< Ufunuo 21 >

1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa kuwa mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza zimekwishapita, na bahari haikuwepo tena.
И видях ново небе и нова земя; защото първото небе и първата земя преминаха; и море нямаше вече.
2 Niliona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ambao ulikuja chini kutoka mbinguni kwa Mungu, ulioandaliwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
Видях и светия град, новия Ерусалим, да слиза из небето от Бога, приготвен като невеста украсена за мъжа си.
3 Nilisikia sauti kubwa kutoka kwenye kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Makao ya Mungu yapo pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao. Watakuwa watu wake, na Mungu mwenyewe atakuwa nao na atakuwa Mungu wao.
И чух силен глас от престола, който казваше: Ето, скинията на Бога е с човеците; Той ще обитава с тях; те ще бъдат Негови люде; и сам Бог, техен Бог, ще бъде с тях.
4 Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na hapatakuwa na kifo tena, au kuomboleza, au kulia, au maumivu. Mambo ya zamani yamekwishakupita.
Той ще обърше всяка сълза от очите им, и смърт не ще има вече; нито ще има вече жалеене, ни плач, ни болка; първото премина.
5 Yeye ambaye alikuwa ameketi juu ya kiti cha enzi alisema, “Tazama! Nafanya mambo yote kuwa mapya.” Alisema, “Andika hili kwa sababu maneno haya ni ya hakika na kweli.”
И Седещият на престола рече: Ето, подновявам всичко. И каза: Напиши, защото тия думи са верни и истинни.
6 Aliniambia, “Mambo haya yalikwisha kupita! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Kwa yeyote aonaye kiu nitampatia kinywaji bila gharama kutoka katika chemchemi za maji ya uzima.
И рече ми: Сбъднаха се. Аз съм Алфа и Омега, началото и краят. На жадния ще дам даром от извора на водата на живота.
7 Yeye ashindaye atayarithi mambo haya, na nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
Който побеждава, ще наследи тия неща; Аз ще му бъда Бог, и той ще Ми бъде син.
8 Lakini kama ilivyo kwa waoga, wasioamini, wachukizao, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, sehemu yao itakuwa katika ziwa la moto wa kiberiti uunguzao. Hiyo ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
А колкото за страхливите, невярващите, мръсните, убийците, блудните, чародейците, идолопоклонниците и всички лъжци, тяхната участ ще бъде в езерото, което гори с огън и жупел. Това е втората смърт. (Limnē Pyr g3041 g4442)
9 Mmoja wa malaika saba alikuja kwangu, mmoja ambaye alikuwa na mabakuli saba yaliyojaa mapigo saba ya mwisho na alisema, “Njoo hapa. Nitakuonesha bibi harusi, mke wa mwana kondoo.”
Тогава дойде един от седемте ангела, които бяха натоварени със седемте последни язви и държаха седемте чаши и ми проговори, казвайки: Дойди, ще ти покажа невестата, жената на Агнето.
10 Kisha alinichukua mbali katika Roho kwenye mlima mkubwa na mrefu na alinionesha mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka chini kutoka mbinguni kwa Mungu.
И отведе ме чрез Духа на една голяма и висока планина, и показа ми светия град, Ерусалим, който слизаше от небето от Бога,
11 Yerusalemu ulikuwa na utukufu wa Mungu, na uzuri wake ulikuwa kama kito cha thamani, kama jiwe la kioo safi la yaspi.
и имаше божествена слава като светеше, както свети някой много скъпоценен камък, като яспис, прозрачен като кристал.
12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye milango kumi na miwili, pamoja na malaika kumi na wawili milangoni. Juu ya milango palikuwa pameandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya wana wa Israeli.
Градът имаше голяма и висока стена, с дванадесет порти, и на портите дванадесет ангела, и надписани над портите имена, които са имената на дванадесетте племена на израилтяните:
13 Upande wa mashariki palikuwa na milango mitatu, upande wa kusini milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, na upande wa magharibi milango mitatu.
откъм изток три порти, откъм север три порти, откъм юг три порти и откъм запад три порти.
14 Kuta za mji zilikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake palikuwa na majina kumi na mawili ya mitume kumi na wawili wa Mwana Kondoo.
И градската стена имаше дванадесет основни камъка с дванадесет имена на тях, имената на дванадесетте апостоли на Агнето.
15 Mmoja aliyeongea nami alikuwa na kipimo cha fimbo iliyotengenezwa kwa dhahabu kwa ajili ya kupima mji, milango yake na kuta zake.
И тоя, който говореше с мене, имаше за мярка златна тръст, за да измери града, портите и стената му.
16 Mji uliwekwa ndani ya mraba; urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Alipima mji kwa kipimio cha fimbo, stadia 12, 000 kwa urefu (urefu wake, upana, na kimo vilifanana).
Градът беше четвъртит, с дължина равна на широчината му; и като измери града с тръстта, излезе дванадесет хиляди стадии. Дължината, широчината и височината му са еднакви.
17 Vilevile alipima ukuta wake, unene wake ulikuwa dhiraa 144 kwa vipimo vya kibinadamu (ambavyo pia ni vipimo vya malaika).
Измери и стената му, която излезе сто и четиридесет и четири лакти; а това беше човешка мярка, употребена от ангела.
18 Ukuta ulikuwa umejengwa kwa yaspi na mji wenye dhahabu safi, kama kioo safi.
Стената му беше оградена от яспис, а самият град от чисто злато, подобно на чисто стъкло.
19 Misingi ya ukuta ilikuwa imepambwa na kila aina ya jiwe la thamani. La kwanza lilikuwa yaspi, la pili lilikuwa yakuti samawi, la tatu lilikuwa kalkedon, la nne zumaridi,
Основните камъни на градските стени бяха украсени със всякакви скъпоценни камъни: първият основен камък беше яспис, вторият сапфир, третият халкидон, четвъртият смарагд,
20 la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolitho, la nane zabarajadi, la tisa yakuti ya manjano, la kumi krisopraso, la kumi na moja hiakintho, la kumi na mbili amethisto.
петият сардоникс, шестият сард, седмият хрисолит, осмият вирил, деветият топаз, десетият хрисопрас, единадесетият яцинт, дванадесетият аметист.
21 Milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili, kila mlango ulitengenezwa kutoka kwenye lulu moja. Mitaa ya mji ilikuwa dhahabu safi, ikionekana kama kioo safi.
И дванадесетте порти бяха дванадесет бисера; всяка порта бе от един бисер; и улицата на града беше от чисто злато, прозрачно като стъкло.
22 Sikuona hekalu lolote ndani ya mji, kwa kuwa Bwana Mungu, ambaye anatawala juu ya vyote, na Mwana Kondoo ni hekalu lake.
И храм не видях в него, защото неговият храм е Господ Бог Всемогъщият и Агнето.
23 Mji haukuhitaji jua au mwezi ili kungaza juu yake kwa sababu utukufu wa Mungu uliangaza juu yake, na taa yake ni Mwana Kondoo.
И градът нямаше нужда от слънце, нито от луна да го осветява, защото Божията слава го осветяваше, и неговото светило е Агнето.
24 Mataifa watatembea kwa mwanga wa mji huo. Wafalme wa dunia wataleta fahari zao ndani yake.
И народите ще ходят по неговата светлина: земните царе ще донасят в него своите славни неща.
25 Milango yake haitafungwa wakati wa mchana, na hapatakuwa na usiku pale.
Портите му не ще се затварят денем, (а нощ не ще има там); ( Гръцки: Защото)
26 Wataleta fahari na heshima ya mataifa ndani yake,
па и народите ще донасят в него славните си и ценни неща.
27 na hakuna kichafu kitakachoingia ndani yake. Wala yeyote ambaye afanyaye jambo lolote la aibu au udanganyifu hataingia, bali ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana Kondoo.
И в него никак няма да влезе нещо нечисто, нито оня, който върши мерзост и който лъже, а само записаните в книгата на живота на Агнето.

< Ufunuo 21 >