< Zaburi 8 >

1 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote, wewe ufunuaye utukufu wako juu mbinguni.
To the Overseer, 'On the Gittith.' A Psalm of David. Jehovah, our Lord, How honourable Thy name in all the earth! Who settest thine honour on the heavens.
2 Kutoka katika midomo ya watoto na vichanga umeumba sifa kwa sababu ya utukufu wako, ili kuwanyamazisha maadui wote na walipa kisasi wote.
From the mouths of infants and sucklings Thou hast founded strength, Because of Thine adversaries, To still an enemy and a self-avenger.
3 Ninapozitazama mbingu, ambazo vidole vyako vimeumba, mwezi na nyota, ambazo umeziweka kila mmoja katika nafasi yake,
For I see Thy heavens, a work of Thy fingers, Moon and stars that Thou didst establish.
4 Binadamu ni nani hata umtazame, na watu hata uwajali wao?
What [is] man that Thou rememberest him? The son of man that Thou inspectest him?
5 Umewaumba chini kidogo kuliko viumbe vya mbinguni na umewazunguka na utukufu na heshima.
And causest him to lack a little of Godhead, And with honour and majesty compassest him.
6 Umemfanya binadamu kutawala kazi ya mikono yako; umeviweka vitu vyote chini ya miguu yake:
Thou dost cause him to rule Over the works of Thy hands, All Thou hast placed under his feet.
7 kondoo na ng'ombe wote, na hata wanyama wa porini,
Sheep and oxen, all of them, And also beasts of the field,
8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, na vyote vipitavyo katika mikondo ya bahari.
Bird of the heavens, and fish of the sea, Passing through the paths of the seas!
9 Yahweh Bwana wetu, ni jinsi gani jina lako ni tukufu katika dunia yote!
Jehovah, our Lord, How honourable Thy name in all the earth!

< Zaburi 8 >