< Ufunuo 6 >

1 Nikatazama wakati mwanakondoo alipofungua moja ya zile muhuri saba, nikasikia mmoja wa wale wenye uhai wanne akisema kwa sauti iliyofanana na radi, “Njoo!”
Je vis que l'agneau ouvrait l'un des sept sceaux, et j'entendis l'un des quatre êtres vivants qui disait, comme d'une voix de tonnerre: « Viens et vois! »
2 Nikatazama na palikuwa na farasi mweupe! Aliyempanda alikuwa na bakuli, na akapewa taji. Alitokea kama mshindi ashindaye ili ashinde.
Alors apparut un cheval blanc, et celui qui le montait tenait un arc. Une couronne lui fut donnée, et il sortit en vainqueur, et pour vaincre.
3 Wakati mwanakondoo alipofungua muhuri wa pili, nikasikia mwenye uhai wa pili akisema, “Njoo!”
Quand il ouvrit le second sceau, j'entendis le second être vivant qui disait: « Viens! »
4 Kisha farasi mwingine akatokea - mwekundu kama moto. Aliye mpanda alipewa ruhusa ya kuondoa amani duniani, ili kwamba watu wachinjane. Huyu aliye mpanda alipewa upanga mkubwa.
Un autre sortit, un cheval roux. A celui qui le montait fut donné le pouvoir d'enlever la paix de la terre, et de faire en sorte que les hommes s'entretuent. Une grande épée lui fut donnée.
5 Wakati mwanakondoo alipofungua ule muhuri wa tatu, nikasikia mwenye uhai wa tatu akisema, “Njoo!” Nikaona farasi mweusi, na aliyempanda ana mizani mkononi mwake.
Quand il ouvrit le troisième sceau, j'entendis le troisième être vivant qui disait: « Viens et vois! » Et voici, il y avait un cheval noir, et celui qui le montait tenait une balance dans sa main.
6 Nikasikia sauti iliyoonekana kuwa ya mmoja wa wale wenye uhai ikisema, “kibaba cha ngano kwa dinari moja na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja. Lakini usiyadhuru mafuta na divai.”
J'entendis une voix au milieu des quatre êtres vivants qui disait: « Un chœnix de blé pour un denier, et trois chœnix d'orge pour un denier! N'abîmez pas l'huile et le vin! »
7 Wakati mwanakondoo alipofungua muhuri ya nne, nilisikia sauti ya mwenye uhai wa nne ikisema, “Njoo!”
Quand il ouvrit le quatrième sceau, j'entendis le quatrième être vivant qui disait: « Viens et vois! »
8 Kisha nikaona farasi wa kijivu. Aliye mpanda aliitwa jina lake mauti, na kuzimu ilikuwa ikimfuata. Walipewa mamlaka juu ya robo ya nchi, kuua kwa upanga, kwa njaa na kwa ugonjwa, na kwa wanyama wa mwitu katika nchi. (Hadēs g86)
Et voici, il y avait un cheval pâle, et le nom de celui qui le montait était la mort. L'Hadès le suivait. Il lui fut donné autorité sur le quart de la terre, pour tuer par l'épée, par la famine, par la mort, et par les bêtes sauvages de la terre. (Hadēs g86)
9 Wakati mwanakondoo alipofungua muhuri ya tano, niliona chini ya madhabahu roho za wale waliokuwa wameuawa kwa sababu ya neno la Mungu na kutokana na ushuhuda walioushika kwa uthabiti.
Quand il ouvrit le cinquième sceau, je vis sous l'autel les âmes de ceux qui avaient été tués à cause de la Parole de Dieu et du témoignage de l'Agneau qu'ils avaient.
10 Wakalia kwa sauti kuu, “mpaka lini, Mtawala wa vyote, mtakatifu na mkweli, utahukumu wakaao juu ya nchi, na kulipiza kisasi damu yetu?”
Ils criaient d'une voix forte, en disant: « Jusques à quand, Maître, le saint et le vrai, jugeras-tu et vengeras-tu notre sang sur les habitants de la terre? »
11 Kisha kila mmoja alipewa kanzu nyeupe na wakaambiwa kuwa wanapaswa kusubiri kidogo hata itakapotimia hesabu kamili ya watumishi wenzao na ndugu zao wa kike na wa kiume itakapotimia ambao watauawa, kama vile ambavyo wao waliuawa.
On donna à chacun d'eux une longue robe blanche. On leur dit qu'ils devaient se reposer encore quelque temps, jusqu'à ce que leurs compagnons de service et leurs frères, qui seraient aussi tués comme eux, aient achevé leur course.
12 Wakati mwanakondoo alipofungua muhuri ya sita, nilitazama na palikuwa na tetemeko kuu. Jua likawa jeusi kama gunia la singa, na mwezi mzima ukawa kama damu.
Je vis, quand il ouvrit le sixième sceau, qu'il y eut un grand tremblement de terre. Le soleil devint noir comme un sac de crin, et la lune entière devint comme du sang.
13 Nyota za mbinguni zikaanguka katika nchi, kama mtini upukutishavyo matunda yake ya wakati wa baridi unapotikiswa na kimbunga.
Les étoiles du ciel tombèrent sur la terre, comme un figuier qui laisse tomber ses figues non mûres quand il est secoué par un grand vent.
14 Anga ilitoweka kama gombo lililoviringishwa. Kila mlima na kisiwa vilihamishwa mahali pake.
Le ciel fut enlevé comme un rouleau qu'on enroule. Toute montagne et toute île furent déplacées de leur place.
15 Kisha wafalme wa nchi na watu maarufu na majemadari, matajiri, wenye nguvu, na kila mmoja aliye mtumwa na huru, wakajificha katika mapango na katika miamba ya milima.
Les rois de la terre, les princes, les chefs militaires, les riches, les forts, tous les esclaves et les hommes libres, se cachèrent dans les cavernes et dans les rochers des montagnes.
16 Wakaiambia milima na miamba, “Tuangukieni! Tuficheni dhidi ya uso wake aketiye kwenye kiti cha enzi na kutoka hasira ya mwanakondoo.
Et ils disaient aux montagnes et aux rochers: « Tombez sur nous, et cachez-nous devant la face de celui qui est assis sur le trône, et devant la colère de l'agneau,
17 Kwa kuwa siku kuu ya gadhabu yao imewadia, na ni nani awezaye kusimama?”
car le grand jour de sa colère est venu, et qui peut subsister? ».

< Ufunuo 6 >