< Ufunuo 1 >

1 Huu ni ufunuo wa Yesu Kristo ambao Mungu alimpa ili kuwaonesha watumishi wake mambo ambayo lazima yatokee karibuni. Aliyafanya yajulikane kwa kumtuma malaika wake kwa mtumishi wake Yohana.
C'est ici la Révélation de Jésus-Christ, que Dieu lui a donnée pour montrer à ses serviteurs les choses qui doivent arriver bientôt, qu'il a envoyée et fait connaître par son ange à son serviteur Jean,
2 Yohana alitoa ushuhuda wa kila kitu alichoona kuhusiana na neno la Mungu na kwa ushuhuda uliotolewa kuhusu Yesu Kristo.
lequel a rendu témoignage à la parole de Dieu et au témoignage de Jésus-Christ, sur tout ce qu'il a vu.
3 Amebarikiwa yeye asomaye kwa sauti na wale wote wanaoyasikia maneno ya unabii huu na kutii kilichoandikwa humo, kwa sababu muda umekaribia.
Heureux celui qui lit et ceux qui entendent les paroles de la prophétie, et qui gardent les choses qui y sont écrites, car le temps est proche.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: neema iwe kwenu na amani kutoka kwake aliyepo, aliyekuwepo, na atakayekuja, na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
Jean, aux sept assemblées qui sont en Asie: Grâce et paix à vous de la part de Dieu, qui est, qui était et qui vient, et des sept Esprits qui sont devant son trône,
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mtawala wa wafalme wa dunia hii. Kwake yeye atupendaye na ametuweka huru kutoka katika dhambi zetu kwa damu yake,
et de la part de Jésus-Christ, le témoin fidèle, le premier-né d'entre les morts, et le chef des rois de la terre. À celui qui nous aime, qui nous a lavés de nos péchés par son sang -
6 ametufanya kuwa ufalme, makuhani wa Mungu na Baba yake - kwake kuwa utukufu na nguvu milele daima. Amina. (aiōn g165)
et qui a fait de nous un Royaume, des prêtres pour son Dieu et Père - à lui la gloire et la domination pour les siècles des siècles. Amen. (aiōn g165)
7 Tazama, anakuja na mawingu; kila jicho litamwona, pamoja na wote waliomchoma. Na kabila zote za dunia wataomboleza kwake. Ndiyo, Amina.
Voici, il vient sur les nuées, et tout œil le verra, même ceux qui l'ont percé. Toutes les tribus de la terre se lamenteront sur lui. Ainsi soit-il, Amen.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “Yeye aliyepo, na aliyekuwepo, na ambaye anakuja, Mwenye nguvu.”
« Je suis l'Alpha et l'Oméga, dit le Seigneur Dieu qui est, qui était et qui vient, le Tout-Puissant. »
9 Mimi, Yohana - ndugu yenu na mmoja anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu; nilikuwa katika kisiwa kiitwacho Patimo kwa sababu ya neno la Mungu na ushuhuda kuhusu Yesu.
Moi, Jean, votre frère et votre associé dans l'oppression, le Royaume et la persévérance en Jésus-Christ, j'étais sur l'île qu'on appelle Patmos, à cause de la Parole de Dieu et du témoignage de Jésus-Christ.
10 Nilikuwa katika Roho siku ya Bwana. Nilisikia nyuma yangu sauti ya juu kama ya tarumbeta,
J'étais en Esprit au jour du Seigneur, et j'entendis derrière moi une voix forte, comme une trompette
11 ikisema, “andika katika kitabu unayo yaona, na uyatume kwa makanisa saba, kwenda Efeso, kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia.”
qui disait: « Ce que tu vois, écris-le dans un livre et envoie-le aux sept assemblées: à Éphèse, à Smyrne, à Pergame, à Thyatire, à Sardes, à Philadelphie et à Laodicée. »
12 Nikageuka kuona ni sauti ya nani aliyekuwa akiongea nami, na nilipogeuka niliona kinara cha dhahabu cha taa saba.
Je me suis retourné pour voir la voix qui me parlait. Et je me retournai, et je vis sept chandeliers d'or.
13 Katikati ya kinara cha taa alikuwemo mmoja kama Mwana wa Adamu, amevaa kanzu ndefu iliyofika chini ya miguu yake, na mkanda wa dhababu kuzunguka kifua chake.
Et parmi les chandeliers, il y en avait un qui ressemblait à un fils d'homme, vêtu d'une robe qui lui descendait jusqu'aux pieds, et d'une ceinture d'or autour de sa poitrine.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe kama theluji, na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
Sa tête et ses cheveux étaient blancs comme de la laine blanche, comme de la neige. Ses yeux étaient comme une flamme de feu.
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana, kama shaba ambayo imekwisha pitishwa katika moto, na sauti yake ilikuwa kama sauti ya maji mengi yanayotiririka kwa kasi.
Ses pieds étaient semblables à de l'airain poli, comme s'il avait été affiné dans une fournaise. Sa voix était comme le bruit des grandes eaux.
16 Alikuwa ameshikilia nyota saba katika mkono wake wa kuume, na kutoka kinywani mwake kulikuwa na upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa uking'aa kama mwanga mkali wa jua.
Il avait sept étoiles dans sa main droite. De sa bouche sortait une épée aiguë à deux tranchants. Son visage était comme le soleil brillant à son plus haut degré.
17 Nilipomwona, nikaanguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kulia juu yangu na kusema, “Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa Mwisho,
Quand je le vis, je tombai à ses pieds comme un mort. Il posa sa main droite sur moi, en disant: « N'aie pas peur. Je suis le premier et le dernier,
18 na ambaye ninaishi. Nalikuwa nimekufa, lakini tazama, ninaishi milele! Na ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn g165, Hadēs g86)
et le Vivant. J'étais mort, et voici que je suis vivant pour les siècles des siècles. Amen. J'ai les clés de la mort et du séjour des morts. (aiōn g165, Hadēs g86)
19 Kwa hiyo, yaandike uliyoyaona, yaliyopo sasa, na yale yatakayotokea baada ya haya.
Écris donc les choses que tu as vues, les choses qui sont, et les choses qui arriveront dans la suite.
20 Kwa maana iliyojificha kuhusu nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na kile kinara cha dhahabu cha taa saba: nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, na kinara cha taa saba ni yale makanisa saba.”
Voici le mystère des sept étoiles que tu as vues dans ma main droite, et des sept chandeliers d'or: Les sept étoiles sont les anges des sept assemblées. Les sept chandeliers sont les sept assemblées.

< Ufunuo 1 >