< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
Laus Cantici David. Qui habitat in adiutorio Altissimi, in protectione Dei cæli commorabitur.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
Dicet Domino: Susceptor meus es tu, et refugium meum: Deus meus sperabo in eum.
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
Quoniam ipse liberavit me de laqueo venantium, et a verbo aspero.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
Scapulis suis obumbrabit tibi: et sub pennis eius sperabis:
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
Scuto circumdabit te veritas eius: non timebis a timore nocturno,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
A sagitta volante in die, a negotio perambulante in tenebris: ab incursu, et dæmonio meridiano.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
Cadent a latere tuo mille, et decem millia a dextris tuis: ad te autem non appropinquabit.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Verumtamen oculis tuis considerabis: et retributionem peccatorum videbis.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Quoniam tu es Domine spes mea: Altissimum posuisti refugium tuum.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
Non accedet ad te malum: et flagellum non appropinquabit tabernaculo tuo.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
Quoniam angelis suis mandavit de te: ut custodiant te in omnibus viis tuis.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
In manibus portabunt te: ne forte offendas ad lapidem pedem tuum.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
Super aspidem, et basiliscum ambulabis: et conculcabis leonem et draconem.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
Quoniam in me speravit, liberabo eum: protegam eum, quoniam cognovit nomen meum.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
Clamabit ad me, et ego exaudiam eum: cum ipso sum in tribulatione: eripiam eum et glorificabo eum.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
Longitudine dierum replebo eum: et ostendam illi salutare meum.

< Zaburi 91 >