< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
O thou that dwellest in the covert of the Most High, and abidest in the shadow of the Almighty;
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
I will say of the LORD, who is my refuge and my fortress, my God, in whom I trust,
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
That He will deliver thee from the snare of the fowler, and from the noisome pestilence.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
He will cover thee with His pinions, and under His wings shalt thou take refuge; His truth is a shield and a buckler.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
Thou shalt not be afraid of the terror by night, nor of the arrow that flieth by day;
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
Of the pestilence that walketh in darkness, nor of the destruction that wasteth at noonday.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
A thousand may fall at Thy side, and ten thousand at Thy right hand; it shall not come nigh thee.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Only with thine eyes shalt thou behold, and see the recompense of the wicked.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
For thou hast made the LORD who is my refuge, even the Most High, thy habitation.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
There shall no evil befall thee, neither shall any plague come nigh thy tent.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
For He will give His angels charge over thee, to keep thee in all thy ways.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
They shall bear thee upon their hands, lest thou dash thy foot against a stone.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
Thou shalt tread upon the lion and asp; the young lion and the serpent shalt thou trample under feet.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
'Because he hath set his love upon Me, therefore will I deliver him; I will set him on high, because he hath known My name.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
He shall call upon Me, and I will answer him; I will be with him in trouble; I will rescue him, and bring him to honour.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
With long life will I satisfy him, and make Him to behold My salvation.'

< Zaburi 91 >