< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Dost thou draw leviathan with an angle? And with a rope thou lettest down — his tongue?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Dost thou put a reed in his nose? And with a thorn pierce his jaw?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Doth he multiply unto thee supplications? Doth he speak unto thee tender things?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Doth he make a covenant with thee? Dost thou take him for a servant age-during?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Dost thou play with him as a bird? And dost thou bind him for thy damsels?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
(Feast upon him do companions, They divide him among the merchants!)
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Dost thou fill with barbed irons his skin? And with fish-spears his head?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Place on him thy hand, Remember the battle — do not add!
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Lo, the hope of him is found a liar, Also at his appearance is not one cast down?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
None so fierce that he doth awake him, And who [is] he before Me stationeth himself?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Who hath brought before Me and I repay? Under the whole heavens it [is] mine.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
I do not keep silent concerning his parts, And the matter of might, And the grace of his arrangement.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who hath uncovered the face of his clothing? Within his double bridle who doth enter?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
The doors of his face who hath opened? Round about his teeth [are] terrible.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
A pride — strong ones of shields, Shut up — a close seal.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
One unto another they draw nigh, And air doth not enter between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
One unto another they adhere, They stick together and are not separated.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
His sneezings cause light to shine, And his eyes [are] as the eyelids of the dawn.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Out of his mouth do flames go, sparks of fire escape.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Out of his nostrils goeth forth smoke, As a blown pot and reeds.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath setteth coals on fire, And a flame from his mouth goeth forth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
In his neck lodge doth strength, And before him doth grief exult.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The flakes of his flesh have adhered — Firm upon him — it is not moved.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart [is] firm as a stone, Yea, firm as the lower piece.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
From his rising are the mighty afraid, From breakings they keep themselves free.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
The sword of his overtaker standeth not, Spear — dart — and lance.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
He reckoneth iron as straw, brass as rotten wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The son of the bow doth not cause him to flee, Turned by him into stubble are stones of the sling.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
As stubble have darts been reckoned, And he laugheth at the shaking of a javelin.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Under him [are] sharp points of clay, He spreadeth gold on the mire.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He causeth to boil as a pot the deep, The sea he maketh as a pot of ointment.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
After him he causeth a path to shine, One thinketh the deep to be hoary.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
There is not on the earth his like, That is made without terror.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Every high thing he doth see, He [is] king over all sons of pride.

< Ayubu 41 >