< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Pesem ukovita Asafova. Poslušaj, ljudstvo moje, nauk moj; nagnite uho svoje govoru mojih ust.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
V priliki odprem usta svoja; od sebe dam skrivnosti časov nekdanjih,
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Kar smo slišali in znali, ko so nam pravili pradedje naši.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
Prikrivali ne bodemo njih otrokom, naslednjemu rodu, da oznanjajo hvalo Gospodovo in moč njegovo, in čudovita dela njegova, katera je storil.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Ker ustanovil je pričanje v Jakobu in postavil zakon v Izraelu, ko je zapovedal pradedom našim, oznanjati svojim otrokom.
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
Da vedó, naslednji rod, otroci prihodnji, in vstanejo ter oznanjajo otrokom svojim.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
Upanje svoje naj stavijo v Boga, in ne pozabijo naj dejanj Boga mogočnega, temuč hranijo naj zapovedi njegove.
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
In ne bodejo naj kakor njih pradedje, rod trdovraten in uporen; rod, kateri ni popravil srca svojega, in katerega duh ni bil stanoviten proti Bogu mogočnemu,
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
Kakor nasledniki Efrajmovi, kateri oboroženi streljajo z lokom in hrbte obračajo ob času bitve.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Ohranili niso zaveze Božje, in branili so se hoditi po zakonu njegovem,
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
Pozabivši dejanj njegovih, in čudovitih del njegovih, katera jim je bil pokazal.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Pred pradedi njihovimi je delal čuda, v deželi Egiptovski, na polji Taniškem.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Razklal je bil morje, da jih je prepeljal čez, in postavil je vode, kakor kùp.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
In spremljal jih je z oblakom podnevi, in vso noč sè svetlim ognjem.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Razklal je bil skale v puščavi, da bi pijačo pripravil v valovih preobilo.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Valove je izpeljal iz skale, in vode dol spuščal kakor reke.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Vendar so dalje grešili še zoper njega, in dražili Najvišjega v sami suhi deželi.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
In izkušajoč Boga mogočnega v srci svojem, térjali so jedi po svojega srca želji.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
In grdo govoreč zoper Boga, rekli so: "Ali bi mogel Bog mogočni napraviti mizo v tej puščavi?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Glej, tako je udaril skalo, da so tekle vode, in potoki so se udrli, ali bi mogel dati tudi živeža? ali bi pripravil mesa svojemu ljudstvu?"
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Zato je Gospod slišal in se razjaril; in ogenj se je bil vnel zoper Jakoba, in jeza je tudi gorela zoper Izraela.
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
Ker niso verovali v Boga, in niso zaupali v blaginjo njegovo.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
Dasi je bil zapovedal gornjim oblakom zgoraj in odprl vrata nebeška,
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
In dežil nad nje máno za jed in dajal žito nebeško;
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Kruh najmočnejših je jedel vsak; popotnico jim je pošiljal do sitega.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Zagnal je sever na nebesih, in z močjo svojo pripeljal jug.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
Ko je dežil nad nje meso kakor prah, in kakor morski pések tiče krilate;
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
Metal jih je med šatore, okolo prebivališč svojih.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
In jedli so in bili so nasiteni močno, in česar so poželeli, prinesel jim je.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Še niso bili iznebili se poželenja svojega, še je bila jed njih v njihovih ustih;
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
Ko je jeza Božja goreča proti njim morila med najmočnejimi iz med njih in pokončavala mladeniče Izraelske.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Po vsem tem so še grešili in niso verovali zavoljo čudovitih dél njegovih.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Zatorej je pogubljal v ničemurnosti njih dní, in njih leta v strahu.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Ko jih je pobijal, ako so popraševali po njem in izpreobrnivši se zjutraj iskali Boga mogočnega,
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
Spomnivši se, da je bil Bog njih skala in Bog mogočni najvišji njih rešnik;
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Če tudi so ga hoteli varati z usti svojimi, in so z jezikom svojim lagali se njemu,
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
In srce njihovo ni bilo obrneno proti njemu, in niso bili stanovitni v zavezi njegovi:
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Vendar je on usmiljen opíral krivico, tako da jih ni pogubil; in odvračal je svoj srd obilo, in ní vnemal vse jeze svoje,
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Spomnivši se, da so meso, veter, ki gre in se ne vrne.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Kolikokrat so ga razdražili v puščavi; žalili so ga v samoti!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
Ki so hitro izkušali Boga mogočnega, in žalili Svetega Izraelovega.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Ne spomnivši se roke njegove, dné, ko jih je bil otél sovražnika.
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
Ko je v Egiptu delal znamenja svoja, in čuda svoja na polji Taniškem.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
Ko je v kri izpremenil njih potoke, in reke njih, da bi ne mogli piti.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
Izpustil je nad njé živali krdelo, da bi jih pokončalo, in žabe, da jih uničijo.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
In dal je njih sad murnu in kobilici njih delo.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
Pobil je s točo njih trte in smokve njih z ognjem, ki je pokončal vse, kamor je prišel.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
Dal je tudi isti toči njih živali, in njih čede žarjavici ognjeni.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Izpustil je nad nje jeze svoje žar, srd in nevoljo in stisko, pošiljajoč oznanovalce nesreče.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Pretehtal je k jezi svoji pot, smrti ni ubranil njih življenja; in živali njih izročil je kugi.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
In udaril je vse prvorojeno v Egiptu; prvino moči v šatorih Kamovih.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
In prepeljal je kakor ovce ljudstvo svoje, in vodil jih je kakor čede po puščavi.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
In peljal jih je varno tako, da se niso bali, potem ko je bilo morje pokrilo njih sovražnike.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Pripeljal jih je do meje svetosti svoje, gore té, katero je pridobila desnica njegova.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
Izgnal je izpred njih obličja narode in storil, da so pripali vrvi posesti in prebivali so v njih šatorih Izraelovi rodovi.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
Vendar so izkušali in razdražili Boga najvišjega, in pričanj njegovih niso se držali.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Temuč obrnili so se ter ravnali izdajalsko, kakor njih pradedje; obrnili so se kakor lok goljufen,
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Ker dražili so ga z višinami svojimi in svojimi maliki, do ljubosumnosti so ga razvneli.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Slišal je Bog in se razsrdil, in zavrgel je silno Izraela.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
Tako, da je zapustivši prebivališče v Silu, šator, katerega je bil postavil med ljudmi,
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
Dal v sužnjost svojo moč, in slavo svojo sovražniku v pest.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
In izročil je meču ljudstvo svoje, ker se je bil razsrdil zoper posestvo svoje.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Ogenj je pokončal mladeniče njegove, in device njegove niso se hvalile.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
Duhovniki njegovi padli so pod mečem, in vdove njegove niso jokale.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Potem se je zbudil Gospod, kakor da bi bil spal, kakor korenjak, pojoč po vinu.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
In udaril je sovražnike svoje nazaj; sramoto večno jim je naložil.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Slednjič je zavrgel šator Jožefov in rodú Efrajmovega ni izvolil.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
Izvolil pa je rod Judov, goro Sijonsko, da bi jo ljubil.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Zidal je enako najvišjim gradovom svetišče svoje, namreč v deželi, katero je utrdil.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
In izvolil je Davida hlapca svojega, in vzel ga iz ograje čede,
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
Peljal ga je od doječih, da bi pasel Jakoba, ljudstvo svoje in Izraela, posestvo svoje,
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Kateri jih je pasel po poštenosti srca svojega, in vodil jih je z najvišjo razumnostjo svojih rok.

< Zaburi 78 >