi ya mito na chemichemi za maji.
Le troisième ange sonna de la trompette, et il tomba du ciel une grande étoile, ardente comme une torche, qui tomba sur le tiers des fleuves et sur les sources d'eau.
11 Jina la nyota ni pakanga. Theluthi ya maji ikawa pakanga, na watu wengi wakafa kutokana na maji yaliyokuwa machungu.
Le nom de l'étoile est « Absinthe ». Un tiers des eaux devint de l'absinthe. Beaucoup de gens moururent à cause de ces eaux, parce qu'elles étaient devenues amères.
12 Malaika wa nne alipiga tarumbeta yake, na theluthi ya jua ikapigwa, pamoja na theluthi ya mwezi na theluthi ya nyota. Kwa hiyo theluthi ya vyote ikageuka kuwa giza; theluthi ya mchana na theluthi ya usiku havikuwa na mwanga.
Le quatrième ange sonna de la trompette. Le tiers du soleil fut frappé, ainsi que le tiers de la lune et le tiers des étoiles, de sorte qu'un tiers d'entre eux fut obscurci; le jour ne brillerait pas pour un tiers, et la nuit de même.
13 Nilitazama, na nikasikia tai aliye kuwa anaruka katikati ya anga, akiita kwa sauti kuu, “Ole, ole, ole, kwa wale wakaao katika nchi, kwa sababu ya mlipuko wa tarumbeta iliyosalia ambayo imekaribia kupigwa na malaika watatu.”
Je vis et j'entendis un aigle qui volait au milieu du ciel et qui disait d'une voix forte: « Malheur! Malheur! Malheur aux habitants de la terre, à cause des autres sonneries des trompettes des trois anges, qui doivent encore retentir! ».

< Ufunuo 8 >