< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
El que mora al abrigo del ʼElyón Morará bajo la sombra del Shadday.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
Diré yo a Yavé: ¡Refugio mío y Fortaleza mía, Mi ʼElohim, en Quien confío!
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
Él te librará de la trampa del cazador, Y de la mortal pestilencia.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
Con sus plumas te cubrirá, Y debajo de sus alas te refugiarás. Escudo y adarga es su verdad.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
No temerás el terror nocturno, Ni a flecha que vuele de día,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
Ni a pestilencia que ande en [la] oscuridad, Ni a mortandad que a mediodía destruya.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
Caerán a tu lado 1.000, Y 10.000 a tu mano derecha, Pero a ti no llegará.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Ciertamente mirarás con tus ojos, Y verás la recompensa de los perversos.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Por cuanto pusiste a Yavé, mi Refugio, A ʼElyón como tu Lugar de morada,
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
No te vendrá mal, Ni alguna plaga tocará tu morada.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
Pues a sus ángeles mandará con respecto a Ti, Que te guarden en todos tus caminos.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
En sus manos te llevarán Para que tu pie no tropiece en piedra.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
Sobre el león y el áspid pisarás. Pisotearás al cachorro de león y al dragón.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
Me amó, Por tanto Yo lo libraré. Lo pondré en alto, Porque conoció mi Nombre.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
Me invocará Y Yo le responderé. Estaré con él en la angustia. Lo libraré y lo glorificaré.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
Lo saciaré de larga vida y le mostraré mi salvación.

< Zaburi 91 >