< Zaburi 92 >

1 Ni jambo jema kumshukuru Yahwe na kuliimbia sifa jina lako, Uliye Juu,
Psalmus Cantici, In die Sabbati. Bonum est confiteri Domino: et psallere nomini tuo Altissime.
2 kutangaza uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi na uaminifu wako kila usiku,
Ad annunciandum mane misericordiam tuam: et veritatem tuam per noctem.
3 kwa kinubi cha nyuzi kumi na kwa tuni ya kinubi.
In decachordo, psalterio: cum cantico, in cithara.
4 Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
Quia delectasti me Domine in factura tua: et in operibus manuum tuarum exultabo.
5 Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
Quam magnificata sunt opera tua Domine! nimis profundæ factæ sunt cogitationes tuæ:
6 Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
Vir insipiens non cognoscet: et stultus non intelliget hæc.
7 Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
Cum exorti fuerint peccatores sicut fœnum: et apparuerint omnes, qui operantur iniquitatem: Ut intereant in sæculum sæculi:
8 Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
tu autem Altissimus in æternum Domine.
9 Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
Quoniam ecce inimici tui Domine, quoniam ecce inimici tui peribunt: et dispergentur omnes, qui operantur iniquitatem.
10 Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
Et exaltabitur sicut unicornis cornu meum: et senectus mea in misericordia uberi.
11 Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
Et despexit oculus meus inimicos meos: et in insurgentibus in me malignantibus audiet auris mea.
12 Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
Iustus ut palma florebit: sicut cedrus Libani multiplicabitur.
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
Plantati in domo Domini, in atriis domus Dei nostri florebunt.
14 Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
Adhuc multiplicabuntur in senecta uberi: et bene patientes erunt,
15 kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.
ut annuncient: Quoniam rectus Dominus Deus noster: et non est iniquitas in eo.

< Zaburi 92 >